Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.

Ee Yesu uliyesema β€œKweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwa”, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema β€œKweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewa”, tazama kwa jina lako ninaomba ……. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema β€œKweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe”, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.

Sali β€˜Salamu Malkia’ na kuongezea, β€˜Mtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombee’.

P.S. – Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Sep 20, 2017
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Aug 24, 2017
πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Aug 13, 2017
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Jul 16, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest Jun 30, 2017
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ James Mduma Guest Jun 3, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest May 29, 2017
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Apr 30, 2017
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Dec 5, 2016
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Lydia Mahiga Guest Nov 14, 2016
πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Sep 8, 2016
πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Aug 11, 2016
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Aug 11, 2016
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Jul 11, 2016
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ Diana Mallya Guest Apr 11, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Joseph Mallya Guest Dec 4, 2015
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest Nov 5, 2015
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Oct 23, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Sep 23, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Aug 25, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest May 23, 2015
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest May 7, 2015
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest Apr 3, 2015
πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About