Leo nimekuandalia Tafakari kuhusu Mambo yanayowazuia Waumini na watumishi wa Mungu Kuishi Kitakatifu na kufikia Ukamilifu. Mambo haya yanaweza yakaonekana sio dhambi au makosa kwa mtu lakini ni vikwazo kwa mtu kufikia Ukamilifu hasa anaposhindwa kuyajua na kuyaepuka. Wengi wanajiona kwamba wako salama lakini kumbe wako katika dhambi.
Mambo hayo ni kama ifuatavyo;
1. MAJIVUNO
Hii ni hali ya kujiona wa thamani sana, wakipekee na unayestahili sana.
Tofauti ya MAJIVUNO na pointi ya pili hapo chini (UMIMI) ni kwamba MAJIVUNO ni kujiona wa thamani lakini huku unatambua Yupo Mungu anayekuzidi. UMIMI ni kujiona kama Sawa na Mungu.
Kwa yale unayoyafanya: Kujiona kwamba wewe ni wa thamani na kipekee sana kwa yale uliyowahi kufanya, unayoyafanya na unayoweza kufanya. (I did, I do, I will do.)
Kwa vile Ulivyo: Kujiona kuwa wewe ni wa kipekee kwa vile ulivyo. Kusahau kuwa Vile ulivyo na vile ulivyonavyo Umepewa Bure na Mungu.
Kwa vile unavyofanyiwa: Kujiona kuwa wewe ni wa kipekee kulingana na wengine wanavyokuona na vile wanavyokufanyia.
Tafakari na ushauri kuhusu Majivuno
Unavyosoma kuwa majivuno ni hali ya kujiona wa thamani sana, wakipekee na unayestahili sana, unaweza ukafikiri sio kosa wala dhambi kujiona hivyo. Lakini makosa yanakuja kwa yale unayoyafanya kwa Majivuno hayo na kujisikia huko.
Majivuno yanakuwa dhambi pale tunapotenda kwa Majivuno na kujiona. Pale tunaposahau kwamba Upekee wetu sio kwamba tulistahili bali ni kwa Neema tuu. Tunakosea pale tunapoanza kuzarau wengine wale wasio kama sisi.
Unaweza ukafikiri kwamba hauna Majivuno lakini miongoni mwa dalili za Majivuno ni kama ifuatavyo;
1. Zarau
2. Kushindwa Kujishusha
3. Kujigamba/ Kujisifu
4. Kupenda upendeleo
5. Kujiona wa Tofauti
Ukiona kuna wakati una dalili kama hizi ujue tayari Majivuno yanajipandikiza ndani yako. Ninaposema Majivuno ni dhambi namaanisha kuwa matokeo/ matendo yanayotokana na dalili/ sifa hizi ndiyo dhambi.
Mambo ya kuzingatia kushinda Majivuno
Unyenyekevu⦠Unyenyekevu⦠Unyenyekevu ndio dawa ya Majivuno.
Utaweza kushinda majivuno kwa Kujishusha na kujiona sawa na wengine.
Unaweza ukashinda Majivuno kwa Kutambua kuwa Vile ulivyo, yale unayoweza kufanya na vile unavyofanyiwa ni Baraka za Mungu tuu. Haimaanishi kuwa umestahili sana kuwa hivyo.
Utashinda majivuno unapotambua kuwa hata wale unaowaona wako chini yako wangeweza kuwa kama wewe tuu. Ni maisha na Mipango ya Mungu ndio iliyofanya ukawa hivyo. Haimaanishi kwamba ni juhudi yako wewe. Wapo wenye Juhudi kuliko wewe lakini wapo chini yako.
2. UMIMI
Kujiona kuwa wewe ni wewe na wewe ni wa kipekee na unastahili kuliko wengine.
Tofauti kubwa na pointi ya kwanza hapo juu ni kwamba UMIMI ni Zaidi ya MAJIVUNO. Ni kujiona Hakuna wa Zaidi yako na wewe unahadhi sawa karibu na Mungu.Β Yaani, Mungu yupo lakini Mimi Pia nipo.
Kwa cheo, kipawa au mamlaka yako: Kujiona kwa cheo, kipawa au Mamlaka yako hakuna anayekuzidi, Mara nyingine kufikiri kwamba hata Mungu mwenyewe hawezi kukuondolea/ kukupinga. Ni kufikiri kwamba hakuna anayeweza kupinga maamuzi yako na hakuna wa kuamua Juu/ Zaidi yako.
Kwa unayoyafanya: Kuona kwamba kwa yale unayoyafanya hakuna kama wewe. Hakuna anayeweza kufanya kama wewe.
