Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:37:40 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Tambi (spaghetti 1/2 ya packet) Mafuta (vegetable oil) Sukari (sugar 1/2 kikombe cha chai) Hiliki (cardamon 1/2 kijiko cha chai) Chumvi (salt 1/2 kijiko cha chai) Tui la nazi (coconut oil 1 kikombe cha chai) Maji kiasi
Matayarisho
Tia mafuta kiasi kwenye sufuria kisha ibandike jikoni (katika moto wa wastani) yakisha pata moto kiasi tia tambi na uanze kuzikaanga kwa kuzigeuzageuza kila mara mpaka zitakapokuwa za yangi ya light brown. baada ya hapo ipua na umwage mafuta ya kwenye tambi (bakiza kidogo sana kwani usipofanya hivyo tambi zitakuwa na mafuta sana) Baada ya hapo zirudishe jikoni na kisha utie hiliki, chumvi, sukari, tui la nazi na maji kiasi. Zifunike kisha ziache zichemke mpaka maji yakauke. Baada ya hapo zigeuze na uzipike mpaka ziive. Nahapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:48 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Makongoro (miguu ya ng'ombe) kiasi Limao 1 kubwa Kitunguu swaum Tangawizi Chumvi Pilipili
Matayarisho
Safisha makongoro kisha yatie kwenye pressure cooker. Kisha tia kitunguu swaum, tangawizi, chumvi,limao na maji kiasi. Baada ya hapo yachemshe mpake yaive na yawe malaini na pia ubakize supu kiasi inaweza kuchukua kama dk 45 au saa 1 hivi. Baada ya hapo yaipue na upakue supu yako kwenye bakuli katia pilipili kiasi kisha itakuwa tayari kwa kuliwa.
Note: Ukiwa unanunua makongoro hakikisha unachukuwa yale yasiyokuwa na manyoya na pia hakikisha usiyachemshe kupitiliza kwani yakiwa malaini sana utashindwa kuyaenjoy.
Jinsi ya kutengeneza biskuti za Matunda Makavu Na Cornflakes
Updated at: 2024-05-25 10:23:08 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga - 4 Vikombe
Sukari - 1 Kikombe
Baking powder 1 kijiko cha chai mfuto
Siagi - 454 gms
Mayai - 2
Matunda makavu (tende, zabibu, lozi) - 1 Kikombe
Vanilla - 2 Vijiko vya chai
Cornflakes - ½ kikombe
JINSI YA KUANDAA
Changanya sukari na siagi katika mashine ya keki (cake mixer) mpaka iwe laini (creamy) Tia yai moja moja huku unachanganya mpaka iwe laini kama sufi. (fluffy) Tia unga, baking powder, matunda makavu, changanya na mwiko. Chota mchanganyiko wa biskuti kwa mkono kama (kiasi cha kijiko kimoja cha supu) fanya duara na uchovye katika cornflakes iliyopondwa kwa mkono (crushed) Zipange katika treya ya kupikia na zipike (bake) katika moto wa 375°F kwa muda wa kiasi dakika 15 huku unazitazama tazama.
Updated at: 2024-05-25 10:34:44 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Blue band vijiko vikubwa 2 Maziwa vikombe 2 Royco kijiko kikubwa 1-2 Pilipili manga (unga) kijiko cha 1 Chumvi kiasi Maji lita 2-3 Boga kipande ½ Viazi mviringo 2 Vitunguu 2 Karoti 2 Nyanya 2
Hatua
• Menya boga, viazi, karoti, nyanya na kwaruza weka kwenya sufuria kubwa. • Menya, osha na katakata vitunguu kisha ongeza kwenye mboga. • Ongeza maji na chumvi chemshwa mpaka vilainike. • Pekecha ikiwa jikoni na moto kidogo • Ongeza blue band, maziwa royco na pilipili manga ukikoroga kwa dakika 5. • Onja chumvi na pakua kama supu. Uwezekano Tumia siagi badala ya margarine.
Updated at: 2024-05-25 10:37:41 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Maini ya kuku 1/2 kilo Vitunguu vikubwa 2 Hoho 1 Pilipil 1 Limao 1/2 Swaum/tangawizi 1 kijiko cha chai Curry powder 1/2 kijiko cha chai Mafuta ya kupikia
Matayarisho
Safisha maini weka pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu,swaum na tangawizi pamoja (hakikisha vitunguu visiwe vya brown), kisha tia maini, curry powder, pilipili, chumvi ,hoho na limao kisha changanya vizuri na ufunike. Pika mpaka maini yaive na hakikisha yanakuwa na rojo kidogo. Baada ya hapo ipua na yatakuwa tayari kwa kuliwa na chochote upendacho kama vile chapati, chips, ugali, wali.
