Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

Zaburi ya Toba, Zaburi ya 51

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Hii ndiyo Sala ya Toba
Zaburi 51
1 Ee Mungu, unirehemu,Sawasawa na fadhili zako.Kiasi cha wingi wa rehema zako,Uyafute makosa yangu.
2 Unioshe kabisa na uovu wangu,Unitakase dhambi zangu.
3 Maana nimejua mimi makosa yanguNa dhambi yangu i mbele yangu daima.
4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako,Na kufanya maovu mbele za macho yako.Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo,Na kuwa safi utoapo hukumu.
5 Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu;Mama yangu alinichukua mimba hatiani.
6 Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni;Nawe utanijulisha hekima kwa siri,
7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi,Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji
8 Unifanye kusikia furaha na shangwe,Mifupa uliyoiponda ifurahi.
9 Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu;Uzifute hatia zangu zote.
10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi,Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu
11 Usinitenge na uso wako,Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.
12 Unirudishie furaha ya wokovu wako;Unitegemeze kwa roho ya wepesi.
13 Nitawafundisha wakosaji njia zako,Na wenye dhambi watarejea kwako.
14 Ee MUNGU, Mungu wa wokovu wangu,Uniponye na damu za watu,Na ulimi wangu utaiimba haki yako.
15 Ee Bwana, uifumbue midomo yangu,Na kinywa changu kitazinena sifa zako.
16 Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
17 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika;Moyo uliovunjika na kupondeka,Ee Mungu, hutaudharau.
18 Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako,Uzijenge kuta za Yerusalemu.
19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki,Na sadaka za kuteketezwa, na kafara.Ndipo watakapotoa ngโ€™ombeJuu ya madhabahu yako.
AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest May 26, 2024
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Edwin Ndambuki Guest Sep 27, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrema Guest Jun 27, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mahiga Guest May 26, 2023
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Charles Mrope Guest Apr 10, 2023
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Nicholas Wanjohi Guest Aug 28, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ David Chacha Guest Mar 7, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Henry Mollel Guest Dec 29, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Dec 18, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Anna Mchome Guest Dec 15, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Charles Mrope Guest Oct 13, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Patrick Mutua Guest Jul 28, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Rose Amukowa Guest Apr 24, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ David Kawawa Guest Feb 13, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mahiga Guest Jan 28, 2021
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Margaret Mahiga Guest Jan 9, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Anthony Kariuki Guest Dec 11, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Ann Awino Guest Oct 7, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Charles Mrope Guest Oct 2, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Sarah Mbise Guest Sep 30, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Joy Wacera Guest Sep 29, 2020
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Peter Mwambui Guest Aug 15, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Linda Karimi Guest Jul 31, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Betty Kimaro Guest Jun 1, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Henry Sokoine Guest Apr 30, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Andrew Odhiambo Guest Apr 12, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Francis Mrope Guest Dec 31, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ David Ochieng Guest Dec 16, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Agnes Lowassa Guest Nov 12, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Lydia Wanyama Guest Oct 11, 2019
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Ruth Kibona Guest Aug 19, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ David Nyerere Guest Jan 20, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Moses Kipkemboi Guest Jan 19, 2019
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mchome Guest Oct 20, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Lucy Kimotho Guest Oct 17, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Lucy Wangui Guest Aug 22, 2018
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mushi Guest Aug 21, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Joyce Aoko Guest Jul 24, 2018
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Moses Mwita Guest Jun 7, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Grace Wairimu Guest Mar 11, 2018
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ George Wanjala Guest Dec 28, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Esther Cheruiyot Guest Sep 29, 2017
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Samuel Omondi Guest May 23, 2017
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Simon Kiprono Guest Apr 29, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Stephen Amollo Guest Feb 7, 2017
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Mary Njeri Guest Jan 4, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Daniel Obura Guest Apr 27, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Peter Mbise Guest Mar 22, 2016
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Bernard Oduor Guest Mar 18, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Mary Mrope Guest Oct 25, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About