Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Mambo ya Msingi Unayopaswa kufahamu kuhusu Ekaristi Takatifu: Mwili na Damu Ya Bwana Wetu Yesu Kristu

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Ekaristi ni nini?

Ekaristi ni Sakramenti ya Mwili na Damu ya Yesu Kristo, katika
maumbo ya mkate na divai. Sakramenti hii
iliwekwa na Yesu Mwenyewe kwenye karamu ya mwisho, siku ya Alhamisi jioni kabla ya mateso
yake. (Yoh 6:1-71; Mt 26:26-28).

Maana ya jina Ekaristia

Tendo la shukrani na baraka.
Jina Ekaristi limetokana na neno la Kigiriki,
εύχαριστείν, maana yake ni “tendo la shukrani”,
“ kutoa shukrani*”, (Lk 22:19; 1Cor 11:24).
Ni tendo ambalo Yesu analifanya kwa Mungu.
Anamshukuru Mungu kwa kukamilisha kazi ya ukombozi. Tendo la baraka – εύλογείν
Kulingana na utamaduni wa Wayahudi baraka ilkua ikitolewa wakati wa mlo ikitukuza kazi za up mbaki za Mungu (Mt 26:26; Mk 14:22).

Injili zinazoongelea kuwekwa kwa Ekaristi

Injili tatu zinatueleza jinsi Yesu Kristo alivyoweka
Ekaristi Takatifu:
Mt 26:26-28.
Mk 14: 22-24
Lk 22:19-20
Mwinjili Yohane anaeleza Yesu Kristo mkate wa
uzima. Sura ya sita.
4. 1Kor 11:23-25
Mtume Paulo anatueleza jambo hilo katika Waraka wa kwanza kwa Wakorintho. 1Kor
11:23-25.

Tunajifunza kutoka kwa Yesu mambo yafuatayo

Lk 22:1. Saa ya Yesu (Lk 22:14). Hapa hamaanishi
saa ya kula, hapana. Bali saa ile ile ya kutimiliza tendo la wokovu. Yohane anapenda kusema saa ya kumtukuza Mungu, saa ya kupita kutoka ulimwengu huu kwenda kwa Baba. Sisi tunaweza kusema, tuna saa maalum ya kuingia katika ulimwengu wa
roho.Saa ya kukutana na Mungu, kutoka
ulimwengu huu kwenda kwa Mungu. (Sala au kifo).
2. Shukrani na masifu kwa Baba (Lk 22:17).
3. Kugawana sisi kwa sisi kikombe cha kwanza (Lk 22:17).
4. Kumbukumbu ya sadaka yake ya wokovu (Lk 22:19).
5. Uwepo wake (Lk 22:19).
6. Damu yake imemwagika kwa ajili yetu, kikombe cha pili (Lk 22:20).
Ekaristi ni Baraka kuu:
Yesu anabariki –kazi ya wokovu inabarikiwa na Yesu Mwenyewe. Hata vitu tunavyovitumia kila siku ni lazima kuviombea
baraka. Kabla ya mageuzo mkate na divai vinaombewa baraka (Mt 26:26).
Yesu anajitoa mwenyewe kwa watu –Yesu anajitoa kwa kila mshiriki (Mt 26:26).

Matunda ya Ekaristi katika maisha ya mkristo.

1. Muungano na Kristo:
Ekaristi inatuunganisha na Kristo kwa muungano wa ndani kabisa (Yoh 6:56).
2. Uzima wa milele : Ekaristi ni chanzo cha
uzima, maisha yetu yote yanapata uzima kwa kushiriki Mwili na damu ya Kristo, (Yoh 6:57).
3. Umoja: Ekaristi inaleta umoja wa kweli.
Tunafanywa kuwa mwili mmoja (1Kor 10:16-17).
4. Huondoa dhambi: Inatuondolea kwa
kuzifuta dhambi ndogo au inatutenga na dhambi ndogo (Mt 26:28; Yoh 1:29). Sakramenti ya
kitubio ndio hasa huondoa dhambi za mauti
(1Yoh 1:7; Yoh 20:22-23).
5. Dawa ya kutuponya kutoka katika umauti:
Ekaristi ni dawa ya kutokufa (Yoh 6:57-58).
6. Kufufuliwa siku ya mwisho: (Yoh 6:54).

