Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Mungu Anakuita Na Kukupa Nafasi Ya Kutubu Na Kumrudia Yeye Ili Akusamehe na Kukubariki

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Ingekuwa heri leo msikie sauti yake! Msifanye migumu mioyo yenu. Zab 95:7-8

Tunaalikwa kutubu na kumrudia Mungu kwa Mioyo yetu yote na kwa nia dhabiti. Mungu ni mwaminifu, atatusamehe dhambi zetu na kutufanya kuwa wapya.

Dawa ya dhambi ni kutubu na kusamehewa.

Kutubu sio kusema tuuΒ "Ninatubu"Β auΒ "Ninaomba msamaha". Kutubu ni kuona uchungu kweli rohoni kwa dhambi tulizotenda, tukizikataa na kunuia kutokuzitenda tena.

12β€œLakini hata sasa,”
nasema mimi Mwenyezi-Mungu,
β€œNirudieni kwa moyo wote,
kwa kufunga, kulia na kuomboleza.
13Msirarue mavazi yenu kuonesha huzuni
bali nirudieni kwa moyo wa toba.”
Mrudieni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu;
yeye amejaa neema na huruma;
hakasiriki upesi, ni mwingi wa fadhili;
daima yu tayari kuacha kuadhibu.
14Huenda Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atabadili nia
na kuwapeni baraka ya mazao,
mkamtolea sadaka za nafaka na kinywaji.
15Pigeni tarumbeta huko Siyoni!
Toeni amri watu wafunge;
itisheni mkutano wa kidini.
16Wakusanyeni watu wote,
wawekeni watu wakfu.
Waleteni wazee,
wakusanyeni watoto,
hata watoto wanyonyao.
Bwana arusi na bibi arusi
na watoke vyumbani mwao.
17Kati ya madhabahu na lango la hekalu,
makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu,
walie na kuomba wakisema:
β€œWahurumie watu wako, ee Mwenyezi-Mungu.
Usiyaache mataifa mengine yatudharau
na kutudhihaki yakisema,
β€˜Yuko wapi basi Mungu wao?’” Yoeli 2:12-17

Uzuri wa Mungu ni kwamba anasamehe na kusahau, tunapotubu dhambi zetu Mungu anatufutia makosa yetu, anaponya majeraha au madhara yaliyoletwa na dhambi hiyo na kisha antubariki kwa Neema na Vipawa vya kusonga Mbele.

Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena dhambi zao.” Yeremia 31:34

Mungu anatambua kwamba Binadamu ni dhaifu na anaweza kuanguka dhambini ndio maana anatupa nafasi ya Kutubu na Kumrudia yeye.

13Afichaye makosa yake hatafanikiwa;
lakini anayeungama na kuyaacha atapata rehema.Β Methali 28:13

Mungu anazifahamu juhudi zetu katika kutafuta kutenda mema ndio maana anakubali toba ya kweli na anatupa matumaini ya kusonga mbele.

"Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu".Β Isaya 1:18

Biblia inatuambia kuwa anaheri yule atubuye na kusamehewa kosa lake kwa sababu hana hatia mbele ya Mungu.

1 Heri yake mtu aliyesamehewa kosa lake,
mtu ambaye dhambi yake imeondolewa kabisa.
2Heri mtu ambaye Mwenyezi-Mungu hamwekei hatia,
mtu ambaye hana hila moyoni mwake.Β Zaburi 32:1-2

Tunapaswa kukumbuka kuwa toba ya kweli ya kutupa msamamaha inaambatana na kuwasamehe wengine na kuondoa kinyongo kwa wengine waliotukosea. Yesu anatufundisha kuwa inatupasa tusamehe ili na sisi tusamehewe.

14β€œMaana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe nyinyi pia. 15Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe nyinyi makosa yenu.Β Mathayo 6:14-15

Tena, Mungu anatusamehe Makosa Yetu bila kujali tunakosea Mara nagpi na tunarudi kwake mara ngapi. Ndio maana Yesu alitufundisha kuwa tunapokosewa na wenzetu ni lazima tuwasamehe haijalishi wametukosea mara ngapi.

3Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, muonye; akitubu, msamehe. 4Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema, β€˜Nimetubu,’ lazima umsamehe.” Luka 17:3-4

Unapotubu na kuomba msamaha ni sharti uwasamehe pia wale waliokukosea ili na wewe usamehewe. Kusameheana na wenzetu ndio tabia ya Kimungu ambayo yatupasa kujifunza na kuiishi ili na sisi tuwe watoto wema wa Mungu.

12Nyinyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo, basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu. 13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe nyinyi.Β Wakolosai 3:12-13

Tumuombe Mungu atujalie Moyo wa toba na kujirudi kwake Kila tunapokosea. Na tumuombe pia atupe nguvu na uwezo wa kuwasamehe wale wanaotukosea.

KUMBUKA:Β Unapotubu dhambi zako na kusamehewa ndipo inapokuwa rahisi kwa sala zako kujibiwa. Mungu ni rafiki ya waliosafi Moyoni, na ndio anaowasikiliza na kuwaonyesha nguvu na uwezo wake.

Nakualika kwa Sala ya Toba, uweze kurudi kwa Mungu. Sali kutoka moyoni, kwa kujua kuwa unapendwa na Mungu, Kwa Imani na Matumaini Kwake.

