VIAMBAUPISHI
Unga wa ngano 1Β 1/2 Kikombe
Baking powder 1 Kijiko cha chai
Baking soda ΒΌ Kijiko cha chai
Chumvi Β½ kijiko cha chai
Sukari 1 kijiko cha supu
Hamira 1/2 Kijiko cha supu
Yai 1
Maziwa Β½ Kikombe
Mafuta ya kukaangia
VIAMBAUPISHI:SHIRA
Sukari 1 Kikombe
Maji Β½ Kikombe
Iliki au Mdalasini ΒΌ kijiko cha chai (ya unga)
MAANDALIZI NA JINSI YA KUPIKA
1. Kwenye bakuli, changanya pamoja unga, baking powder, baking soda, chumvi, sukari na hamira.
2. Katika kibakuli, piga mayai na maziwa pamoja.
3. Changanya mchanganyiko wa mayai na wa unga ; na ukande kama unga wa maandazi.
4. Ikisha fura, sukuma unga kama wa maandazi na ukate mitai .
5. Pasha moto mafuta na uchome hadi iwe rangi ya dhahabu, upande zote mbili.
6. Ipikie shira lakini isiwe nzito .
7. Tia mitai na upepete hadi sukari ienee kote na zitakuwa tayari kuliwa.
No comments yet. Be the first to share your thoughts!