Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:34:44 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
• Maziwa ya mama pekee ndio chakula na kinywaji cha mtoto bora zaidi kwa watoto kwa miezi sita ya kwanza. • Ni jambo la muhimu sana kunyonyesha watoto wachanga kwa muda wa miezi minne na uendelee kunyonyesha hadi mtoto atakapofikisha mwaka mmoja na kuendelea.
• Mtoto akifikisha miezi sita ndio wakati muafaka wa kumpa vyakula vya nyongeza vilivyotayarishwakatika hali ya usafi.
• Onana na mnasihi akushauri kuhusu muda na jinsi ya kumuanzishia mtoto wako vyakula vya nyongeza
• Vyakula vya ngogeza viwe ni vya mchanganyiko wa makundi yafuatayo ya chakula:- vyakula vya nafaka, venye asili ya nyama, mbogamboga na matunda, mafuta na sukari (kiasi). Lisha kila chakula kwa siku kadhaa kwa kufuatanisha kabla hujaaza chakula chengine kipya.
• Usimuachilie mtoto alale kama chupa ya maziwa ingali mdomoni, ili kuepukana na kuoza kwa meno na madhara ya.
• Watoto wanaopewa maziwa ya mama pekee hawaugui mara kwa mara, na wakiugua, makali ya ugonjwa hupungua na hupona mapema kwa sababu yale maziwa ya mwanzo ya njano yenye viini vingi vya kumkinga dhidi ya magonjwa.
Updated at: 2024-05-25 10:34:40 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Ndizi mbichi - 10
Nyama - kilo 1
Nazi ya kopo - 1
Chumvi - 1 Kijiko cha chakula
Ndimu - 1
Bizari ya manjano - 1 Kijiko cha chai
Pili pili mbichi - 3
Nyanya (tomatoes) - 2
Kitunguu maji - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi iliyosagwa - 1 Kijiko cha chakula
Namna ya Kutayarisha Na Kupika
Kata nyama vipande vipande na uisafishe. Chemsha nyama weka chumvi, thomu, tangawizi na ndimu. Iache iwive. Kata kata nyanya na kitunguu, kisha mimina kwenye nyama inayochemka, weka na bizari nusu kijiko. Wacha supu iwive kisha weka pembeni. Ukumbusho: Hakikisha supu inakuwa kiasi na si nyingi. Menya maganda ndizi na uzikate vipande vipande vya kiasi. Zikoshe ndizi na uziweke ndani ya sufuria. Weka maji ndani ya sufuria kisha zichemshe ndizi mpaka ziwe laini kidogo. Zimwage maji ndizi kisha mimina supu na nyama ndani ya ndizi. Mimina nazi pili pili na bizari nusu kijiko ndani ya ndizi na uziweke kwenye jiko zichemke mpaka zibakie na urojo kiasi. Onja chumvi na uongeze kadri utakavyopenda. Weka pembeni zipoe. Pakua ndizi kwenye sahani au bakuli tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:34:52 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Maziwa ya unga 2 vikombe
Sukari 3 vikombe
Maji 3 vikombe
Unga wa ngano ½ kikombe
Mafuta ½ kikombe
Iliki kiasi
Jinsi ya kuandaa na kupika
Paka sinia mafuta kabla ya kupika labania Katika sufuria chemsha maji na sukari pamoja na iliki mpaka inate vizuri Kisha mimina mafuta koroga Halafu mimina unga wa ngano na ukoroge haraka haraka Kisha tia unga wa maziwa, endelea kukoroga usiwe na madonge mpaka uwe rangi ya browni isiokoleza. Kisha mimina mchanganyiko kweye sinia uliyoipaka mafuta, iwache ipoe na kata kata upendavo na itakuwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:37:49 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viambaupishi
Mchele 2 Mugs
Mboga mchanganyiko za barafu 1 Mug
(Frozen veg)
Tuna (samaki/jodari) 2 kopo
