Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Mchele - 3 vikombe
Nyama ya kusaga - 1 LB
Mchanganyiko wa Nafaka upendazo; maharagwe, njegere, mbaazi n.k 1 mug
Vitunguu maji kata vipande vipande - 3 vya kiasi
Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 2 vijiko vya supu
Mafuta - ½ Kikombe
Mchanganyiko wa bizari (Garam Masala) - 2 vijiko vya chai
Vipande vya supu (Maggi cubes) - 3
Maji (inategemea mchele) - 5
Chumvi - Kiasi
MAPISHI
Osha mchele na roweka. Weka mafuta katika sufuria na kaanga vitunguu mpaka viwe brown. Tia Thomu na tangawizi, kaanga kidogo. Weka nyama ya kusaga, chumvi na garam masala, endelea kukaanga mpaka nyama iwive. Mwaga maji yaliomo katika kopo la nafaka na utie nafaka pekee humo. Tia maji na vipande vya supu (Maggi cubes) huku unavivuruga, koroga kidogo. Tia mchele, koroga kidogo. Funika na pika kwa moto mdogo mpaka karibu na kukauka ukikorogoka kidogo. (kama unavyopika pilau ya kawaida) *Epua uipike katika moto wa oven 350-400 Deg kwa muda wa dakika 15. *Kama sufuria uliyotumia sio ya kupikia katika oven, mimina katika chombo chochote kinachotumika kwa oven kama bakuli la pyrex au treya za foil. Pakua katika sahani na iko tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:06 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga - Vikombe 2
Samli au shortening ya mboga - 2 Vijiko vya supu
Maziwa ¾ Kikombe
Iliki - Kiasi
Mafuta ya kukarangia Kiasi
VIAMBAUPISHI :SHIRA
Sukari - 1 Kikombe
Maji ¾ Kikombe
Vanila ½ Kijiko cha chai
Zafarani (ukipenda) - Kiasi
JINSI YA KUPIKA
Katika kisufuria pasha moto maziwa na wakati huo huo chemsha Samli katika kisufuria kengine. Tia unga katika bakuli na iliki, kisha mimina samli iliyochemka na huku unachanganya. Tia maziwa na uwendele kuchanganya vizuri isiwe na madonge, ikiwa maziwa haitoshi ongeza maji kidogo. Kisha uwache unga ukae mahali pa joto kwa muda wa dakika 10 hivi. Halafu fanya viduara vidogo vidogo, kisha finyiza kwenye greta yenye vishimo vidogo ili upate umbo lake. Kisha karanga kwenye mafuta yaliyopata moto hadi vibadilike rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta. Chemsha shira, ikiwa tayari mimina visheti na upepete na kuzichanganya zipate shira kote. Weka kwenye sahani na zitakuwa tayari kwa kuliwa na kahawa.
Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan
Updated at: 2024-05-25 10:23:16 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Nyama ya mbuzi au ng’ombe ya mafupa - 2 LB
Mchanganyiko wa dengu (hadesi, mchele, chooko, ngano, dengu n.k au nunua ya tayari iliyokwisha changanywa - 2 Vikombe
Kitungu maji (vikate vidogo) - 1
Mafuta - ¼ Kikombe
Nyana kata ndogo ndogo - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawazi iliyosagwa - 1 Kijiko cha supu
Bizari ya haliym - 2 vijiko vya supu
Nyanya ya kopo - 2 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha nyama na chumvi ½ kijiko mpaka iive, toa mafupa. Chemsha mchanganyiko wa dengu mpaka ziive. Katika sufuria weka mafuta, kaanga vitunguu vilainike, tia thomu na tangawizi, bizari ya haliym, nyanya ya kopo. Kaanga mpaka iwive. Tia nyama iliyowiva na supu yake kidogo. Tia mchanganyiko wa dengu tia kwenye mashine ya kusaga (blender), saga na ile supu ya nyama isagike vizuri Mimina kwenye sufuria changanya, tia ndimu kidogo, acha moto mdogo mdogo kwa muda wa dakika 15. Tia katika bakuli, pambia kwa vitunguu vilivyokaangwa vya rangi ya hudhurungi vikavu, pilipili mbichi (ukipenda) na kotmiri, ikiwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:10 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga - 4 Vikombe vya chai Sukari ya laini (icing sugar) - 1 Kikombe cha chai Baking powder - 2 Vijiko vya chai Mayai - 2 Siagi au margarine - 1 Kikombe cha chai Vanilla -1 Kijiko cha chai Maziwa ya kuchanganyia - kiasi Tende iliyotolewa koko - 1 Kikombe ufuta (sasame) kiasi 1/4 kikombe
MAANDALIZI
Changanya unga, siagi, baking powder, na sukari katika mashine. Kisha tia mayai, vanilla na halafu maziwa kidogo kidogo hadi mchanganyiko ushikamane. Gawanya madonge mawili na usukume kama chapati, lakini sio nyembamba sana. Tandaza tende robo ya duara na unyunyize ufuta duara zima: kisha kunja hadi mwisho na ukate kate, kisha upange katika trei ya kuvumbika. Vumbika (bake) moto wa 350°F kwa muda wa dakika 20 au hadi vigeuke rangi na viwive. Zikisha iiva ziache zipowe na zitakuwa tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:48 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Tango 1/2 Kitunguu 1/2 Cherry tomato 8 Lettice kiasi Green olives kidogo Black olives kidogo Hoho jekundu 1 Carrot Giligilani kidogo
