Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Zaburi ya Toba, Zaburi ya 51

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Hii ndiyo Sala ya Toba
Zaburi 51
1 Ee Mungu, unirehemu,Sawasawa na fadhili zako.Kiasi cha wingi wa rehema zako,Uyafute makosa yangu.
2 Unioshe kabisa na uovu wangu,Unitakase dhambi zangu.
3 Maana nimejua mimi makosa yanguNa dhambi yangu i mbele yangu daima.
4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako,Na kufanya maovu mbele za macho yako.Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo,Na kuwa safi utoapo hukumu.
5 Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu;Mama yangu alinichukua mimba hatiani.
6 Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni;Nawe utanijulisha hekima kwa siri,
7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi,Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji
8 Unifanye kusikia furaha na shangwe,Mifupa uliyoiponda ifurahi.
9 Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu;Uzifute hatia zangu zote.
10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi,Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu
11 Usinitenge na uso wako,Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.
12 Unirudishie furaha ya wokovu wako;Unitegemeze kwa roho ya wepesi.
13 Nitawafundisha wakosaji njia zako,Na wenye dhambi watarejea kwako.
14 Ee MUNGU, Mungu wa wokovu wangu,Uniponye na damu za watu,Na ulimi wangu utaiimba haki yako.
15 Ee Bwana, uifumbue midomo yangu,Na kinywa changu kitazinena sifa zako.
16 Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa,Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
17 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika;Moyo uliovunjika na kupondeka,Ee Mungu, hutaudharau.
18 Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako,Uzijenge kuta za Yerusalemu.
19 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki,Na sadaka za kuteketezwa, na kafara.Ndipo watakapotoa ng’ombeJuu ya madhabahu yako.
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest May 26, 2024
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Sep 27, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Elizabeth Mrema Guest Jun 27, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest May 26, 2023
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Apr 10, 2023
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Aug 28, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ David Chacha Guest Mar 7, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Dec 29, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Dec 18, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Dec 15, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Oct 13, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Jul 28, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest Apr 24, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ David Kawawa Guest Feb 13, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Andrew Mahiga Guest Jan 28, 2021
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Jan 9, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Dec 11, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Oct 7, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Oct 2, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Sarah Mbise Guest Sep 30, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Sep 29, 2020
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Peter Mwambui Guest Aug 15, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Jul 31, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Jun 1, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Apr 30, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest Apr 12, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Dec 31, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ David Ochieng Guest Dec 16, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Agnes Lowassa Guest Nov 12, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Oct 11, 2019
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Aug 19, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ David Nyerere Guest Jan 20, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Jan 19, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Oct 20, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Oct 17, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest Aug 22, 2018
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Aug 21, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Jul 24, 2018
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Moses Mwita Guest Jun 7, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Grace Wairimu Guest Mar 11, 2018
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ George Wanjala Guest Dec 28, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Sep 29, 2017
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest May 23, 2017
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest Apr 29, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Stephen Amollo Guest Feb 7, 2017
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Jan 4, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Apr 27, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Mar 22, 2016
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Mar 18, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Mary Mrope Guest Oct 25, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About