Sala ya Toba

Mungu wangu, Baba wa mbinguni, nakuja mbele zako nikiwa na moyo uliovunjika na toba ya kweli. Nakiri kuwa mimi ni mwenye dhambi, na nimekosa mbele zako kwa njia nyingi. Nimefanya mambo ambayo hayakupendeza, na nimeshindwa kutenda yale uliyoniagiza. Kwa kuwa Neno lako linasema, "Kwa maana wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu" (Warumi 3:23).

Ee Bwana, naomba unisamehe dhambi zangu zote. Nimetenda dhambi kwa mawazo, kwa maneno, na kwa matendo. Ninatubu kwa dhati na kwa kweli kutoka moyoni mwangu. Naomba unioshe kwa damu ya Yesu Kristo, Mwanao mpendwa, ambaye alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu. Kama unavyosema katika Neno lako, "Lakini ikiwa tutatembea katika nuru kama Yeye alivyo katika nuru, tu ushirika sisi kwa sisi, na damu yake Yesu Kristo, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote" (1 Yohana 1:7).

Ninakiri kuwa mimi ni mnyonge bila wewe, na siwezi kufanya lolote bila msaada wako. Naomba unijaze na Roho Mtakatifu, aniongoze na kunipa nguvu ya kushinda majaribu na dhambi. Ee Mungu, niongoze katika njia zako za haki, na unisaidie kuishi maisha yanayokupendeza. Kwa kuwa Neno lako linasema, "Basi kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu" (Wakolosai 3:1).

Ninakuja mbele zako nikiwa na unyenyekevu na moyo wa toba. Naomba unirehemu na unifanye kuwa kiumbe kipya ndani ya Kristo. Kama unavyosema katika Neno lako, "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama! yamekuwa mapya" (2 Wakorintho 5:17). Asante kwa upendo wako usio na kikomo, na kwa neema yako inayotosha kila siku. Naomba haya yote kwa jina la Yesu Kristo, aliye Mwokozi wangu.

Bwana, naomba unifundishe kuwa mtiifu na kuwa na moyo wa shukrani kwa kila jambo. Acha neno lako likae kwa wingi ndani yangu, na linibadilishe kutoka ndani hadi nje. Nisaidie kuacha njia zote za dhambi, na kuwa mwaminifu kwako katika kila hali. Kwa kuwa Neno lako linasema, "Neno lako nimeliweka moyoni mwangu, nisije nikakutenda dhambi" (Zaburi 119:11).

Ninakubali kuwa mimi ni mnyonge na ninahitaji msaada wako kila siku. Nakiri dhambi zangu na naomba unisamehe. Naomba unipatie moyo safi, na kunifufua kiroho. Kama unavyosema katika Neno lako, "Ee Mungu, uniumbie moyo safi, unirejeshee roho iliyotulia ndani yangu" (Zaburi 51:10). Naomba unifanye kuwa mwanga na chumvi duniani, ili niweze kuonyesha upendo wako kwa wengine. Kwa kuwa Neno lako linasema, "Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima" (Mathayo 5:14).

Asante, Bwana, kwa kusikia sala yangu. Naamini kuwa umesikia na kujibu ombi langu. Ninatangaza kuwa mimi ni wa Kristo, na ninakubaliana na mapenzi yako maishani mwangu. Kama unavyosema katika Neno lako, "Ninaweza kufanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu" (Wafilipi 4:13). Kwa jina la Yesu, Amina.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 100

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Jul 13, 2024
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest Mar 28, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Ann Wambui Guest Nov 9, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Sep 8, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Jul 30, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Victor Mwalimu Guest Jun 15, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Mar 26, 2023
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Mar 18, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ James Kimani Guest Feb 28, 2023
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Feb 1, 2023
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest Dec 15, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Stephen Amollo Guest Oct 20, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Diana Mumbua Guest Jul 29, 2022
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Francis Njeru Guest Jul 2, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Jun 26, 2022
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Jun 6, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Jan 25, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Jan 19, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Dec 30, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ James Kimani Guest Dec 29, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Nov 29, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Oct 19, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Aug 31, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Agnes Njeri Guest Aug 22, 2021
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Jul 23, 2021
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Catherine Mkumbo Guest Jul 16, 2021
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Jul 15, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Jane Muthoni Guest May 31, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest May 1, 2021
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Apr 7, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Michael Mboya Guest Mar 8, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Feb 20, 2021
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Jan 11, 2021
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest Dec 16, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Dec 10, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Jane Muthui Guest Oct 16, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Diana Mumbua Guest Jun 27, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Jun 22, 2020
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ James Kimani Guest Mar 24, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Mar 15, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Feb 23, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Nov 23, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Grace Njuguna Guest Oct 17, 2019
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Grace Njuguna Guest Sep 20, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Aug 26, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Grace Minja Guest Jul 18, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Jul 2, 2019
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Thomas Mtaki Guest Jun 28, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Jun 17, 2019
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Jun 9, 2019
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ David Ochieng Guest Apr 10, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest Mar 18, 2019
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Mary Kidata Guest Jan 23, 2019
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ David Ochieng Guest Dec 30, 2018
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Dec 4, 2018
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ John Malisa Guest Nov 25, 2018
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Nov 2, 2018
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Emily Chepngeno Guest Sep 22, 2018
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest Aug 27, 2018
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest Aug 2, 2018
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About