Salad dressing Yogurt 1/2 kikombe Swaum 1/2 kijiko cha chai Limao 1/2 Pilipili ya unga 1/4 kijiko cha chai Chumvi kidogo Olive oil kiasi
Matayarisho
Osha vitu vyote kisha vikaushe maji. Baada ya hapo ktk bakuli kubwa katakata, lettice, tango,hoho, kitunguu,giligilani na kisha ikwangue carrot na utie bila kusahau nyanya zote pamoja na olives.Baada ya hapo ichanganye vizuri, kisha tengeneza salad dressing kwa kuchanganya vitu vyote vilivyo (kwenye list ya salad dressing) kisha koroga vizuri.Baada ya hapo ichanganye na salad.Na hapo salad yako itakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuila na chochote upendacho kama vile chips, nyama choma au au chakula kikuu.
Updated at: 2024-05-25 10:37:43 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Salmon fillet 2 Potatao wedge kiasi Lettice kiasi Cherry tomato Limao 1 Swaum Chumvi Olive oil
Matayarisho
Mmarinate samaki na chumvi, swaum na nusu ya limao kisha muweke pembeni, baada ya hapo washa oven kisha tia potato wedge zikisha karibia kuiva anza kumpika samaki, tia mafuta kidogo sana kama kijiko kimoja cha chai hivi katika frypan isiyoshika chini yakisha pata moto kiasi muweke samaki wako (upande wenye ngozi chini kwanza) Mpike mpaka uone rangi ya kahawia kwa chini kisha mgeuze upande wa pili, uku samaki wako akiwa anaendelea kuiva, tayarisha salad yako kwa kusafisha lettice na nyanya kisha zichanganye pamoja kisha tengeneza salad dressing pembeni , kamua limao kisha tia olive oil na chumvi kidogo, Baada ya hapo samaki na potato wedge vitakuwa vimeiva, andaa mlo wako na utakuwa tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:47 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Dagaa (dried anchovies packet 1) Unga wa ugali (corn meal flour 1/4 kilo) (unaweza kutumia unga wa choice uipendayo) Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2) Kitunguu maji (onion 1) Limao (lemon 1/4) Pilipili mbuzi nzima bila kukata (scotch bonnet pepper1, do not chop) Chumvi (salt 1/4 ya kijiko cha chai) Mafuta (vegetable oil) Hoho (green pepper)
Matayarisho
Chambua dagaa kwa kutoa vichwa vyao na utumbo, baada ya hapo waloeke katkika maji ya moto kwa muda wa dakika 5 na uaoshe tena katika maji ya baridi na uwakaushe uwaweke pembeni. Ukishamaliza katakata kitunguu na uandae nyanya tayari kwa upishi. Bandika sufuria ya kupikia dagaa jikoni na utie mafuta, yakishapata moto tia vitunguu pamoja na dagaa. Kaanga mpaka dagaa wawe light brown kisha tia nyanya, chumvi na pilipili. Pika nyanya mpaka ziive (ukitaka kujua kama nyanya zimeiva utaona zinatengana na mafuta) Baada ya hapo kamulia limao kidogo sana na tia pilipili hoho na zipike kama dakika mbili. kisha ipua. Ukisha maliza kupika dagaa andaa chungu cha ugali. Kwanza unatakiwa kuchemsha maji ya moto, kisha koroga pembeni unga kiasi katika maji ya baridi na utie kwenye maji yanayochemka, Fanya kama unatengeneza uji, uji wa ugali ukishachemka tia unga na uanze kuusonga mpaka ugali uive. Ukisha iva pakua na usevu na mboga tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:57 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga 300gm
Siagi 225gm
Icing Sugar 60gm
Chokoleti iliyokoza (Dark Chocolate) - 225gm
Vanilla – Vijiko 2 vya chai
Yai -1
Baking Powder ½ kijiko cha chai
Njugu za vipande ½ kikombe cha chai
Njugu zilizosagwa ¼ kikombe cha chai
JINSI YA KUTAYARISHA
Piga sukari na siagi katika mashine ya keki mpaka iwe laini Kisha mimina yai na vanilla koroga vizuri Mwisho mimina unga na baking powder polepole mpaka ichanganyike. Kata kata umbo (shape) lolote unavyopenda (kama nyota, pembetatu,duara, kopa n.k) Panga kwenye treya na choma kwa moto wa 350°C , vikibadilika rangi kidogo tu vitoe Yayusha chokoleti tia kwenye bakuli ndogo. kisha paka kwa kijiko au chovyea upande mmoja mmoja wa biskuti kisha nyunyizia njugu za kipande na njugu ya unga. Panga kwenye sahani tiyari kunywewa na chai ya maziwa au kahawa.