Kwa unayofanyiwa: Kuona kwamba hakuna anayestahili kufanyiwa kama wewe.
Kwamba Unaweza kufanya chochote: Kudhani kwamba unaweza kufanya chochote kile kwa sababu wewe ni wewe.
Tafakari na ushauri kuhusu UMIMI
Ninapoongelea Umimi siwalengi wenye mamlaka Makubwa ya juu tuu, Nalenga pia mtu mmoja mmoja kwa sababu kila mtu anayo mamlaka na Mwili na Utu wake. Unayo kipawa cha utu wako, uwanaume wako, uwanawake wako, Uzima wako. Vile vile Mamlaka ya Familia yako, jumuiya, ukoo n.k. Unamamlaka ya mwili wako na kwa hiyo kwa mwili huo usiutumie kwa uovu kwa sababu tuu umepewa mwili huo.
Kwa hiyo basi, ninapoongelea UMIMI naanzia chini kabisa kwenye Mamlaka na Mwili wako na Utu wako mpaka kwenye ngazi za jamii Kama Vyeo vya Kijamii na Kiinjili.
Unaweza ukadhani kwamba UMIMI sio makosa lakini makosa yanazaliwa pale unapotenda kwa kufuata umimi wako (Vile ulivyo). Dhambi inakuja pale Kwa sababu ya mamlaka yako unapoamua mambo kwa sababu unajua hakuna wa kukupinga. Kwa sababu ya uwezo wako wa kufanya mambo kufanya vitu kwa ubaya kwa sababu tuu unajua hakuna anayekuzidi/ anayeweza kufanya kama wewe/ anayeweza kukuzuia.
Dhambi inatokana na Kujiona kwako kuwa hakuna anayekuzidi kunakupelekea kushawishika kufanya mambo mengine ili kudhihirisha kuwa hakuna anayekuzidi kweli. Hasa kwa uonevu na ubabe.
UMIMI unaanza kuzaa dhambi pale mtu anapomsahau Mungu wake aliyemuumba na Kumpa huo UMIMI (Kumfanya vile alivyo). Unaposahau kuwa yupo Mungu aliyekupa hayo mamlaka, kipaji, kipawa na cheo ndipo unapoweza kuanza kukosea kwa UMIMI.
Mambo ya kuzingatia kushinda UMIMI
Kushinda UMIMI inahitaji unyenyekevu wa kujitambua kuwa Mamlaka, Kipaji, Kipawa au cheo chako Umepewa na Mungu na Unatakiwa Ukitumie kwa Mapenzi ya Mungu.
Ukitaka kuushinda UMIMI unapaswa kutambua kwamba yote yana Mwisho.
Vile vile unatakiwa ujue kuwa Ipo siku utatolea hesabu kwa kile ulichopewa. Ipo siku utaulizwa kwamba Umefanya nini na Mamlaka, Kipaji, Kipawa au cheo chako. Ndio maana wenye hekima wanaogopa sana kuwa na Mamlaka, Kipaji, Kipawa au cheo kwa sababu wanajua kuwa wanayo kazi kubwa kuliko wale wasiokuwa nacho.
Ukitambua kwamba unawajibika kwa vile ulivyo, basi ujitahidi kutenda kwa kumpendeza Mungu.
KUMBUKA Vile ulivyo inaweza kuwa njia rahisi ya kuufikia Ukamilifu na Utakatifu au inaweza ikawa Mtego kwako kwa kufikia Ukamilifu na Utakatifu. Ni wewe tuu kuamua Unaishije kwa Vile Ulivyo.
3. HASIRA, UKOROFI NA CHUKI
Hasira: Kukasirika haraka kwa kukosa uvumilivu na kutokutambua kuwa unapoishi na binadamu wengine ni lazima/ kawaida kukwazika. Watu hawawezi kufanya yote unayoyataka.
Ukorofi: Kuwa mbabe na kuweka vizuizi na masharti ya kiukorofi, pamoja na kufanya vitendo vya ukorofi na ukaidi kwa walio chini yako na hata walio juu yako.
Chuki: Kuwa na kinyongo na uchungu na watu wengine ambapo matokeo yake ni kufanyiana vitendo vya kikatili huku ukiwaza kuwa ni halali yako.
Tafakari na ushauri kuhusu Hasira, Ukorofi na chuki
Hasira, Ukorofi na chuki ni mambo ambayo mara nyingi yanaweza kuonekana sio dhambi moja kwa moja ila matokeo yake ndio yanaonekana kuwa ni dhambi. Hii ni kwa sababu kwa hali ya kawaida ya binadamu ni kawaida kwa mtu kuwa na Hasira, Ukorofi na chuki lakini vile anavyotenda baada ya kupata hasira au chuki inayopelekea ukorofi ndio inayosababisha mambo haya kuzaa dhambi.
