Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:34:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga - 2 Vikombe Sukari ya icing - 1 Kikombe Siagi - 250 gm Yai - 1 Vanilla - 2 Vijiko vya chai Baking powder -1 Kijiko cha chai Jam - ¼ kikombe Lozi - ¼ kikombe
JINSI YA KUPIKA
Koroga siagi na sukari katika mashine ya keki (cake mixer) mpaka iwe laini (creamy). Tia yai na vanilla koroga mpaka mchanganyiko uwe laini kama sufi. Tia unga na baking powder changanya na mwiko. Chota mchanganyiko kwa mkono (kiasi cha kijiko kimoja cha supufanya duara kisha weka kwenye treya ya kupikia. Bonyeza kila kiduara katikati kwa kidole, kisha weka jam na tupia lozi zilizomenywa na kukatwa katwa. Pika (bake) katika oven moto wa 375° F kama muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama
Mapishi ya Pilau Ya Nyama Ng'ombe Karoti Na Zabibu
Updated at: 2024-05-25 10:37:34 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo - Nyama
Nyama ng’ombe ya mifupa ilokatwa vipande - 1 kilo
Tangawizi na thomu (somu/garlic) ilosagwa - 2 vijiko vya supu
Bizari mchanganyiko/garama masala - 1 kijiko cha chai
Chumvi - Kiasi
Vipimo - Wali
Mchele - 4 glass
Mbatata/viazi menya katakata - 3 kubwa
Vitunguu katakata - 5
Kitunguu thomu kilosagwa (garlic/somu) - 1 kijiko cha supu
Hiliki ya unga - 1 kijiko cha chai
Bizari nzima ya pilau/cumin - 1 mti
Samli au mafuta - 2 Vijiko vya supu
Karoti zilokatwakatwa nyembamba - 6-7
Zabibu - Kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katika sufuria weka mafuta kijiko kimoja cha supu tia nyama na viungo vyake. kaushe katika moto hadi ikaribie kukauka kisha tia maji kiasi cha kuivisha na kubakisha supu ya mchele. Katika sufuria ya kupikia weka samli au mafuta ishike moto. Tia mbatata/viazi kaanga, tia vitunguu kaanga kidogo. Tia kitunguu thomu, hiliki, bizari ya pilau endelea kukaanga hadi viwe rangi ya brown kidogo. Tia mchele kaanga kidogo, kisha mimina nyama na supu yake. Funika wali uwive. Weka kikaangio katika moto, tia samli kijiko kimoja kisha tia karoti na zabibu, kaanga kwa sekunde chache tu kwa ajili ya kulainisha karoti na zabibu. Utakapopakuwa wali, pambia juu karoti na zabibu.
Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan
Updated at: 2024-05-25 10:23:16 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Nyama ya mbuzi au ng’ombe ya mafupa - 2 LB
Mchanganyiko wa dengu (hadesi, mchele, chooko, ngano, dengu n.k au nunua ya tayari iliyokwisha changanywa - 2 Vikombe
Kitungu maji (vikate vidogo) - 1
Mafuta - ¼ Kikombe
Nyana kata ndogo ndogo - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawazi iliyosagwa - 1 Kijiko cha supu
Bizari ya haliym - 2 vijiko vya supu
Nyanya ya kopo - 2 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha nyama na chumvi ½ kijiko mpaka iive, toa mafupa. Chemsha mchanganyiko wa dengu mpaka ziive. Katika sufuria weka mafuta, kaanga vitunguu vilainike, tia thomu na tangawizi, bizari ya haliym, nyanya ya kopo. Kaanga mpaka iwive. Tia nyama iliyowiva na supu yake kidogo. Tia mchanganyiko wa dengu tia kwenye mashine ya kusaga (blender), saga na ile supu ya nyama isagike vizuri Mimina kwenye sufuria changanya, tia ndimu kidogo, acha moto mdogo mdogo kwa muda wa dakika 15. Tia katika bakuli, pambia kwa vitunguu vilivyokaangwa vya rangi ya hudhurungi vikavu, pilipili mbichi (ukipenda) na kotmiri, ikiwa kuliwa.
