Sidebar with Floating Button
AckySHINE Katoliki
☰
AckyShine

Maswali na Majibu kuhusu Ibada ya Misa

Featured Image

Ishara ndogo ya Msalaba juu ya panda la uso, mdomo, na kifua kabla ya Injili ina maana gani?


Maana yake ni kama Ahadi kuwa, Niko tayari kulifahamu Neno la Mungu kwa akili yangu, Nitalitangaza kishujaa kwa Midomo yangu, Nitalipenda na kulishika kwa Moyo wangu wote.







Je ni dhambi kukosa Misa Jumapili?


NDIYO. Ni dhambi kubwa kukosa Misa kwa Makusudi siku ya Jumapili/Dominika na Sikukuu zilizoamriwa.







Sakramenti ya Ekaristi ni nini?


Sakramenti ya Ekaristi ni Sakramenti ya Mwili na Damu ya Yesu Kristo, aliye kweli katika Maumbo ya Mkate na Divai. (Yoh 6:1-17, Mt 26:26-28)







Ni wakati gani katika Misa Mkate na Divai vinageuka Mwili na Damu yake Kristo?


Ni katikati ya Misa padri asemapo maneno Matakatifu aliyosema Yesu mwenyewe: "HUU NDIO MWILI WANGU; HII NDIO DAMU YANGU"

26 Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akamshukuru Mungu, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, β€œTwaeni mle; huu ni mwili wangu.” 27 Kisha akatwaa kikombe cha divai, akashukuru, akawapa akisema, β€œKunyweni nyote; 28 maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi. 29 Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”
30 Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni. (Mat 26:26-30)







Je Sakramenti ya Ekaristi hujulikana kwa majina yapi?


Majina haya;

1. Ekaristi Takatifu
2. Karamu ya Bwana
3. Misa Takatifu
4. Sakramenti Takatifu ya Altare
5. Komunyo Takatifu
6. Sadaka Takatifu
7. Kumega Mkate







Baada ya Mitume kufa ni nani wanafanya Sakramenti ya Ekaristi


Badaa ya Mitume kufa Maaskofu na Mapadri wanaendelea kuadhimisha Sakramenti ya Ekaristi Takatifu







Ni lini Yesu Kristo aliwapa Maaskofu na Mapadri Uwezo wa kugeuza mkate na divai kuwa Mwili na Damu yake?


Yesu Kristo aliwapa Maaskofu na Mapadri Uwezo wa kugeuza mkate na divai kuwa Mwili na Damu yake alipowafanya Mitume kuwa Mapadri katika karamu ya mwisho aliposema "FANYENI HIVI KWA UKUMBUSHO WANGU" (Lk 22:14-20)







Misa ni nini?


Misa ni sadaka safi ya Wakristo kwa Mungu, ndiyo sadaka ya Agano Jipya ambayo
Kristo kwa njia ya Padri anamtolea Mungu Baba mwili na damu yake katika umbo la mkate na divai kama alivyojitolea mwenyewe juu ya msalaba.







Sadaka ya Msalaba ni nini?


Sadaka ya Msalaba ni tendo la mateso na kifo cha Bwana wetu Yesu Kristojuu ya Msalaba pale Kalvari







Ni kwa nini Sadaka ya Misa Takatifu ni Sadaka ile ile ya Msalaba?


Sadaka ya Misa Takatifu ni ile ile ya Msalaba kwa sababu ni sadaka moja tu, kuhani na kafara ni yule yule.

Tofauti ni namna tu yankuitoa hiyo sadaka. (1Kor 11:26, Ebr 9:14,25-28)
Pale msalabani damu ilimwagika lakini katika Ekaristi damu haimwagiki tena







Misa Takatifu hutolewa kwa nani?


Misa Takatifu hutolewa kwa Mungu Baba Mwenyezi (Ebr 5:1-10, Law 9:7).







Yesu aliweka sadaka ya Misa Takatifu kwa makusudi gani?


Yesu aliweka sadaka ya Misa Takatifu ili;

1. Amtolee Baba sadaka bora siku zote
2. Atujalie mastahili yake Msalabani
3. Azilishe roho kwa neema za sadaka hiyo. (Ebr 5:1-10, 7:27).







Sadaka ya Misa Takatifu yatolewa kwa nia gani?


Sadaka ya Misa Takatifu yatolewa kwa nia ya kumwabudu Mungu, kumshukuru, kujipatanisha nae na kumwomba. (Ebr 9:14)







Misa Takatifu hutolewa kwa ajili ya nani?


Misa Takatifu hutolewa kwa ajili ya kanisa nzima yaani kwa ajili ya watu wote wazima na wafu. (Ebr 9:14. Rum 1:9)







Kutolea Misa kwa Marehemu maana yake ni nini?


