Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/katoliki/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Madhara ya kuwa mnene kupindukia

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Unene(obesity), ni ugonjwa unaokua kwa kasi kipindi hiki ukiambatana na madhara makubwa kiafya hata vifo. Unene hupimwa kwa kutumia kipimo kinachotambulika kitaalamu kama BMI (yaani uzito kwa Kilogram kugawa kwa urefu kwa mita mara mbili). Tatizo la unene uliopindukia huweza kusababisha mhusika kutengwa katika jamii, kubaguliwa, kudhihakiwa hata kunyanyapaliwa hivyo kuleta madhara kisaikologia kwa mgonjwa. Sababu za unene uliopindukia ni pamoja na kurithi. Mtoto aliyezaliwa na wazazi wanene, ana asilimia 80 ya kuwa mnene, aliyezaliwa na wazazi wembamba, ana asilimia 10 ya kuwa mnene. Utamaduni na ukosefu wa nidhamu katika vyakula, pia unachangia unene uliopindukia. Mfano; kuna ongezeko kubwa la watoto na vijana wanene kwa sasa mijini kuliko vijijini. Madhara yaletwayo na unene uliopindukia ni mengi, lakini kwa uchache ni pamoja na kulika kwa jointi hasa za miguu, maumivu kiunoni na katika nyonga, shinikizo la damu, kisukari, pia kukosa usingizi kutokana na kubanwa kwa hewa. Mengine ni athma, kiungulia, mafuta mengi mwilini, magonjwa ya moyo na moyo kushidwa kufanya kazi na mawe katika kibofu cha nyongo. Wagonjwa hujikuta wakishindwa kufanyakazi vyema ili kujipatia kipato, hivyo kuwa tegemezi, kunyanyapaliwa pia huleta matatizo ya kisaikologia kama nilivyoeleza awali. Matibabu ya ugonjwa huu ni pamoja na kubadili mfumo na aina ya maisha. Hii ni pamoja na kuwa na nidhamu katika chakula na kufanya mazoezi. Ni wazi kwamba wazazi na watoto wanaoishi mjini, wanakabiliwa na tatizo hili, kutokana na maisha ya mfumo mgando ( kula kazi bila jasho-kulala, au kula-kusoma-kulala). Matibabu ya muda mrefu ya tatizo hili na ambayo husaidia mgonjwa kwa kiwango kikubwa ni kufanyiwa upasuaji. Upasuaji katika tumbo ndiyo tiba mwafaka kwa unene uliopindukia.
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Sababu za magonjwa ya figo na jinsi ya kuondokana na janga la magonjwa ya Figo

Sababu za magonjwa ya figo na jinsi ya kuondokana na janga la magonjwa ya Figo

1.Usichelewe kwenda HAJA.ย Kutunza mkojo kweye kibofu chako kwa muda mrefu ni wazo ... Read More
Matumizi ya tunda la shelisheli kama dawa ya ngozi

Matumizi ya tunda la shelisheli kama dawa ya ngozi

Shelisheli lililokomaa huwa na uzito wa hadi kilo 6, ambapo mshelisheli unaweza kukua kwa urefu w... Read More

Namna ya kuongeza nguvu za kiume bila kutumia dawa

Namna ya kuongeza nguvu za kiume bila kutumia dawa

Upungufu wa nguvu za kiume umekua tatizo kubwa sana kwa wanaume wengi. Tatizo hili limewakumba wanau... Read More
PROSTATE GLAND (TEZI DUME) TATIZO SUGU KWA WANAUME

PROSTATE GLAND (TEZI DUME) TATIZO SUGU KWA WANAUME

-Hii ni tezi ya wanaume yenye sifa zifuatazo.
~Ina umbo km yai(oval shape)
~Ina ukubwa ... Read More

Faida za kula Karoti kiafya

Faida za kula Karoti kiafya

Asilimia kubwa tunapenda kutumia karoti katika kuunga katika mboga ya nyama na si kuila karoti ka... Read More

Jinsi ya kutibu chunusi kwa Siki ya tufaa

Jinsi ya kutibu chunusi kwa Siki ya tufaa

Siki ya tufaa (Apple cider vinegar) ni moja kati ya dawa zinazojulikana katika kutibu chunusi ahs... Read More

Sababu, dalili na jinsi ya kujikinga na tatizo la kiungulia kwa wanawake wajawazito

Sababu, dalili na jinsi ya kujikinga na tatizo la kiungulia kwa wanawake wajawazito

Hii ni hali inayowakumba mama wajawazito walio wengi. Inaweza kutokea kipindi chochote cha ujauzi... Read More

Vyakula 7 vya kuepuka kula ili uwe na afya nzuri

Vyakula 7 vya kuepuka kula ili uwe na afya nzuri

Inasemwa kuwa โ€œwewe ni kile unachokulaโ€ kwa kumaanisha kuwa mwonekano wetu na afya ya mwili n... Read More

Faida 10 za kulala mapema kiafya

Faida 10 za kulala mapema kiafya

Mapera ni matunda yanayo patikana kwa wingi lakini mara nyingi huwa hayapendelewi sana kutokana n... Read More

UJUE NA UFAHAMU MFUMO WA MOYO (CARDIOVASCULAR SYSTEM)

UJUE NA UFAHAMU MFUMO WA MOYO (CARDIOVASCULAR SYSTEM)

Mfumo huu wa moyo una kazi zifuatazo:-

๐Ÿ‘‰kupampu damu Mwilini pia kusafirisha gas, taka n... Read More

MADHARA YA SHISHA

MADHARA YA SHISHA

Yafuatayo ni madhara ya shisha; 1.Kansa Licha ya kupita ndani ya maji, moshi wa shisha huwa na kiwa... Read More
Matumizi ya mbaazi kama dawa

Matumizi ya mbaazi kama dawa

Mbaazi ni zao la chakula ambalo linalimwa sehemu nyingi sana hapa nchini, zao hili pia linaweza k... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles | โœ๐Ÿป Re-Write Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About