Updated at: 2024-05-25 10:22:58 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa ngano (plain flour 1/2 of kilo) Siagi (butter vijiko 2 vya chakula) Yai (egg 1) Chumvi (1/2 ya kijiko cha chai) Hiliki (ground cardamon 1/4 ya kijiko cha chai) Maji ya uvuguvugu (warm water) Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Weka unga wa ngano katika bakuli la kukandia, kisha tia chumvi na hiliki na uchanganye kwanza, baada ya hapo tia siagi na uichanganye vizuri na unga mpaka ipotee. Baada ya hapo tia tena yai na uchanganye vizuri. Mchanganyiko ukishachanganyika vizuri sasa unaweza kutia maji ya uvuguvugu kidogo, kidogo huku ukiwa unauchanganya ili kupata donge. Baada ya hapo anza kukanda hilo donge mpaka mabuje yote yapotee na unga uwe mlaini, ambapo itakuchukua kama dakika 15. Baada ya hapo tawanyisha unga katika madonge ya wastani (yasiwe makubwa sana au madogo sana) Ukimaliza hapo, andaa kibao cha kusukumia chapati kwa kukitia unga kidogo ili chapati isinatie kwenye kibao. Sukuma donge moja la chapati mpaka liwe flat na kisha weka kijiko kimoja cha mafuta na usambaze. ukisha maliza ikunje (roll). Fanya hivyo kwa madonge yote yaliyobakia. Baada ya hapo andaa chuma cha kuchomea (fry-pan) katika moto wa wastani. Kisha anza kusukuma chapati (ni vizuri ukaanza na zile ulizozikunja mwanzo ili kuzipa nafasi zile za mwisho ziweze kulainika) ukiwa unasukuma hakikisha zinakuwa flat (na zisiwe nene sana au nyembamba sana) Ukishamaliza hapo tia kwenye chuma cha kuchomea. Acha iive upande mmoja then igeuze upande wa pili. Tia mafuta ama kijiko kimoja kikubwa upande wa chini wa chapati na uanze kuukandamiza kwa juu uku ukiwa unaizungusha. fanya hivyo uku ukiwa unaigeuza kuiangalia kwa chini ili isiungue. ikishakuwa ya brown, geuza upande wa pili na urudie hivyohiyvo mpaka chapati iive. Rudia hii process kwa chapati zote zilizobakia.
Siri ya chapati kuwa laini ni kutia siagi au mafuta ya kutosha kipindi unazikanda na pia kuzikanda mpaka unga uwe laini.
Updated at: 2024-05-25 10:34:53 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga 2 Vikombe
Samli au shortening ya mboga 2 Vijiko vya supu
Maziwa ¾ Kikombe
Iliki Kiasi
Mafuta ya kukarangia Kiasi
Shira
Sukari 1 Kikombe
Maji ¾ Kikombe
Vanila ½ Kijiko cha chai
Zafarani (ukipenda) Kiasi
Jinsi ya kupika na kuandaa
Katika kisufuria pasha moto maziwa na wakati huo huo chemsha Samli katika kisufuria kengine. Tia unga katika bakuli na iliki, kisha mimina samli iliyochemka na huku unachanganya, kisha tia maziwa na uwendele kuchanganya vizuri isiwe na madonge, ikiwa maziwa haitoshi ongeza maji kidogo. Kisha uwache unga ukae mahali pa joto kwa muda wa dakika 10 hivi. Halafu fanya viduara vidogo vidogo, kisha finyiza kwenye greta yenye vishimo vidogo ili upate umbo kama kwenye picha. Kisha karanga kwenye mafuta yaliyopata moto hadi vibadilike rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta. Chemsha shira, ikiwa tayari mimina visheti na upepete na kuzichanganya zipate shira kote. Weka kwenye sahani na zitakuwa tayari kwa kuliwa na kahawa.