Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Vile unavyoweza kuwa DARAJA au KIKWAZO kwa wengine

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Kwa namna unayoishi unaweza ukawa daraja au kikwazo cha wengine kuishi maisha ya Amani raha na fanaka.
Unaweza ukawa daraja kwa maana kwamba wewe unaweza kuwa sababu ya wengine kupata Baraka na neema za Mungu.
Unaweza kuwa kikwazo kwa maana kwamba unaweza kuwa wewe ni sababu ya wengine kutokupata Baraka na Neema za Mungu.

Kwa jinsi unavyoishi unaweza ukawa chanzo cha Baraka kwa wengine au chanzo cha matatizo na vikwazo kwa wengine.

Vile unavyoweza kuwa Daraja kwa Wengine

Unaweza kuwa daraja au njia ya wengine kupata neema na Baraka katika maisha yao kulingana na matendo yako mema na Ibada yako kwa Mungu.

Kwa ucha Mungu wako, watu wako unaowapenda sana wanaweza kubarikiwa na kupata neema za Mungu Pamoja na wewe. Wale watu unaochangamana nao watabarikiwa kwa sababu na wewe umebarikiwa.
Kwa mfano wewe kama ni mzazi mcha Mungu unaweza ukawa chanzo cha Baraka na neema kwa watoto wako na kwa mwenzi wako wa ndoa. Vivyo hivyo na kwa watoto, mtoto anaweza kuwa chanzo cha Baraka kwa wazazi wake.

Inawezekana kuna Amani katika familia yako kwa sababu tuu wewe ni miongoni mwa wanafamilia hiyo na hivyo Mungu ameachilia Amani katika familia yako kwa sababu tuu wewe upo pale na wewe ni mcha Mungu.

Unaweza kuona sasa wewe ni chanzo cha Baraka kwa wale watu wako wa karibu. Kwa sababu tuu wewe ni mcha Mungu, na wao wanabarikiwa pamoja na wewe. Mungu anapobariki familia yako na wao pia wanabarikiwa.

Kwa hiyo basi, unapolegalega katika ucha Mungu wako unaweza pia kusababisha kulegalega au kikwazo cha Baraka za wengine.

Vile unavyoweza kuwa Kikwazo kwa Wengine

Unaweza kuwa kikwazo au kizuizi cha wengine kupata neema na Baraka katika maisha yao kulingana na matendo yako mabaya na kukosa kwako kumcha Mungu.

Kwa kuacha kumcha Mungu, watu wako unaowapenda sana wanaweza kukosa kubarikiwa na kukosa neema za Mungu kwa sababu wewe unazuia Baraka hizo. Wale watu unaochangamana nao watakosa Baraka kwa sababu umeandikiwa kutokubarikiwa na wanachanganyikana na asiyestahili kubarikiwa.

Kwa mfano wewe kama ni mzazi asiyemcha Mungu unaweza ukasababisha watoto wako wakashindwa kubarikiwa kwa sababu tuu kwa udhambi wako unazuia Baraka kwa familia yako yote wakiwemo watoto wako. Vivyo hivyo na wazazi wanaweza wakashindwa kubarikiwa kwa sababu watoto wao wanawazuilia Baraka zao.

Inawezekana hakuna Amani katika familia yako kwa sababu tuu wewe ni miongoni mwa wanafamilia hiyo. Kunakosekana Amani katika familia yako kwa sababu tuu wewe upo pale na wewe ni mdhambi/ mtu asiyemcha Mungu.

Unaweza kuona sasa wewe ni chanzo cha kukosekana Baraka kwa wale watu wako wa karibu. Kwa sababu tuu wewe ni mtu asiye mcha Mungu, na wao wanazuiliwa baraka pamoja na wewe. Mungu anapoacha kuibariki familia yako na wao pia wanakosa baraka. Kwa mfano unapokosa Amani na Mafanikio ukae ukijua kuwa wale unaowapenda na wanaokutegemea nao watakosa Amani na hawatanufaika kwa sababu hauna mafanikio.

Mwisho

Wewe ni kama Kiungo cha myororo wa Baraka au laana kwa wale uwapendao hasa familia yako. Ukibarikiwa unabarikiwa pamoja nao, ukilaaniwa unalaaniwa pamoja nao.

Kwa sababu hiyo, mara zote chagua kuishi kwa kumcha Mungu kwa sababu huwezi jua ni wangapi walioko nyuma yako na wanaobarikiwa kwa sababu ya ucha Mungu wako.

Mche Mungu kwa juhudi zote kwa sababu hujui ni wangapi wanaonufaika na ucha Mungu wako. Vilevile jitahidi usiwe mdhambi sana kwa sababu huwezi kujua ni wangapi wanaokosa Baraka za Mungu kwa udhambi wako.

Kumcha Mungu kuna faida kwako na kwa wengine, hasa unaowapenda. Kuto kumcha Mungu ni hasara kwako na kwa wale unaowapenda hasa familia yako

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 101

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest Jul 18, 2024
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ DANFORD MAGECHE Guest Jul 10, 2024
ASANTE.
πŸ‘₯ George Tenga Guest May 13, 2024
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Alice Jebet Guest May 8, 2024
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Feb 3, 2024
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Jan 15, 2024
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Dec 3, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Nov 10, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Philip Nyaga Guest Sep 13, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Sep 6, 2023
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Jul 8, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Faith Kariuki Guest Jun 27, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest May 24, 2023
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest May 6, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Apr 5, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Victor Mwalimu Guest Mar 15, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Jan 23, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Dec 16, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Victor Mwalimu Guest Dec 12, 2022
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Nov 8, 2022
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Sep 26, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Janet Sumaye Guest Jul 20, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Apr 28, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Apr 27, 2022
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ John Lissu Guest Mar 27, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Feb 27, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest Dec 30, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Diana Mallya Guest Dec 29, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest Dec 19, 2021
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest Dec 7, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Nov 24, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ John Malisa Guest Nov 18, 2021
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Nov 12, 2021
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ George Mallya Guest Nov 4, 2021
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Sep 19, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Philip Nyaga Guest Aug 2, 2021
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Jul 13, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Mary Sokoine Guest Jun 29, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Mariam Hassan Guest Jun 2, 2021
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Apr 21, 2021
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Mar 15, 2021
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Mar 2, 2021
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Jane Muthoni Guest Jan 26, 2021
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Nov 6, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Oct 10, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Oct 9, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Jul 27, 2020
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Jul 1, 2020
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest May 31, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest May 15, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Apr 25, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Mar 25, 2020
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ John Malisa Guest Mar 18, 2020
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Mar 12, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Mar 6, 2020
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Jacob Kiplangat Guest Mar 2, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ John Lissu Guest Feb 26, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ James Malima Guest Feb 5, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Dec 26, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Oct 1, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About