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele - 2 Mugs
Mboga mchanganyiko za barafu (Frozen veg) - Mug
Tuna (samaki/jodari) - 2 kopo
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi -2 vijiko vya supu
Garam masala - 1 kijiko cha supu
Nyanya - 2
Kitungu maji - 1
Mdalasini nzima - 2 vijiti
Karafuu - 6 chembe
Pilipili mbichi - 1
Chumvi - kiasi
Viazi - 3
Maji - 2 ½ Mugs
Mafuta - 3 vijiko vya supu
Maandalizi
Osha mchele na uroweke kwa muda wa dakika 20 Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown). Mimina viazi, thomu na tangawizi, bizari zote na kaanga. Tia nyanya uliyokatakata ikaange mpaka iwive. Tia tuna endelea kukaanga kidogo tu. Tia maji, yatakapochemka tia mchele. Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa ½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Mchele wa pishori (basmati) - 4
Vitunguu katakata - 3
Nyanya (tungule) katakata vipande vikubwa - 3 -5
Pilipili boga la kijani (capsicum) katakata
Supu ya kitoweo au vidonge vya supu - 1
Bizari mchanganyiko Garama masala - 5-7
Pilipili mbichi ya kusaga - Kiasi
Zaafarani ya maji (flavor) - 1 kijiko cha chakula
Mafuta ya kupikia - ¼ kikombe
Samaki wa kukaanga
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Roweka mchele kiasi nusu saa kisha chemsha mchele kwa supu uive nusu kiini. Mwaga maji chuja. Wakati mchele unapikika, weka mafuta katika sufuria kubwa ya kupikia wali, kaanga vitunguu mpaka vigeuke rangi ya hudhurungi. Tia nyanya na vitu vinginevyo vyote kaanga kidogo tu. Mwaga wali katika sufuria na nyunyizia zaafarani kisha changanya na masala vizuri. Funika upike katika oven (bake) au juu ya stovu moto mdogo mdogo kiasi dakika 15- 20. Epua ikiwa tayari, pakua kwenye sahani kisha tolea kwa samaki wa kukaanga.
Mapishi ya Chai ya maziwa, mandazi, uyoga na mayai
Updated at: 2024-05-25 10:22:58 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mandazi (angalia jinsi ya kupika katika recipe ya mandazi ya nyuma) Uyoga (mashroom kikombe 1 cha chai) Mayai (eggs 4) Hoho (greenpepper 1/4 ya hoho) Nyanya (fresh tomato 1) Kitunguu (onion 1/4 ya kitunguu) Chumvi (salt) Mafuta (vegetable oil) Hiliki nzima (cardamon 4) Masala ya chai (tea masala 1 kijiko cha chai) Pilipili mtama iliyosagwa (ground black pepper 1/4 ya kijiko cha chai) Maziwa (fresh milk 1 kikombe cha chai) Majani ya chai (tea leaves) Maji kiasi. Sukari (sugar)
Matayarisho
Jinsi ya kupika chai, weka maziwa, maji kiasi,hiliki, masala ya chai, pilipili mtama na majani katika sufuria. Chemsha kwa muda wa dakika 10 na chai itakuwa tayari. Jinsi ya kupika mayai, weka mafuta kiasi katika fry pan na utie vitunguu, vikaange kidogo kisha tia nyanya, chumvi na hoho. Pika kwa muda wa dakika 4 kisha tia mayai na uyaache yaive mpaka yakauke kisha geuza upande wa pili na uyapike mpaka ya ive kisha ipua. Jinsi ya kupika uyoga, weka mafuta kidogo katika fry pan kisha tia uyoga na chumvi na ukaange mpaka uive katika moto wa wastani. Ukisha iva breakfast yako itakuwa teyari kwa kuseviwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:47 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Nyama ya ng'ombe (beef 1/2 kilo) Mchele (rice 1/2 kilo) Vitunguu (onion 2) Viazi (potato 2) Vitunguu swaum (garlic 3 cloves) Tangawizi (ginger) Nyanya ya kopo (tomato 1/2 ya tin) Curry powder (1/2 kijiko cha chai) Binzari nyembamba ya kusaga (cumin 1/2 kijiko cha chai) Binzari manjano (tarmaric 1/2 kijiko cha chai) Mafuta (vegetable oil) Chumvi (salt) Rangi ya chakula (food colour) Giligilani (fresh coriander) Maziwa ya mgando (yogurt kikombe 1 cha chai) Hiliki nzima (cardamon 3cloves) Karafuu (clove 3) Pilipili mtama nzima (black pepper 5) Amdalasini (cinamon stick 1)
Matayarisho
Katakata nyama kisha ioshe na uiweke kwenye sufuria kisha tia kitunguu swaum, tangawizi, nyanya, curry powder, binzari zote, chumvi na maziwa ya mgando kisha bandika jikoni ichemke mpaka nyama iive na mchuzi ubakie kidogo.Baada ya hapo kaanga viazi na uweke pembeni, kisha kaanga vitunguu na mafuta mpaka viwe ya brown na kisha uvitie viazi vitunguu, na mafuta yake katika nyama. Koroga na uache uchemke kidogo kisha ipua na utie fresh coriander iliyokatwa na hapo mchuzi wako utakuwa tayari. Baada ya hapo loweka mchele wako kwa muda wa dakika 10, kisha chemsha maji yatie chumvi, hiliki, karafuu, pilipili mtama na abdalasin na mafuta. Yakisha chemka tia mchele na uache uchemke mpaka ukauke maji yakisha kauka tia rangi ya chakula na uanze kugeuza ili ichanganyike na wali wote. Baada ya hapo ufunike na uache mpaka uive. Na baada ya hapo biriani litakuwa tayari kwa kuliwa.