
Zaburi ya Toba, Zaburi ya 51

Hii ndiyo Sala ya Toba
Zaburi 51
1 Ee Mungu, unirehemu,Sawasawa na fadhili zako.Kiasi cha wingi wa rehema zako,Uyafute makosa yangu.
2 Unioshe kabisa na uovu wangu,Unitakase dhambi zangu.
3 Maana nimejua mimi makosa yanguNa dhambi yangu i mbele yangu daima.
4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako,Na kufanya maovu mbele za macho yako.Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo,Na kuwa safi utoapo hukumu.
5 Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu;Mama yangu alinichukua mimba hatiani.
6 Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni;Nawe utanijulisha hekima kwa siri,
7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi,Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji
8 Unifanye kusikia furaha na shangwe,Mifupa uliyoiponda ifurahi.
9 Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu;Uzifute hatia zangu zote.
10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi,Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu
11 Usinitenge na uso wako,Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.
12 Unirudishie furaha ya wokovu wako;Unitegemeze kwa roho ya wepesi.
13 Nitawafundisha wakosaji njia zako,Na wenye dhambi watarejea kwako.
14 Ee MUNGU, Mungu wa wokovu wangu,Uniponye na damu za watu,Na ulimi wangu utaiimba haki yako.
15 Ee Bwana, uifumbue midomo yangu,Na kinywa changu kitazinena sifa zako.
16 Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
17 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika;Moyo uliovunjika na kupondeka,Ee Mungu, hutaudharau.
18 Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako,Uzijenge kuta za Yerusalemu.
19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki,Na sadaka za kuteketezwa, na kafara.Ndipo watakapotoa ng’ombeJuu ya madhabahu yako.
Comments
Please log in or register to leave a comment or reply.
Elizabeth Mrope (Guest) on May 26, 2024
Katika imani, yote yanawezekana
Edwin Ndambuki (Guest) on September 27, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Elizabeth Mrema (Guest) on June 27, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Lucy Mahiga (Guest) on May 26, 2023
Rehema zake hudumu milele
Charles Mrope (Guest) on April 10, 2023
Mwamini katika mpango wake.
Nicholas Wanjohi (Guest) on August 28, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
David Chacha (Guest) on March 7, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Henry Mollel (Guest) on December 29, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Elizabeth Mrope (Guest) on December 18, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Anna Mchome (Guest) on December 15, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Charles Mrope (Guest) on October 13, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Patrick Mutua (Guest) on July 28, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Rose Amukowa (Guest) on April 24, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
David Kawawa (Guest) on February 13, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Andrew Mahiga (Guest) on January 28, 2021
Rehema hushinda hukumu
Margaret Mahiga (Guest) on January 9, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Anthony Kariuki (Guest) on December 11, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Ann Awino (Guest) on October 7, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Charles Mrope (Guest) on October 2, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
Sarah Mbise (Guest) on September 30, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Joy Wacera (Guest) on September 29, 2020
Sifa kwa Bwana!
Peter Mwambui (Guest) on August 15, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
Linda Karimi (Guest) on July 31, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Betty Kimaro (Guest) on June 1, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Henry Sokoine (Guest) on April 30, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Andrew Odhiambo (Guest) on April 12, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Francis Mrope (Guest) on December 31, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
David Ochieng (Guest) on December 16, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Agnes Lowassa (Guest) on November 12, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
Lydia Wanyama (Guest) on October 11, 2019
Nakuombea 🙏
Ruth Kibona (Guest) on August 19, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
David Nyerere (Guest) on January 20, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Moses Kipkemboi (Guest) on January 19, 2019
Dumu katika Bwana.
Andrew Mchome (Guest) on October 20, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
Lucy Kimotho (Guest) on October 17, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Lucy Wangui (Guest) on August 22, 2018
Endelea kuwa na imani!
Lucy Mushi (Guest) on August 21, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Joyce Aoko (Guest) on July 24, 2018
Mungu akubariki!
Moses Mwita (Guest) on June 7, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Grace Wairimu (Guest) on March 11, 2018
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
George Wanjala (Guest) on December 28, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Esther Cheruiyot (Guest) on September 29, 2017
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Samuel Omondi (Guest) on May 23, 2017
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Simon Kiprono (Guest) on April 29, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
Stephen Amollo (Guest) on February 7, 2017
Baraka kwako na familia yako.
Mary Njeri (Guest) on January 4, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Daniel Obura (Guest) on April 27, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Peter Mbise (Guest) on March 22, 2016
Neema na amani iwe nawe.
Bernard Oduor (Guest) on March 18, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Mary Mrope (Guest) on October 25, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi