Vipimo vya Wali:
Mchele - 3 vikombe
*Maji ya kupikia - 5 vikombe
*Kidonge cha supu - 1
Samli - 2 vijiko vya supu
Chumvi kiasi
Hiliki - 3 chembe
Bay leaf - 1
Vipimo Vya Kuku
Kidari (chicken breast) - 1Kilo
Kitunguu - 1
Tangawizi mbichi - Β½ kipande
Kitunguu saumu(thomu/galic) - 7 chembe
Pilipili mbichi - 3
Ndimu - 2
Pilipilimanga - 1 kijiko cha chai
Mdalasini - Β½ kijiko cha chai
Jira/Cummin ya unga - 1 kijiko cha chai
Maji - ΒΌ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Wali:
Osha na roweka mchele kisha weka sufuria katika moto tia samli ipashe moto.
Tia hiliki, bay leaf, kaanga, kisha tia mchele ukaange kidogo.
Tia maji, chumvi na kidonge cha supu, upike wali kama unavyopika pilau.
*Maji kisia kwa kutegemea mchele ulivyo.
*Unaweza kutumia supu yoyote badala ya kidonge.
Kuku:
Katakata kidari cha kuku vipande vya kiasi, weka katika sufuria, tia ndimu, bizari zote, chumvi.
Katakata kitunguu vipande vidogodogo, pilipili, na kitunguu thomu (chopped), tia katika kuku.
Chuna tangawizi mbichi tia katika kuku. Changanya vitu vyote vizuri.
Tia maji kiasi ΒΌ kikombe tu kiasi cha kumkaushia kuku. Weka katika moto mpike huku unageuzageuza. Anapokaribia kukauka epua akiwa tayari kuliwa na wali (na saladi upendayo)
No comments yet. Be the first to share your thoughts!