Jambo lililo baya Zaidi ni kwamba dhambi inayotokana na Hasira, Ukorofi na chuki mara nyingi huonekana kama ni halali na haki ya mtu. Kwa Mfano, watu wengi wanaona kuwa ni kawaida kuwa mtu akikukasirisha lazima umfanyizie/ umtendee kitu kibaya. Wengine wanafikiri kuwa mtu anapokukasirisha lazima umuonyeshe ubabe. Na wengine wanaona ni kawaida kabisa kuwa na chuki na kinyongo hasa wanapotendewa visivyo na kuhisi kuwa ni haki yao kuchukia na kuwa na Kinyongo.
Lakini ukweli ni kwamba matendo yote yanayotendwa kwa Hasira, Ukorofi na chuki ni dhambi na makosa mbele ya Mungu. Kushindwa kuzuia Hasira, Ukorofi na chuki ni chanzo kikubwa cha dhambi kwa Wakristu walio wengi hasa Watumishi wa Mungu.
Makosa na dhambi za Hasira, Ukorofi na chuki yanawakoseha Neema za Mungu Watumishi wengi wa Mungu kwa sababu wengi wao hawaoni kama ni dhambi au ni makosa kufanya jambo kwa Hasira, Ukorofi na chuki. Wapo waumini na Watumishi wengi wa Mungu ambao wanaweza kufwatilia kikamilifu matakwa yote ya Imani yao lakini wanalegalega katika Imani yao kwa sababu ya kushindwa kutambua na kujiepusha na makosa na dhambi zitokanazo na Hasira, Ukorofi na chuki.
Mambo ya kuzingatia kushinda Hasira, Ukorofi na chuki
Kushinda Hasira
Ili kushinda hasira ni muhimu kuishi kwa kujua wakati wowote ule yupo mtu anaweza kukukosea.
Ni vizuri kuelewa kua wote wanaokukosea hawakukosei kwa kupenda au kwa kusudi. Ni lazima kutambua Katika maisha kuna mambo mengi yanayoweza yakafanya mtu akukosee au kukukwaza wewe. Huu ndio uhalisia wa Maisha.
Ni vizuri kujua kuwa Hasira ni hali inayoweza kuzimwa ukiamua kuizima na ni hali inayoweza kuwaka sana ukiamua kuiwasha. Sasa ni wewe kuchagua kuizima au kuiwasha.
Muhimu Zaidi kukumbuka ni kwamba Umeitwa Kuishi upendo wa Mungu na wa Jirani kwa maana hii umeitwa kusamehe na kuvumilia wengine huku ukiwaongoza na kuwaelekeza kile kinachotakiwa.
Kushinda Ukorofi
Namna kuu ya kushinda ukorofi ni kuwa mvumilivu. Kuwa mvumilivu na kuweza kuachilia (Kupotezea).
Unaweza kushinda ukorofi kwa Kutambua kuwa sio mara zote ni lazima kushindana na kubishana.
Kushinda Chuki
Kushinda chuki ni ngumu sana hasa unapokuwa tayari na katabia ka kuweka kinyongo au kuona uchungu/ wivu.
Wewe kama Mtumishi wa Mungu unaweza kushinda chuki kwa kujiepusha na tabia ya Kushindana na Kujilinganisha.
Chuki ni tabia au mazoea na kwa sababu hiyo unapotaka kuishinda unatakiwa ujijengee tabia na mazoea ya kinyume chake ambayo ni kujiepusha na mashindano na Kujilinganisha.
Zaidi sana, chuki inaweza kushindwa kwa ukarimu. Unapokua mkarimu unashinda chuki na wivu. Vilevile kwa ukarimu huu unaweza ukazuia chuki ya watu wengine. Utawasaidia wengine wasiwe na chuki na wewe pia, huku na wewe unajizuia na chuki.
MWISHO
Katika mambo yote haya Matatu unaweza ukaona kuwa naongelea Dhambi ya asili ya Binadamu. Dhambi ya Asili ya Binadamu ya Kujiona (PRIDE). Kila binadamu anazaliwa kwa kiasili akiwa na hali ya kujiona (PRIDE). Kila binadamu anazaliwa akiwa anajiona kuwa yeye ni yeye na Hakuna kama yeye.