Kutolea Misa kwa Marehemu ni kutolea Misa kwa ajili ya roho zilizoko toharani ili ziweze kuingia mbinguni







Misa Takatifu ina sehemu kuu ngapi?


Misa Takatifu ina sehemu kuu mbili

1. Litrujia ya Neno
2. Liturujia ya Ekaristi







Litrujia ya Ekaristi ina sehemu kuu ngapi?


Litrujia ya Ekaristi ina sehemu kuu tatu

1. Matayarisho ya vipaji
2. Sala ya Ekaristi
3. Ibada ya Komunyo







Ni vitu gani vya msingi na vya lazima katika kuadhimisha Ekaristi Takatifu?


Vitu vya lazima katika kuadhimisha Ekaristi Takatifu ni

1. Mkate wa Ngano
2. Divai ya mzabibu







Kabla ya Kupokea Ekaristi Takatifu Tunasali sala gani?


Tunasali "Ee Bwana sistahili uingie kwangu lakini sema neno tu na roho yangu itapona"







Katika Ekaristi Takatifu Tunampokea nani?


Katika Ekaristi Takatifu Tunampokea Yesu Kristo Katika Maumbo ya Mkate na Divai na tunaungana naye (Yoh 6:57)







Mkristo awe katika hali gani kabla ya kupokea Ekaristi Takatifu?


1. Awe na Neema ya Utakaso yaani asiwe na dhambi ya mauti.
2. Awe na Imani, Ibada na Kumtamani Yesu.

3. Afunge chakula Muda wa saa Moja na Kileo zaidi ya masaa matatu.
4. Awe safi kimwili.
5. Awe na adabu na heshima.







Komunyo Takatifu Hutuletea neema gani?


1. Hulinda na kuongeza neema ya Utakaso iliyo uzima wa roho zetu.
2. Hutuondolea dhambi ndogo na kupunguza hatari ya kutenda dhambio kubwa.

3. Hututia bidii na nguvu ya kutenda mema kwa kutuongezea Imani, Matumaini na Mapendo.
4. Huleta Umoja katika Kanisa, sio sisi na Kristo tuu bali sisi kwa sisi.







Mkristo akipokea Ekaristi Takatifu akiwa na dhambi rohoni anatenda dhambi gani?


Mkristo akipokea Ekaristi Takatifu akiwa na dhambi anatenda dhambi kubwa yaani kufuru Sakramenti.

26 Maana kila mnapokula mkate huu na kukinywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja. 27 Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana. (1 Kor 11;26 - 27)

28Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho; 29 maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe. 30 Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa. 31 Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo. 32Lakini tunapohukumiwa na Bwana, tunafunzwa tuwe na nidhamu, ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu. (1 Kor 11;28 - 32)







Je, Kanisa linahimiza waamini wapokee Ekaristi wakati gani?


Kanisa linahimiza waamini wapokee Komunyo Takatifu kila siku wanaposhiriki Misa







Nani Mhudumu wa adhimisho la Ekaristi Takatifu?


Mhudumu wa adhimisho la Ekaristi Takatifu ni Askofu na Padre







Je, Mkristo akipokea kipande cha Hostia amempokea Yesu Mzima?


Ndiyo, Amempokea Yesu Mzima kabisa, Hata akipewa zaidi ya hostia moja amempokea Yesu Mzima







Sakramenti ya Ekaristi Takatifu Huifadhiwa wapi?


Sakramenti ya Ekaristi Takatifu Huifadhiwa kwenye Tabernakulo







Tabernakulo ni nini?


Tabernakulo ni mahali Patakatifu anapokaa Yesu wa Ekaristi siku zote







Sakramenti ya Ekaristi Takatifu hukaa Tabernakulo kwa sababu gani


Sakramenti ya Ekaristi Takatifu hukaa Tabernakulo kwa ajili ya watu wote hasa wagonjwa







Ishara wazi ya Sakramenti ya Ekaristi Takatifu ni nini?


Ishara wazi ya Sakramenti ya Ekaristi Takatifu ni maumbo ya mkate na divai, na maneneo ya mageuzo ya Yesu mwenyewe Padri akiyatamka.







Baada ya kumpokea Yesu wa Ekaristi tufanye nini?


Baada ya kumpokea Yesu wa Ekaristi: Tumwabudu,tumshukuru, tumwombe kwani yeye ni Mwenyezi. (Mt 2:11, Lk 17:11)

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Frank Macha (Guest) on June 8, 2024

Nakuombea πŸ™

Samuel Were (Guest) on March 16, 2024

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Robert Ndunguru (Guest) on December 14, 2023

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

David Ochieng (Guest) on July 20, 2023

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Janet Mbithe (Guest) on May 17, 2023

Neema na amani iwe nawe.

