Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

Soma stori hii, unaweza ukajifunza kitu

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Kijana mmoja alisafiri kwa meli na rafiki zake,
wakiwa katikati ya safari yao meli ilianza
kuzama. Watu wengi pamoja na rafiki wa yule
kijana walikufa maji wakati wanajaribu kujiokoa
kwa kuogelea, lakini yule kijana alifanikiwa

kushika ubao ulioelea majini akaanza kuelea nao,
maji yalimpeleka hadi kisiwa cha mbali sana
ambako hakukuwa na watu wala wanyama
isipokuwa wadudu tu! Alifika ufukweni amechoka
sana na asiyeamini tukio lililotokea, akaishi huko
kwa kula matunda. Aliweza kujenga ka-kibanda
kwa shida sana maana hakuwa na shoka wala
panga, hatimaye akaanza maisha mapya.
Aliishi muda mrefu kisiwani na tayari alishazoea
mazingira yale ya shida japo shida haizoeleki.
Mara zote nyakati za jioni aliwasha moto kwa
kupekecha vijiti. Siku moja kama kawaida yake
aliwasha moto nje karibu na kibanda chake, aliota
moto muda mrefu hatimaye akapitiwa na usingizi.
Alilala hapo hapo hadi usiku wa manane
aliposhtushwa na joto kali lisilo la kawaida.
Kumbe moto ulishika nyasi za kibanda chake na
kibanda chote kikaungua moto.Alilia sana na
kumlaani sana Mungu kwa mateso hayo akisema
"Hivi Mungu nimekukosea nini mpaka unitese
hivi? Pamoja na shida zote hizi bado
unaniongezea shida nyingine, umeteketeza makazi
yangu ilhali nimejenga kwa shida, Hukuridhika
kunitenga mbali na familia yangu nilipoishi kwa
raha? Hukuridhika kuwaua rafiki zangu wote
baharini? Kwanini Mungu umekuwa mkatili hivi?
Bora nife tuu maana nimeshachoshwa na hizi
shida!" akaendelea kulalamika na kumlaani Mungu
hadi kukapambazuka.
Ilipofika asubuhi aliiona meli ikija kwa mbali
kuelekea alipo, alishangaa maana hakuna meli
yoyote inayoweza kwenda kisiwa kile labda kama
imepotea njia. Meli ilipofika ufukweni yule kijana
akaifuata, alienda moja kwa moja hadi kwa
kapteni.Kapteni akamwambia "tuliona moto mkali
sana usiku tukahisi ni meli inawaka moto
tukasema tuje ili tutoe msaada..kwa kweli
tumetembea masaa mengi sana hadi kufika hapa,
mshukuru Mungu maana ametumia moto kutuleta
hapa" yule kijana kusikia hivyo alilia sana,
akajilaumu kwa jinsi alivyo mnung'unikia Mungu.
Akaelewa kuwa Mungu ana njia nyingi za kuleta
msaada kwa mtu. Akapiga magoti akatubu huku
akimshukuru Mungu. Safari ya kurudi nyumbani
ikaanza.
FUNDISHO: Wakati mwingine Kuna mambo
mabaya huwa yanatokea katika maisha yetu
yanayotufanya tuone kama Mungu ametusahau.
Tunamnung'unikia na kumlaumu Mungu bila
kujua kuwa Mungu ana njia nyingi sana kutuletea
msaada. Njia za Mungu huwa zinaonekana kama
ujinga fulani, lakini kiukweli ujinga wa Mungu
ndiyo akili kubwa ya mwisho ya mwanadamu.
Tunasahau kuwa mabaya tunayokutana nayo
yanafanya kazi kwa Manufaa ya hatma zetu.
Unaweza fukuzwa kazi usijue kumbe ndio
unaelekea katika kazi bora zaidi, unaweza
kuachwa na mtu uliyempenda sana ukadhani
ndiyo mwisho wa maisha kumbe Mungu
amekuandalia mtu mwingine mwenye mapenzi ya
dhati mtakayefikia malengo ya kujenga familia,
unaweza kukataliwa na kutengwa na ndugu
kumbe Mungu amekuandalia watu-baki
watakaofanikisha ufikie malengo yako pasipo
masimango ya ndugu, hata rafiki wanaweza
kukusaliti kumbe Mungu amewaondoa makusudi
ili kukuepusha na mabaya waliyoyapanga juu
yako. Sasa usimlaumu Mungu ukadhani
anakuzidishia matatizo, hapo anatafuta njia ya
kuyaondoa hayo matatizo.
Mshukuru Mungu kwa Kila Jambo, kwakuwa
hajawahi kukuwazia mabaya. Anakuwazia mema
sikuzote.
Tafadhari Share kama umeipenda na marafiki
zako wajifunzeโ€ฆโ€ฆ.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Sharon Kibiru Guest Jul 6, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mahiga Guest May 14, 2024
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Mary Kidata Guest Apr 21, 2024
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Monica Adhiambo Guest Jan 15, 2024
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Mary Mrope Guest Jan 7, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ David Sokoine Guest Jan 6, 2024
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Francis Njeru Guest Sep 30, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Lydia Wanyama Guest Mar 26, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Victor Kamau Guest Jan 25, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ James Kawawa Guest Dec 10, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Betty Cheruiyot Guest Sep 26, 2022
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Josephine Nduta Guest Jul 7, 2022
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Andrew Odhiambo Guest Jun 14, 2022
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Grace Mligo Guest Apr 16, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Jackson Makori Guest Dec 6, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Alice Jebet Guest Nov 17, 2021
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Jane Muthui Guest Aug 29, 2021
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Monica Nyalandu Guest Mar 29, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kiwanga Guest Nov 20, 2020
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Patrick Kidata Guest Nov 18, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Nora Lowassa Guest Oct 15, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Lydia Wanyama Guest Sep 3, 2020
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Victor Mwalimu Guest Feb 22, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Anna Malela Guest Feb 4, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Ruth Mtangi Guest Jan 2, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Agnes Lowassa Guest Sep 30, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mushi Guest Jul 11, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Benjamin Masanja Guest Jun 19, 2019
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Ann Wambui Guest Mar 26, 2019
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ George Wanjala Guest Jan 4, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Simon Kiprono Guest Dec 19, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Nov 24, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Rose Lowassa Guest Jul 6, 2018
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mahiga Guest May 30, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Margaret Anyango Guest Mar 5, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Peter Mwambui Guest Oct 1, 2017
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Joyce Nkya Guest May 20, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Wilson Ombati Guest Mar 6, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Rose Kiwanga Guest Feb 9, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Francis Mrope Guest Nov 3, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Alice Wanjiru Guest Oct 30, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Joy Wacera Guest Aug 6, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Grace Mligo Guest Mar 4, 2016
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Irene Akoth Guest Feb 18, 2016
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Esther Cheruiyot Guest Jan 28, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Ruth Wanjiku Guest Nov 4, 2015
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Nancy Akumu Guest Aug 28, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Grace Wairimu Guest Aug 4, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Nicholas Wanjohi Guest Jul 16, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Mary Kidata Guest Apr 9, 2015
Nakuombea ๐Ÿ™

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About