Jinsi ya kupika Biriani ya Nyama Ng'ombe Na Mtindi
Updated at: 2024-05-25 10:37:39 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele wa biriani - 5 gilasi
Nyama ya ngombe ya mifupa - 1 ½ kilo na nusu
Vitunguu - 2 kilo
Tangawizi mbichi - ¼ kikombe
Thomu (saumu/garlic) - 3 vijiko vya supu
Mtindi - 2 vikombe
Nyanya ilokatwakatwa (chopped) - 3
Nyanya kopo - 1 kikombe
Masala ya biriani - 2 vijiko vya supu
Hiliki ya unga - 2 vijiko vya chai
Pilipili mbichi ilosagwa - 3 kiasi
Kotmiri ilokatwakatwa - 1 msongo (bunch)
Rangi ya biriani ya manjano - ½ kijiko cha chai
Zaafarani au zaafarani flavour - 1 kijiko cha supu
Mafuta ya kukaangia
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katakata vitunguu ukaangae katika mafuta mpaka vigeuke rangi ya brown ilokoza. Weka nyama iwe ilokatwakatwa katika treya au bakuli kubwa la oveni. Chaganya pamoja na tangawizi, thomu, nyanya, nyanya kopo, mtindi, masala ya biriani, chumvi, pilipili. Acha irowanike kwa muda wa masaa mawili takriban. Funika kwa karatasi ya jalbosi (foil paper) utie katika oveni upike muda wa dakika 45 takriban mpaka nyama iwive na huku unachanganya changanya sosi. Ikiwa ina maji ongezea nyanya kopo iwe nzito. Epua funua, kisha vuruga vitungu umwagie pamoja na kotmiri na umwagie mafuta ya moto kiasi. Ongezea kutia masala ya biriani na hiliki ya unga. Chemsha mchele nusu kiini, mwaga maji chuja, umwagie juu ya sosi ya nyama ukipenda kuchanganya au chemsha wali pekee. Nyunyizia rangi ya biriani pamoja na zaafarani flavour au zaafarani yenyewe ukipenda. Mimina mchele juu ya masala ya nyama, funika urudishe ndani ya oven upike muda wa kiasi ya dakika ishirini. Epua upake kwa kuchota wali kwanza kisha masala uwekee juu yake, kiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:34:43 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga ngano vikombc 3 Unga mbegu za mchicha kikombe 1 Baking powder vijiko vidogo Maziwa kikombe 1 Sukari kikombe 1 Blue band kikombe ½ Mayai 10-12
Hatua
• Chagua, osha, kausha mbegu za mchicha mweupe, kisha saga zilainike. • Chekecha unga wa ngano, unga wa mbegu za mchicha na baking powder Kwenye bakuli kubwa. • Ongeza sukari na changanya. • Ongeza mayai kidogo, kidogo ukikoroga na mwiko kwenda njia moja mpaka ilainike. • Kama rojo ni zito ongeza mayai, au maziwa ili iwe laini, ongeza vanilla na koroga. • Paka mafuta kwenye chombo cha kuoka au sufuria na chekechea unga kidogo. • Mimina rojo ya keki na oka kwenye oveni au kama ni sufuria funika, weka moto mwingi juu, chini weka moto kidogo. • Ukinusia harufu nzuri ya vanilla, funua, choma kisu katikati ya keki, kama ni kavu epua, pozesha na pakua kama kitafunio.
Updated at: 2024-05-25 10:23:10 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga - 6 vikombe
Samli - ½kikombe
Baking Powder - ½kijiko cha chai
Maziwa- 1 kikombe
Maji -Kisia kiasi kama unga bado mzito
VIAMBAUPISHI VYA SHIRA
Sukari - 5 vikombe
Maji - 2 1/2 vikombe
Vanilla - 2 vijiko vya chai
Rangi ya orange - 1 kijiko cha chai
Iliki ya unga - 1 Kijiko cha chai
MAANDALIZI
Changanya unga wa dengu, samli, baking powder pamoja na maziwa katika mashine ya keki (cake mixer). Ukisha changanya angalia kama mchanganyiko wako umekua mwepesi kidogo kuliko wa keki, kama bado mzito basi ongeza maji kiasi. Kisha weka mafuta kiasi kwenye karai,weka na samli kikombe kimoja, weka kwenye moto wa kiasi. Mafuta yakisha pata moto, chukua kijiko kikubwa cha matundu chota mchanganyiko wako na kijiko cha kawaida tia kwenye kijiko cha matundu. Hakikisha kijiko cha matundu kiwe juu ya karai ili mchanganyiko wako uchuruzike ndani ya mafuta yalio pata moto. Pika ndani ya mafuta mpaka iwive, ila usiache ikawa brown. Toa mchanganyiko ulowiva tia ndani ya shira uliyo pika. Hakikisha shira iwe imepoa kabla ya kutia mchanganyiko huo. Endelea kupika mchanganyiko wako mpaka uishe, kila ukitoa katika mafuta hakikisha unatia ndani ya shira. Ukishamaliza wote kanda huo mchanganyiko ulokua ndani ya shira mpaka uone shira yote imekauka (yaani iwe imeingia ndani ya mchanganyiko). Tupia zabibu kavu na lozi zilizo katwa, changanya na mkono. Wacha mchanganyiko katika bakuli, funika na foil mpaka siku ya pili. Siku ya pili chukua mchanganyiko kiasi katika mkono tengeneza mviringo (round).