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi 2 vijiko vya supu
Garam masala 1 kijiko cha supu
Nyanya 2
Kitungu maji 1
Mdalasini nzima 2 vijiti
Karafuu 6 chembe
Pilipili mbichi 1
Chumvi kiasi
Viazi 3
Maji 2 ½ Mugs
Mafuta 3 vijiko vya supu
Jinsi ya kuandaa na kupika
Osha mchele na uroweke kwa muda wa dakika 20 Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown). Mimina viazi, thomu na tangawizi, bizari zote na kaanga. Tia nyanya uliyokatakata ikaange mpaka iwive. Tia tuna endelea kukaanga kidogo tu. Tia maji, yatakapochemka tia mchele. Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa ½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:12 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Mchele wa pishori (basmati) - 4
Nyama ya kuku bila mafupa - 1 Lb
Kamba saizi kubwa - 1Lb
Mchanganyiko wa mboga - njegere, karoti,
mahindi, maharage ya kijani (spring beans) - 2 vikombe
Figili mwitu (Cellery) - 2 mche
Vitunguu vya majani (spring onions) - 4-5 miche
Kebeji - 2 vikombe
Pilipili ya unga nyekundu - 1 kijiko cha chai
Pilipili manga ya unga - 1 kijiko cha chai
Sosi ya soya - 3 vijiko vya supu
Mafuta - 1/4 kikombe
Chumvi - kiasi
MAPISHI
Osha na roweka mchele. Tia kamba chumvi na pilipili nyekundu ya unga. Tia mafuta vijiko viwili katika kikaango (frying pan), kaanga kamba kidogo tu, weka kando. Katakata kuku vipande vidogo vidogo, tia chumvi na pilipili manga. Kaanga kaTika kikaango (ongeza mafuta kidogo) Weka kando. Katika karai, tia mafuta kidogo kama vijiko vitatu vya supu, tia kamba na kuku, tia mboga za mchanganyiko, sosi ya soya na chumvi, kaanga kidogo. (Kama mboga sio za barafu) itabidi uchemshe kidogo. Katakata kebeji, figili mwitu (cellery) na vitunguu vya majani (spring onions) utie katika mchaganyiko. acha kwa muda wa chini ya dakika moja katika moto. Chemsha mchele, tia mafuta kidogo au siagi, chumvi upikie uive nusu kiini, mwaga maji uchuje. Changanya vyote na wali rudisha katika sufuria au bakuli la oveni, funika na upike kwa moto wa kiasi kwa muda wa dakika 15-20 takriban. Epua na upakue katika sahani ukiwa tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:10 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga - 1 Kikombe
Sukari ya kusaga - 3/4 Kikombe
Siagi - 125 gms
Yai - 1
Baking powder - 1/2 kijiko cha chai
Zabibu kavu - 1/2 kikombe
Cornflakes iliyovunjwa (crushed) - 2 Vikombe
Vanilla - 1 kijiko cha chai
MAANDALIZI
Tia kwenye mashine ya kusaga (blender) au mashine ya keki, siagi, yai na vanilla uchanganye hadi ichanganyike vizuri. Tia baking powder, zabibu na unga na changanya vizuri. Paka siagi sinia ya kupikia ya oveni. Tengeneza viduara vidogo vidogo. Weka cornflakes katika sahani ya chali (flat) na zungusha viduara humo kisha upange katika sinia ya oveni. Pika katika moto wa 350ºF kwa muda wa dakika 20-25 hadi vigeuke rangi na viwive.
Jinsi ya kuishi maisha marefu (Mambo ya kuzingatia ili uishi maisha marefu)
Updated at: 2024-05-25 10:34:45 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuishi ukiwa na afya na kuishi maisha marefu kunawezekana kwa kubadili hali ya maisha unayoishi inayoharibu afya yako mfano uvutaji wa sigara, unywaji wa pombe kupita kiasi,kutokufanya mazoezi na kutokula matunda na mbogamboga.
