Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:37:49 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mackerel 2 Kitunguu swaum na tangawizi (ginger and garlic paste) 1 kijiko cha cha kula Pilipili iliyo katwakatwa (chopped scotch bonnet ) 1/2 Limao (lemon) 1/2 Chumvi (salt) kiasi Curry powder 1/2 kijiko cha chai Coriander powder 1/2 kijiko cha chai Mafuta 1 kijiko cha chai
Matayarisho
Safisha samaki kisha wakaushe maji ( ukipenda unaweza kuwakata kati au ukawapika wazima) Baada ya hapo wakate mistari kila upande ( ili spaces ziweze kuingia ndani) kisha waweke kwenye bakuli na utie spice zote. Wachanganye vizuri kisha waweke frijini na uwaache wamarinate kwa muda wa masaa 3. Baada ya hapo washa oven kisha wapakaze mafuta na uwafunge kwenye foil na uwatie kwenye oven kwa muda wa dakika 20. Baada ya hapo fungua foil na uwaache kwenye oven kwa muda wa dakika 10 ili wapate kukauka kidogo. Na hapo watakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuwala kwa kitu chochote upendacho.
Updated at: 2024-05-25 10:23:12 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Mchele wa pishori (basmati) - 4
Nyama ya kuku bila mafupa - 1 Lb
Kamba saizi kubwa - 1Lb
Mchanganyiko wa mboga - njegere, karoti,
mahindi, maharage ya kijani (spring beans) - 2 vikombe
Figili mwitu (Cellery) - 2 mche
Vitunguu vya majani (spring onions) - 4-5 miche
Kebeji - 2 vikombe
Pilipili ya unga nyekundu - 1 kijiko cha chai
Pilipili manga ya unga - 1 kijiko cha chai
Sosi ya soya - 3 vijiko vya supu
Mafuta - 1/4 kikombe
Chumvi - kiasi
MAPISHI
Osha na roweka mchele. Tia kamba chumvi na pilipili nyekundu ya unga. Tia mafuta vijiko viwili katika kikaango (frying pan), kaanga kamba kidogo tu, weka kando. Katakata kuku vipande vidogo vidogo, tia chumvi na pilipili manga. Kaanga kaTika kikaango (ongeza mafuta kidogo) Weka kando. Katika karai, tia mafuta kidogo kama vijiko vitatu vya supu, tia kamba na kuku, tia mboga za mchanganyiko, sosi ya soya na chumvi, kaanga kidogo. (Kama mboga sio za barafu) itabidi uchemshe kidogo. Katakata kebeji, figili mwitu (cellery) na vitunguu vya majani (spring onions) utie katika mchaganyiko. acha kwa muda wa chini ya dakika moja katika moto. Chemsha mchele, tia mafuta kidogo au siagi, chumvi upikie uive nusu kiini, mwaga maji uchuje. Changanya vyote na wali rudisha katika sufuria au bakuli la oveni, funika na upike kwa moto wa kiasi kwa muda wa dakika 15-20 takriban. Epua na upakue katika sahani ukiwa tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:09 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Philo (thin pastry) manda nyembamba - 1 paketi
Siagi - ¼ Kikombe cha chai
Baking powder - 2 Vijiko vya chai
Pistachio/ lozi - 2 vikombe vya chai
Mafuta - ½ Kikombe
VIAMBAUPISHI VYA SHIRA
Sukari - 2 Vikombe vya chai
Maji - 2 ½ Vikombe vya chai
ndimu - ½ kijiko cha chai
JINSI YA KUANDAA
Tafuta treya iliyokuwa sawa na ukubwa wa hizo manda nyembamba (philo) au zikate hizo manda kwa ukubwa wa treya (mraba au mstatili) Kisha yeyusha siagi changanya na mafuta. Kisha panga manda moja pakaza mafuta juu yake kisha weka manda nyingine juu yake kisha pakaza mafuta tena weka manda nyingine juu yake, endelea kufanya hivyo mpaka ziwe kama sita au saba kisha nyunyizia pistachio na lozi halafu panga tena manda na mafuta manda na mafuta tena sita au saba kisha nyunyizia tena pistachio na lozi. Panga namna hivyo mpaka treya ijae inapofika manda ya mwisho kata vipande vya mraba vidogodogo humo humo kwenye treya kisha nyunyizia mafuta yaliyobaki. Washa moto wa oven 350°F kwa muda wa dakika 20 au hadi rangi ibadilike kidogo (isikauke sana) Chemsha syrup yako kama shira ya majimaji lakini isiwe nzito sana ikishakuwa tayari mwisho tia ndimu acha ipoe kidogo kisha miminia juu ya treya yote halafu malizia kunyunyizia pistachio na lozi zilizobaki. Zikishakuwa tayari zipange kwenye sahani tayari kwa kuliwa.
ANGALIZO
Ukishatoa treya kwenye oven wacha ipoe kidogo na syrup yako pia wacha ipoe kidogo kabla hujamimina, ukitia ya motomoto zitalainika. Manda nyembamba za baklawa zinauzwa tiyari madukani kwenye pakiti.