Log in to access your menu with tools for managing ๐ tasks, ๐ฅ clients, ๐ฐ finances, ๐ learning, ๐ personal growth, and ๐ spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Ujumbe mzuri wa kumwambia mpenzi wako kuwa yeye tuu mdiye kakutawala
Updated at: 2024-05-25 15:36:48 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Fikra hutawala mtima wangu, Kwa madhila yalojaa duniani, Kwa muhali wa yanayojiri, Kwa machweo na mawio, Kwa totoro ama nuruni, Nao moyo hukosa ukamilifu, Kwa utashi wa zake hisia, Zinipazo sababu kuu, Ya upendo juu yako, Ya kukufanya daima uwe, Mawazoni mwangu.
Mawazoni ama ndotoni, Daima wewe hutawala, Kila asubuhi niamkapo, Nao usiku nilalapo, U chakula changu akilini, Nalo tulizo langu moyoni, Daima huuwaza upekee, Wewe uliojaaliwa, Na hivyo naihisi furaha, Daima wewe uwapo, Mawazoni mwangu.
Updated at: 2024-05-25 15:22:47 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Wewe ni taa kwangu imulikayo gizani, nakupenda sana mpenzi wangu wa moyo, utakuwa wangu siku dear! Kosa nililofanya ni kwa bahati mbaya, naomba unisamehe na ninaahidi kutorudia tena katika penzi letu!
Ujumbe mzuri wa SMS wa kumfariji mpenzi wako maisha yake yanapokuwa magumu
Updated at: 2024-05-25 15:36:58 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Furaha yangu kubwa ni kuliona tabasamu lako, kujua uko na furaha, na kuhisi upendo wako. Najua kuwa maisha mara nyingine huwa ni makatili, na hiyo ni sababu niko hapa kukuonyesha kuwa maisha yanaweza kuwa mazuri kama kuna mtu anayekujali.
Dah! Safari yetu ilikuwa ngumu kweli ila hatimaye tumefika japo ni usiku sana hebu tupige hodi tusije kabwa na vibaka hapa nje. Hodiiiiii, Hodiiiii,
Updated at: 2024-05-25 15:37:09 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Dah! Safari yetu ilikuwa ngumu kweli ila hatimaye tumefika japo ni usiku sana hebu tupige hodi tusije kabwa na vibaka hapa nje.
Hodiiiiii, Hodiiiii,
Tunaomba tufungulie Mlango,, sisi tunaitwa FURAHA, AMANI na UPENDO. Tumebeba HEKIMA, BUSARA na MAFANIKIO. Tulikuwa wengi HURUMA na UPOLE wanakuja nyuma. CHUKI na WIVU hawana nauli. TABU ni mahututi. SHIDA yuko jela. MATATIZO amepigwa shoti ya umeme. MIKOSI amefariki njiani. LAANA ameliwa na mamba. UVIVU ameungua na maji ya moto hajiwezi. Tutakuwa nawe daima maana tumefika kwa NEEMA . Mungu akulinde na mabaya yote katika dunia hii. ucku mwema.