Mambo yanayoweza kukusaidia kuishi maisha marefu ni kama yafuatayo
Kuuandaa mwili kwa maisha marefu kwa kufanya mazoezi
Kuwa makini kutambua na kutibu matatizo ya kiafya
Kuepuka mazingira na kufanya kazi kwa namna au kazi zinazoweza kudhuru maisha yako. Mfano kuendesha gari bila kufuata utaratibu, kutokuvaa vifaa vya kujikinga wakati wa kazi
Epuka vitu vyenye sumu vinavyoweza kudhuru afya yako na kukuletea matatizo ya kiafya kama dawa za mimea na mifugo, zitumie kama inavyotakiwa
Usinywe pombe, usivute sigara wala kutumia dawa za kulevya
Updated at: 2024-05-25 10:34:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Maziwa mazito matamu (condensed milk) - 2 vibati
Sukari - 1 kikombe
Samli 1 ½ kikombe
Vanilla 2 kifuniko cha chupa yake
Hiliki ilosagwa - 2 vijiko vya chai
Sinia kubwa ya bati Paka samli
MAANDALIZI
Changanya maziwa, sukari na samli katika sufuria isiyogandisha chakula (non-stick) uweke katika moto. Koroga huku ikipikika hadi ianze kugeuka rangi na kuanza kuachana. Usiache mkono kuroga isije kufanya madonge. Tia hiliki na vanilla, endelea kuipika. Itakapogeuka rangi vizuri mimina katika sinia na haraka uitandaze kwa mwiko huku ukiuchovya katika maji na kuendelea kuitandaza hadi ikae sawa kote. Pitisha kisu kuikataka ili ikipoa iwe wepesi kuitoa vipande.
Kila inapozidi kupoa na kukaa ndipo fagi inakauka na kumumunyuka.
Updated at: 2024-05-25 10:34:44 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Njia za kupima Afya
Njia mbalimbali hutumika kupima hali ya lishe, njia hizi ni;
1. Vipimo vya umbile la mwili
2. Vipimo vya maabara
3. Kuchukua historia ya ulaji na maradhi
Vipimo vya umbile la mwili
Baadhi ya vipimo ambavyo vinaweza kutumika kutoa tahadhari kuhusu magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza ni;
1. Uwiano wa uzito na urefu au Body Mass Index (BMI).
2. Mzunguko wa kiuno.
3. Uwiano wa mzunguko wa kiuno na nyonga.
4. Kulinganisha uzito na umri.
Uwiano wa uzito na urefu au Body Mass Index (BMI).
Hiki ni kipimo kinachotumika kuangalia uwiano wa urefu na uzito wa mtu, ni muhimu kuchukua vipimo kwa usahihi.Uwiano wa uzito katika Kilogramu na urefu katika mita hupatikana kwa kutumia kanuni ifuatayo:
BMI= uzito (Kg)/Urefu2 (m2)
BMI huwa na viwango mbalimbali vilivyowekwa na shirika la Afya duniani (WHO) kutafsiri hali ya lishe ya mtu ambavyo ni
1. BMI chini ya 18.5 = uzito pungufu.
2. BMI kati ya 18.5 mpaka 24.9= uzito unaofaa.
3. BMI kati ya 25.0 mpaka 29.9 = unene uliozidi.
4. BMI ya 30 au zaidi = unene uliokithiri au kiribatumbo.
Mahitaji ya chakula mwilini hutegemea umri, jinsi, hali ya kifiziolojia (kama ujauzito na kunyonyesha), hali ya kiafya, kazi na mtindo wa maisha. Uzito wa mwili hutegemea na chakula unachokula, pamoja na shughuli unazofanya, mara nyingi unene hutokana na kula chakula kwa wingi. Unene uliokithiri unachangia kwa kiwango kikubwa kupata magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza kama kisukari, magonjwa ya moyo, shinikizo kubwa la damu, na saratani. Uzito uliozidi unapaswa kupunguzwa ili kuepuka magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza
Jinsi ya kupunguza unene uliozidi
1. Tumia mafuta kwa kiasi kidogo kwenye chakula
2. Epuka kula vyakula vyenye mafuta mengi hususani vinavyopikwa kwa kudumbukizwa kwenye mafuta, au vinavyokaangwa kwa mafuta mengi.
3. Epuka matumizi ya vinywaji au vyakula venye sukari nyingi
4. Epuka asusa zenye mafuta mengi au sukari nyingi kati ya mlo na mlo.
5. Ongeza vyakula venye makapi- mlo kwa wingi kama matunda, mboga mboga na nafaka zisizokobolewa.
BMI haitumiki kwa wanawake wajawazito, BMI haitumiki kwa watoto na vijana walio na umri chini ya miaka 18, BMI haitumiki kwa watu wasioweza kusimama vyema, waliovimba miguu, na wanawake wanaonyonyesha katika miezi sita ya mwanzo baada ya kujifungua.