Lydia Mutheu (Guest) on May 10, 2023

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Lydia Mahiga (Guest) on December 13, 2022

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Vincent Mwangangi (Guest) on October 31, 2022

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Richard Mulwa (Guest) on September 26, 2022

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Alice Wanjiru (Guest) on September 2, 2022

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Richard Mulwa (Guest) on August 18, 2022

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Agnes Lowassa (Guest) on August 9, 2022

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Grace Mushi (Guest) on June 30, 2022

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Vincent Mwangangi (Guest) on April 16, 2022

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

John Kamande (Guest) on November 14, 2021

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

John Lissu (Guest) on June 13, 2021

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Esther Cheruiyot (Guest) on May 24, 2021

Mwamini Bwana; anajua njia

Linda Karimi (Guest) on May 14, 2021

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Peter Mwambui (Guest) on April 14, 2021

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

John Lissu (Guest) on April 1, 2021

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Tabitha Okumu (Guest) on September 15, 2020

Mwamini katika mpango wake.

Janet Wambura (Guest) on July 20, 2020

Neema ya Mungu inatosha kwako

Vincent Mwangangi (Guest) on May 18, 2020

Baraka kwako na familia yako.

Monica Nyalandu (Guest) on April 17, 2020

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Grace Mligo (Guest) on April 5, 2020

Dumu katika Bwana.

Betty Akinyi (Guest) on March 16, 2020

Nguvu hutoka kwa Bwana

Jane Muthoni (Guest) on February 8, 2020

Mungu akubariki!

Grace Mushi (Guest) on October 16, 2019

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Martin Otieno (Guest) on July 19, 2019

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Peter Mwambui (Guest) on July 14, 2019

Mungu ni mwema, wakati wote!

Alice Wanjiru (Guest) on February 26, 2019

Katika imani, yote yanawezekana

Anna Kibwana (Guest) on January 28, 2019

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

David Kawawa (Guest) on December 30, 2018

Sifa kwa Bwana!

John Mwangi (Guest) on November 30, 2018

Endelea kuwa na imani!

Janet Mwikali (Guest) on June 9, 2018

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Sarah Achieng (Guest) on June 7, 2018

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Jackson Makori (Guest) on March 3, 2018

Rehema hushinda hukumu

Lydia Mahiga (Guest) on February 9, 2018

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Joseph Njoroge (Guest) on November 9, 2017

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Faith Kariuki (Guest) on April 29, 2017

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

David Kawawa (Guest) on March 14, 2017

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Lucy Mushi (Guest) on December 19, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Peter Otieno (Guest) on November 21, 2016

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Lucy Wangui (Guest) on July 12, 2016

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

David Kawawa (Guest) on June 1, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

Samuel Were (Guest) on May 27, 2016

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Agnes Njeri (Guest) on April 13, 2016

Rehema zake hudumu milele

Patrick Kidata (Guest) on August 25, 2015

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

David Nyerere (Guest) on July 29, 2015

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

George Mallya (Guest) on July 3, 2015

Imani inaweza kusogeza milima

Related Posts

Maswali na Majibu kuhusu Malaika

Maswali na Majibu kuhusu Malaika

Read More

Mafundisho kuhusu Neema

Mafundisho kuhusu Neema

Read More
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Maandiko Matakatifu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Maandiko Matakatifu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Maandiko Matakatifu?

Kanisa Katoliki linaamini kwa... Read More

Mambo ya Muhimu kufahamu kuhusu Mungu

Mambo ya Muhimu kufahamu kuhusu Mungu

Read More

Mambo ya Msingi unayotakiwa kufahamu kuhusu Sakramenti ya Daraja

Mambo ya Msingi unayotakiwa kufahamu kuhusu Sakramenti ya Daraja

Read More
Mambo ya Muhimu kufahamu kuhusu Ishara ya Msalaba

Mambo ya Muhimu kufahamu kuhusu Ishara ya Msalaba

Read More
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu familia na ndoa?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu familia na ndoa?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu familia na ndoa? Kanisa Katoliki linaamini kuwa familia n... Read More

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi upendo na huruma kwa wengine kama Kristo alivyofanya?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi upendo na huruma kwa wengine kama Kristo alivyofanya?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi upendo na huruma kwa wengine kama Kristo alivyofa... Read More

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kuheshimu uhuru wa dini na kukuza uelewa na amani kati ya dini mbalimbali?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kuheshimu uhuru wa dini na kukuza uelewa na amani kati ya dini mbalimbali?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kuheshimu uhuru wa dini na kukuza uelewa ... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu umoja wa Kanisa?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu umoja wa Kanisa?

Kanisa Katoliki ni moja ya madhehebu makubwa ya Kikristo duniani. Imani yake kuhusu umoja wa Kani... Read More

Maswali yanayoulizwa sana kuhusu Ibada ya Kanisa Katoliki

Maswali yanayoulizwa sana kuhusu Ibada ya Kanisa Katoliki

Read More

Mafundisho kuhusu Toharani

Mafundisho kuhusu Toharani

Read More