Hali hii ya kuzaliwa ya kujiona ndio inayopelekea Majivuno, Umimi pamoja na Hasira, Ukorofi na chuki
Kuweza kuushinda kabisa Utu na Ubinadamu wako hapo utakua umeweza kushinda Ile asili yako ya dhambi. Ukiweza kushinda ile asili yako ya dhambi ndio utakuwa umejiepusha na makosa haya.
Tunakosa Utii kwa Mungu tunaposhindwa kupambana na Majivuno, Umimi pamoja na Hasira, Ukorofi na chuki
Mungu ametupa Amri Kuu ya Upendo. Upendo kwake na kwa Binadamu. Lakini amri hii haiwezi kutimizwa kama hatutaweza kushinda kwanza Majivuno, Umimi, Hasira, Ukorofi na Chuki.
Mungu na Akubariki sana kwa Neema zake na akuwezeshe uweze kushinda dhambi na makosa yasiyoonekana kama dhambi, ambayo ndiyo yanayozuia Waumini na watumishi wa Mungu kuufikia Ukamilifu na Utakatifu.
Nicholas Wanjohi (Guest) on March 15, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
Lucy Mahiga (Guest) on November 8, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mary Kendi (Guest) on November 7, 2023
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Sarah Mbise (Guest) on November 2, 2023
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Joseph Kawawa (Guest) on October 21, 2023
Neema ya Mungu inatosha kwako
James Malima (Guest) on September 5, 2023
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Grace Wairimu (Guest) on April 11, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
Dorothy Mwakalindile (Guest) on March 20, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Richard Mulwa (Guest) on December 28, 2022
Mwamini katika mpango wake.
Joyce Nkya (Guest) on December 15, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
Rose Amukowa (Guest) on October 9, 2022
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Faith Kariuki (Guest) on October 1, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Ann Wambui (Guest) on September 10, 2022
Mungu akubariki!
Peter Mbise (Guest) on August 13, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Lucy Mahiga (Guest) on July 27, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Janet Sumaye (Guest) on July 8, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
David Nyerere (Guest) on June 12, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
Joseph Kiwanga (Guest) on June 11, 2022
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Margaret Anyango (Guest) on May 27, 2022
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Elizabeth Mrema (Guest) on May 19, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
David Nyerere (Guest) on May 7, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Rose Mwinuka (Guest) on March 14, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
Alice Wanjiru (Guest) on March 8, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Monica Nyalandu (Guest) on February 12, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
David Chacha (Guest) on January 11, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Catherine Mkumbo (Guest) on December 11, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Esther Cheruiyot (Guest) on November 21, 2021
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Diana Mallya (Guest) on November 13, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Stephen Kikwete (Guest) on November 6, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Paul Ndomba (Guest) on October 15, 2021
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Wilson Ombati (Guest) on October 2, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Joyce Aoko (Guest) on August 19, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Josephine Nduta (Guest) on August 9, 2021
Baraka kwako na familia yako.
Edwin Ndambuki (Guest) on July 29, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Carol Nyakio (Guest) on April 26, 2021
Katika imani, yote yanawezekana
Sarah Karani (Guest) on April 14, 2021
Dumu katika Bwana.
Sarah Karani (Guest) on April 13, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Victor Kimario (Guest) on April 1, 2021
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Mariam Kawawa (Guest) on March 27, 2021
Rehema zake hudumu milele
Victor Sokoine (Guest) on December 4, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Andrew Odhiambo (Guest) on November 30, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Agnes Njeri (Guest) on September 28, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
Rose Kiwanga (Guest) on August 18, 2020
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Lydia Mutheu (Guest) on August 11, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Jane Muthoni (Guest) on June 25, 2020
Nakuombea π
Anna Kibwana (Guest) on March 7, 2020
Rehema zake hudumu milele
Samson Mahiga (Guest) on December 14, 2019
Mwamini katika mpango wake.
Irene Akoth (Guest) on November 15, 2019
Dumu katika Bwana.
Grace Minja (Guest) on November 5, 2019
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Philip Nyaga (Guest) on November 4, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Kenneth Murithi (Guest) on October 18, 2019
Neema na amani iwe nawe.
Monica Nyalandu (Guest) on October 5, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mariam Kawawa (Guest) on August 6, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Lucy Kimotho (Guest) on July 12, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Emily Chepngeno (Guest) on June 21, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Miriam Mchome (Guest) on June 16, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
Hellen Nduta (Guest) on February 20, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
George Wanjala (Guest) on February 15, 2019
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Moses Mwita (Guest) on January 26, 2019
Rehema hushinda hukumu
George Ndungu (Guest) on January 22, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia