Updated at: 2024-05-25 10:23:13 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji ya wali
Mchele - 3 vikombe
Vitunguu (viliokatwa vidogo vidogo) - 2
Mafuta - 3 vijiko vya supu
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai
Bizari ya pilau - 1 kijiko cha supu
Mdalasini - 1 kijiti
Hiliki - 3 chembe
Pilipili manga nzima - chembe chache
Siagi - Vijiko 2 vya supu
Chumvi - kiasi
Mahitaji kwa kuku
Kuku kidari (Breast) kata vipande vipande - 2 LB
Mafuta - 3 vijiko vya supu
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu
Kotmiri iliyokatwa ndogo ndogo - kiasi
Bizari ya pilau (cummin au jiyrah) - 1 kijiko cha chai
Pilipili kubwa tamu la kijani - 1
Pilipili kubwa tamu nyekundu - 1
(zikate vipande vipande)
Karoti iliyokunwa - 1 β 2
Chumvi - Kiasi
Mapishi ya Wali:
Roweka mchele kwa muda fulani kutegemea mchele
Katika sufuria tia mafuta na kaanga vitunguu hadi vibadilike rangi kidogo.
Tia thomu iliyosagwa, mdalasini, bizari ya pilau, hiliki, pilipili manga na chumvi, kaanga kidogo.
Tia mchele kaanga kidogo, kisha tia maji ya moto kiasi kutegemea na aina ya mchele kama kawaida ya kupika wali kama pilau.
Tia sigai, funika upikike wali hadi uwive.
Mapishi ya Kuku:
Mchanganye kuku pamoja na thomu/tangawizi iliyosagwa, chumvi, pilipili mbichi.
Katika karai tia mafuta yapate moto vizuri.
Mtie kuku, bizari ya pilau (jiyrah) na ukaange, karibu na kuiva tia vitunguu.
Tia mapilipili makubwa, kotmiri, na kaanga kwa dakika moja tu uzime moto na epua weka kando.