Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Maria Bikira Milele, na mkubwa wa Familia Takatifu. Umechaguliwa na Mwakilishi wa Kristu kama Msimamizi wa kimbingu na mlinzi wa Kanisa alilolianzisha Kristu. Ndiyo maana ninakuomba kwa matumaini makuu usaidizi wako wenye nguvu kwa ajili ya Kanisa zima duniani.
Mlinde kwa namna ya pekee, kwa upendo wa kikweli wa ki-baba, Baba Mtakatifu na Maaskofu wote na Mapadre wenye ushirika na Kiti cha Petro. Uwe mlinzi wao wote wanaotumikia wokovu wa wanadamu kati ya majaribu na mahangaiko ya maisha haya, na utujalie kwamba watu wote wa dunia hii wamfuate Kristu na Kanisa alilolianzisha.
Mpendwa Mtakatifu Yosefu, ukubali majitoleo ya nafsi yangu ambayo sasa ninafanya. Ninajiweka wakfu kwako kwa ajili ya utumishi wako, ili daima wewe uwe baba yangu, mlinzi wangu, na kiongozi wangu katika njia ya wokovu. Unijalie usafi mkuu wa moyo na matamanio makuu ya maisha ya kiroho. Unijalie ili matendo yangu yote, kwa mfano wako, yawe kwa ajili ya sifa na utukufu wa Mungu, pamoja na Moyo wa kimungu wa Yesu, moyo safi wa Maria, na moyo wako wa ki-baba. Uniombee, nami nishiriki kifo chako cha furaha na kitakatifu.
Amina.
Dorothy Nkya (Guest) on August 17, 2017
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mwanaidi (Guest) on July 17, 2017
🙏🙏🙏
Michael Mboya (Guest) on May 23, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Daniel Obura (Guest) on March 6, 2017
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
Grace Mligo (Guest) on February 5, 2017
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Peter Tibaijuka (Guest) on December 5, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Moses Kipkemboi (Guest) on November 17, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
David Chacha (Guest) on October 5, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mary Njeri (Guest) on July 16, 2016
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
Mercy Atieno (Guest) on June 2, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Joseph Mallya (Guest) on April 26, 2016
🙏🌟 Mungu akujalie amani
John Lissu (Guest) on April 25, 2016
🙏💖 Nakushukuru Mungu
Robert Okello (Guest) on April 17, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Mariam Kawawa (Guest) on April 13, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mercy Atieno (Guest) on March 25, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
Anna Kibwana (Guest) on March 19, 2016
Rehema hushinda hukumu
Benjamin Masanja (Guest) on March 11, 2016
Mungu akubariki!
Grace Majaliwa (Guest) on November 1, 2015
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
Charles Mrope (Guest) on July 3, 2015
Mwamini Bwana; anajua njia
Grace Mligo (Guest) on May 31, 2015
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
Nancy Kabura (Guest) on May 19, 2015
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mary Mrope (Guest) on May 16, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mary Mrope (Guest) on April 23, 2015
Amina