MAANDALIZI YA SHIRA
Katika sufuria, tia sukari, maji, iliki, vanilla na rangi. weka kwenye moto wacha ichemke mpaka itowe povu (bubbles) juu. Kisha toa povu, wacha shira kwenye moto kama dakika 3. Hakikisha shira yako iwe inanata kiasi kwenye vidole, lakini iwe nyepesi kidogo kuliko shira ya kaimati.
Jinsi ya kupika Biskuti Nyembamba (Wafer Bar) Za Chokoleti Na Njugu
Updated at: 2024-05-25 10:23:08 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Wafer Powder/gram wafer (unga wa biskuti uliosagwa wa tayari) - vikombe 2
Maziwa ya Mgando Matamu ya Kopo - 2 vikombe
Nazi iliyokunwa - ½ Kikombe
Chokoleti vipande vipande - 1 Kikombe
Njugu vipande vipande - ½ Kikombe
Siagi - 227 g
MAPISHI
Yeyusha siagi motoni kisha changanya na unga wa wafer acha kidogo motoni Mimina katika treya unayochomea itandaze vizuri, kisha mimina maziwa juu yake pamoja na njugu vipande , nazi iliyokunwa na vipande vya chokoleti. Choma (bake) kwenye oveni kwa moto wa 350ºC kwa dakika 20. Katakata tayari kwa kuliwa
Jinsi ya kutengeneza Wali Wa Dengu Kwa Samaki Wa Kukaanga
Updated at: 2024-05-25 10:37:33 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele wa basmati - 3 Vikombe
Dengu - 2 vikombe
Viazi - 3 vikubwa
Kitunguu - 2 kubwa
Nyanya - 2
Pilipili mbichi kubwa - 3
Pilipilimanga - ½ kijiko cha chai
Garama Masala (bizari mchanganyiko) -1 kijiko cha chai
Supu ya vidonge (stock cubes) - 2 vidonge
Chumvi - kiasi
Mafuta - ¼ kikombe
Zaafarani - 1 kijiko cha chai
Samaki wa kukaanga
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Dengu kama sio za tayari kwenye kopo, roweka na zichemshe hadi ziwive
Maandalizi ya Masala Ya Dengu:
Zaafarani – iroweke katika maji ya dafu dafu (warm) ya chini ya robo kikombe weka kando. Osha mchele, roweka. Menya viazi na vitunguu, katakata vitunguu, na nyanya , weka kando. Katakata viazi vipande vidogo vidogo kwa umbo la mchemraba (cubes). Katika sufuria tia mafuta yakipata moto, tia viazi ukaange kidogo kwa moto mdogo mdogo hadi kukaribia kuwiva, toa weka kando. Kaanga vitunguu hadi vigeuka rangi ya hudhurungi isiyokoza (light brown) kisha tia nyanya ukaange kidogo. Tia vidonge vya supu (stock cubes) uvivuruge katika mchanganyiko, katakata pilipili mbichi kwa urefu tia, uendelee kukakaanga. Tia bizari, chumvi. Zima moto, changanya dengu na viazi katika mchanganyiko huo.
Mapishi ya Wali:
Chemsha mchele kama kawaida ya kupika wali mweupe, kiini kiwe kimewiva nusu yake. Chuja maji kisha changanya katika mchanganyiko wa dengu. Nyunyizia zaafarani, uchanganye wali na mchanganyiko kidogo tu. Funika acha uive katika mtoto mdogo mdogo au tia katika oveni hadi uive kama kawaida ya kupika wali. Pakua katiha sahani na tolea na samaki yoyote wa kukaanga.