Vipimo
Mchele wa pishori (basmati) - 4
Vitunguu katakata - 3
Nyanya (tungule) katakata vipande vikubwa - 3 -5
Pilipili boga la kijani (capsicum) katakata
Supu ya kitoweo au vidonge vya supu - 1
Bizari mchanganyiko Garama masala - 5-7
Pilipili mbichi ya kusaga - Kiasi
Zaafarani ya maji (flavor) - 1 kijiko cha chakula
Mafuta ya kupikia - ΒΌ kikombe
Samaki wa kukaanga
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Roweka mchele kiasi nusu saa kisha chemsha mchele kwa supu uive nusu kiini. Mwaga maji chuja.
Wakati mchele unapikika, weka mafuta katika sufuria kubwa ya kupikia wali, kaanga vitunguu mpaka vigeuke rangi ya hudhurungi.
Tia nyanya na vitu vinginevyo vyote kaanga kidogo tu.
Mwaga wali katika sufuria na nyunyizia zaafarani kisha changanya na masala vizuri.
Funika upike katika oven (bake) au juu ya stovu moto mdogo mdogo kiasi dakika 15- 20.
Epua ikiwa tayari, pakua kwenye sahani kisha tolea kwa samaki wa kukaanga.
No comments yet. Be the first to share your thoughts!