Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, APRILI 1, 2022: IJUMAA, JUMA LA 4 LA KWARESIMA

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

ย 

SOMO 1


Hek. 2:1, 12-22

Wasiomsadikia Mungu walisema hivi, huku wakimfikiri yasiyo kweli, Zaidi ya hayo na tumwotee mtu wa haki, maana hatuna haja naye, naye yu kinyume cha matendo yetu; atukaripia ya kama tumeiasi torati, na kutushitaki ya kama tumekosa adabu. Asema ya kwamba anamjua Mungu, na kujiita mtumishi wa Bwana. Ametuwia magombezi ya fikira zetu. Hata kumtazama twaona ni kugumu; maan amaisha yake si sawasawa na masiha ya wengine, na mwenendo wake ni wa kigeni. Tuanhesabiwa naye kuwa kama madini hafifu; anajitenga na njia zetu kama na uchafu. Wenye haki asema kuwa mwisho wao ni heri; hujivuna ya kwamba Mungu ndiye baba yake.
Haya na tuone kama maneno yake ni kweli; tufanye kujaribu yatakayompata wakati wa mwisho wake; mradi mwenye haki akiwa ni mwana wa Mungu, Yeye atamtegemeza na kumwokoa mikononi mwa adui zake. Na tumhakikishe kwa jeuri na maumivu, ili tujifunze upole wake na kuithibitisha saburi yake akidhulumiwa. Hata tumhukumu auawe mauti ya aibu, maana ataangaliwa sawasawa na maneno yake.
Ndivyo walivyosemezana, wakakosea kabisa. Kwa maana uovu wao uliwapofusha; hawakuzijua siri za Mungu; wala hawakuutarajia mshahara wa utakatifu, wala kudhani ya kwamba iko thawabu kwao wenye roho zisizo na hatia.

Neno la Bwanaโ€ฆ Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI


Zab. 34:16-20, 22 (K) 18

ย 

(K) Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo.

Uso wa Bwan ani juu ya watenda mabaya,
Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
Walilia, naye Bwan akasikia,
Akawaponya na taabu zao zoe. (K)

Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo,
Na waliopondeka roho huwaokoa.
Mateso ya mwenye haki ni mengi,
Lakini Bwana humponya nayo yote. (K)

Huihifadhi mifupa yake yote,
Haukuvunjika hata mmoja.
Bwana huzikombo a nafsi za watumishi wake,
Wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao. (K)

SHANGILIO


Lk. 8:15


Heri wale walishikao neno la Mungu katika moyo wao mwema na mnyofu, na wazaao matunda katika uvumilivu.

INJILI


Yn. 7:1-2, 25-30

Baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya; maana hakutaka kutembea katika Uyahudi, kwa sababu Wayahudi walikuw awakitafuta kumwua.
Na sikukuu ya Wayahudi, Sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu. Hata ndugu zake walipokwisha kukwea kuiendea sikukuu, ndipo yeye naye laipokwea, si kwa wazi bali kana kwamba kwa siri.
Basi baadhi ya watu wa yerusalemu wakasema, Je! Huyu siye wanayemtafuta ili wamwue? Na kumbe! Anena waziwazi, wala hawamwambii neno! Yamkini hao wakuu tuna jua hakika ya kuwa huyu ndiye Kristo? Lakini huyu twamjua atokako; bali Kristo atakapokuja hakuna ajuaye atokako.
Basi Yesu akapaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, Mimi mnanijua, na huko nitokako mnakujua; wala sikuja kwa nafsi yangu; ila yeye aliyenipeleka ni wa kweli, msiyemjua ninyi. Mimi namjua, kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.
Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyeunyosha mkono wake ili kumshika, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Majaliwa Guest Jun 26, 2024
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Monica Adhiambo Guest Apr 8, 2024
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mtei Guest Dec 24, 2023
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Andrew Odhiambo Guest Sep 30, 2023
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Henry Mollel Guest Jul 11, 2023
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Rose Amukowa Guest May 14, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Lucy Wangui Guest Apr 17, 2023
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Daniel Obura Guest Mar 29, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Lucy Wangui Guest Dec 6, 2022
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Samson Mahiga Guest Nov 8, 2022
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Joyce Mussa Guest Oct 12, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Josephine Nekesa Guest Sep 8, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Charles Mboje Guest Aug 25, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Irene Akoth Guest Jul 14, 2022
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Susan Wangari Guest Jun 4, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Joy Wacera Guest Jun 2, 2022
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ John Mushi Guest Jan 21, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Vincent Mwangangi Guest Jan 4, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Joy Wacera Guest Aug 27, 2021
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Samuel Omondi Guest May 26, 2021
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Frank Macha Guest May 5, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Ruth Kibona Guest Jan 26, 2021
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Mariam Kawawa Guest Jan 22, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Stephen Kangethe Guest Jan 12, 2021
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Alice Wanjiru Guest Oct 9, 2020
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ George Ndungu Guest Jun 17, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Faith Kariuki Guest Apr 6, 2020
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ George Ndungu Guest Feb 1, 2020
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ James Mduma Guest Jan 28, 2020
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kitine Guest Jan 8, 2020
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Janet Mbithe Guest Sep 27, 2019
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Susan Wangari Guest Aug 17, 2019
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Peter Otieno Guest Jun 5, 2019
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Martin Otieno Guest Apr 14, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Josephine Nduta Guest Apr 7, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Emily Chepngeno Guest Feb 1, 2019
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Violet Mumo Guest Sep 4, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Francis Mrope Guest Jun 22, 2018
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Esther Nyambura Guest Oct 7, 2017
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Jackson Makori Guest Jun 21, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ James Kimani Guest Dec 9, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Peter Tibaijuka Guest Oct 9, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Frank Sokoine Guest Sep 25, 2016
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ John Lissu Guest Sep 5, 2016
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ George Ndungu Guest Jul 27, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Joseph Mallya Guest Jul 14, 2016
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Andrew Odhiambo Guest Mar 16, 2016
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Diana Mallya Guest Nov 18, 2015
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Oct 3, 2015
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Kevin Maina Guest Jun 25, 2015
Kwa Mungu, yote yanawezekana

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About