Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Amri Kumi za Mungu: Mambo ya Msingi unayopaswa kufahamu

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Amri kumi za Mungu ni zipi?

1. Ndimi Bwana, Mungu wako usiabudu miungu wengine.
2. Usiape bure kwa jina la Mungu wako.
3. Fanya siku ya Mungu

4. Waheshimu Baba na Mama, upate miaka mingi na heri duniani.
5. Usiue
6. Usizini
7. Usiibe
8. Usiseme uongo
9. Usitamani mwanamke asiye mke wako.
10. Usitamani mali ya watu.


Je, ni lazima kila mtu ashike Amri kumi za Mungu?

Ndiyo. Ni lazima kila mtu ashike Amri kumi za Mungu hata kama si Mkristo kwa sababu Mungu ni mkubwa wa watu wote. (Kut 20:1-17, Kumb 5:1-21)


Kwa nini Mungu alitupa Amri kumi?

Mungu alitupa amri kumi ili kutufudisha mambo yatupasayo kwa Mungu, kwa watu na kwetu sisi wenyewe


Katika amri ya kwanza ya Mungu tumeamriwa nini?

Tumeamriwa tusadiki kuwa Mungu ni mmoja, ndiye Baba yetu na Mkubwa wetu: tumpende, tumwabudu yeye peke yake. (Mt 10:33, Kumb 6:4-9)


Wakatoliki tunamwabudu Mungu kwa namna gani?

Tunamwabudu Mungu kwa sala , sadaka na matendo mema


Katika amri ya kwanza ya Mungu tumekatazwa nini?

Tumekatazwa kumdharau Mungu na kuweka imani yetu katika viumbe badala ya Mungu.


Je, kuna viumbe ambavyo tunaviheshimu kwa kumtukuza Mungu?

Ndiyo twamuheshimu Bikira Maria, Malaika na Watakatifu.


Kwa nini yatupasa kuwaheshimu Watakatifu?

Kwa sababu hao ni washindi, rafiki wa Mungu na waombezi wetu.


Je, tuna ruhusa ya kuwaabudu Watakatifu?

Hatuna ruhusa ya kuwaabudu Watakatifu tunawaheshimu tu.


Je sanamu zimekatazwa?

Sanamu hazijakatazwa, ila tunaziheshimu kwa sababu zinatukumbusha Mungu na Watakatifu. (Kut 25:18-22).

18 Nawe fanya makerubi mawili ya dhahabu; uyafanye ya kazi ya kufua, katika hiyo miisho ya kiti cha rehema, huku na huku. 19 Weka kerubi moja mwisho mmoja, na kerubi la pili mwisho wa pili; fanya hayo makerubi ya kitu kimoja na kiti cha rehema, mwisho huku na mwisho huku. 20 Na hayo makerubi yatainua mabawa yao juu, na kukifunika hicho kiti cha rehema kwa mabawa yao, na nyuso zao zitaelekeana hili na hili; nyuso za hayo makerubi zitaelekea kiti cha rehema. 21 Weka kiti cha rehema juu ya hilo sanduku, kisha utie huo ushuhuda nitakaokupa ndani ya sanduku. 22 Nami nitaonana nawe hapo, na kuzungumza nawe pale nilipo juu ya kiti cha rehema, katikati ya hayo makerubi mawili yaliyo juu ya sanduku la ushuhuda, katika mambo yote nitakayokuagiza kwa ajili ya wana wa Israeli. Kutoka 25 :18-22.

Vile vile Mungu alishawahi kuwaagiza Waisraeli Wachonge sanamu ya nyoka na yeyote atakayeumwa na nyoka akiiangalia atapona.


Mfano wa sanamu takatifu ni zipi?

Sanamu ya Bikira Maria, Mtoto Yesu, Mt. Yosefu, Moyo wa Yesu na za Watakatifu.


Ni nanai ana kosa kumuabudu Mungu?

Anayekosa kumuabudu Mungu ni yule;

1. Anayeacha kusali au anayesali hovyo
2. Anayemkufuru Mungu
3. Anayeamini na kushika mambo ya kipagani


Mambo gani yanavunja amri ya kwanza ya Mungu?

Mambo hayo ni;

1. Kuabudu sanamu
2. Kufanya matambiko
3. Kwenda kwa waganga
4. Kupiga bao au ramli
5. Kuvaa hirizi
6. Kushiriki mambo ya kichawi n.k.


Ni nini maana ya kuabudu sanamu?

Kuabudu sanamu ni kukipa kiumbe chochote heshima au upendo anaostahili Mungu peke yake.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Jul 17, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Andrew Mahiga Guest May 22, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Dec 20, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Dec 10, 2023
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ John Malisa Guest Nov 8, 2023
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Victor Malima Guest Oct 31, 2023
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Apr 8, 2023
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Jan 29, 2023
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest Jan 23, 2023
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Nov 15, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Elijah Mutua Guest Oct 12, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Jul 15, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Peter Tibaijuka Guest Apr 24, 2022
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Apr 2, 2022
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest Jan 30, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Sep 16, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Victor Malima Guest Sep 5, 2021
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Aug 6, 2021
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Jul 29, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Jun 12, 2021
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Apr 14, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Jacob Kiplangat Guest Jan 6, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Oct 28, 2020
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Sep 27, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ John Kamande Guest Sep 15, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Jul 18, 2020
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Jul 6, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Mary Kidata Guest Jun 29, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Apr 22, 2020
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ George Ndungu Guest Feb 22, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Oct 9, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Victor Kamau Guest Aug 10, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Jun 29, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Francis Njeru Guest May 29, 2019
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest May 10, 2019
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Feb 4, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Mar 17, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Nov 26, 2017
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest Nov 19, 2017
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Oct 24, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Sep 30, 2017
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest Apr 28, 2017
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Apr 1, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ George Tenga Guest Aug 17, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Apr 25, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest Sep 16, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Lydia Mahiga Guest Aug 14, 2015
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Jun 22, 2015
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ George Wanjala Guest Jun 7, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest May 26, 2015
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About