Nguvu ya Ekaristi

–Kuponywa kwa
kuondolewa dhambi zetu.
Nguvu za Mungu zimo katika Ekaristi. Kabla ya kupokea Ekaristi tunasali Ee Bwana siesta hili uingie kwangu lakini sema neno tu na roho yangu
itapona. Bila shaka litakuwa kosa kubwa kwetu sisi kufikiri kwamba uponyaji unahusu masuala ya
mwili tu. Si kila uponyaji ni uponyaji wa mwili.
Mtume Paulo katika Waraka wa kwanza kwa Wathesalonike sura ya 5:23 kuwa sisi wanadamu tu mwili, roho na nafsi . Hivyo tunaweza kuponywa nafsi zetu na roho zetu. Hata kama uponyaji haujanja katika mwili.
Lakini mara nyingi ukitokea uponyaji wa ndani basi matokeo
yake utayaona hata kimwili. (anima sana in
corpore sano) (Roho yenye afya katika mwili
wenye afya)
1. Ekaristi Takatifu inayalinda maisha ya
kimanga ya roho tuliyoyapokea wakati wa Ubatizo
, kwa kupata anayekomunika nguvu za kimungu za kupambana na vishawishi, na
kudhoofisha nguvu za tamaa. Inaimarisha uhuru wa mapenzi ya nafsi zetu wa kuhimili
mashambulizi ya shetani.
2. Ekaristi Takatifu inaongeza maisha ya
neema ambayo tayari tunayo. Hufanya hivyo kwa kuhuisha fadhila na vipaji vya Roho Mtakatifu
tulivyonavyo.
3. Ekaristi Takatifu inayatibu magonjwa ya kiroho ya nafsi kwa kuziondoa dhambi ndogo na kumkinga mtu na adhabu ndogo ndogo za kidunia
zitokanazo na dhambi. Ondoleo la dhambi ndogo na mateso ya muda yasababishwayo na dhambi hizi hufanyika mara moja kwa sababu ya upendo
kamili kwa Mungu ambao huamshwa kwa
kuipokea Ekaristi. Ondoleo la dhambi hizi
hutegemea kiasi cha upendo unaoelekezwa
kwenye Ekaristi (Lk 7:47).
4. Ekaristi Takatifu inatupa furaha ya kiroho tunapomtumikia Kristo, tunapotetea njia yake,
tunapotekeleza majukumu yetu ya maisha, na kufanya sadaka zetu zinazotukabili zile ni katika kuiga maisha ya Mwokozi wetu.
The ListPages module does not work recursively.
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Samson Tibaijuka Guest Jun 1, 2024
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Sharon Kibiru Guest Jan 23, 2024
Baraka kwako na familia yako.
👥 Lucy Mushi Guest Dec 24, 2023
Endelea kuwa na imani!
👥 Monica Adhiambo Guest Aug 17, 2023
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Dorothy Nkya Guest May 22, 2023
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Edward Chepkoech Guest Jan 20, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Janet Mbithe Guest Aug 12, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Janet Sumaye Guest Aug 7, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Sarah Mbise Guest Jul 23, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Paul Kamau Guest Jun 26, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Jane Malecela Guest Jun 2, 2022
Rehema hushinda hukumu
👥 Margaret Mahiga Guest May 29, 2022
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 James Kawawa Guest May 27, 2022
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Edith Cherotich Guest Apr 25, 2022
Sifa kwa Bwana!
👥 Wilson Ombati Guest Apr 2, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
👥 James Kimani Guest Jan 23, 2022
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Fredrick Mutiso Guest Sep 17, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Stephen Kikwete Guest Dec 29, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Victor Malima Guest Sep 10, 2020
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Joyce Aoko Guest Aug 10, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Rose Waithera Guest Jul 7, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Patrick Akech Guest Apr 9, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Miriam Mchome Guest Feb 10, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Josephine Nduta Guest Feb 9, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Peter Mbise Guest Dec 13, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Joseph Kawawa Guest May 20, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 David Ochieng Guest Apr 3, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Sarah Karani Guest Mar 10, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Robert Ndunguru Guest Feb 20, 2019
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Richard Mulwa Guest Feb 2, 2019
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Brian Karanja Guest Oct 26, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Mary Kendi Guest Sep 26, 2018
Nakuombea 🙏
👥 Raphael Okoth Guest Jun 22, 2018
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Grace Minja Guest Jun 5, 2018
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Sharon Kibiru Guest Apr 16, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Mariam Hassan Guest Feb 12, 2018
Dumu katika Bwana.
👥 Elizabeth Mrema Guest Dec 23, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Chris Okello Guest Dec 16, 2017
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 John Kamande Guest Dec 12, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Samuel Were Guest Nov 20, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Grace Wairimu Guest Nov 2, 2017
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Michael Onyango Guest Sep 14, 2017
Neema na amani iwe nawe.
👥 Joseph Njoroge Guest Mar 25, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Joyce Aoko Guest Oct 19, 2016
Mwamini katika mpango wake.
👥 Christopher Oloo Guest Oct 13, 2016
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Miriam Mchome Guest Oct 11, 2016
Rehema zake hudumu milele
👥 Joseph Kawawa Guest Jun 4, 2016
Mungu akubariki!
👥 George Ndungu Guest May 15, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Elizabeth Malima Guest Apr 9, 2016
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Mary Sokoine Guest May 20, 2015
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About