Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_196aa780770fd8942fb487ab63a361b3, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/katoliki/sidebar.php on line 18

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/katoliki/sidebar.php on line 18

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_196aa780770fd8942fb487ab63a361b3, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/katoliki/right_sidebar.php on line 13

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/katoliki/right_sidebar.php on line 13
Sidebar with Floating Button
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_196aa780770fd8942fb487ab63a361b3, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/katoliki/top_menu.php on line 10

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/katoliki/top_menu.php on line 10
AckySHINE Katoliki
AckyShine
Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_196aa780770fd8942fb487ab63a361b3, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/katoliki/display_user.php on line 4

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/katoliki/display_user.php on line 4

Kisa cha mama na mwanae na mkwe wake

Featured Image

Kuna kijana mmoja daktari alikwenda kuposa. Binti aliyemposa akamuwekea masharti mazito. Akamwambia chagua mawili imma kunioa mimi au kukaa na mama yako, kwa sababu ukinioa mimi sitokubali mama yako aje hata harusini kwangu! Yule kijana aliemewa. Hakujua la kufanya. Mke anamtaka, lakini mama yake pia anampenda. Hivyo aliamua kuomba ushauri kwa mwalimu wake wa chuo kikuu. Alimwambia: moyo wangu unampenda mno binti niliyekwenda kumposa, lakini pia siwezi kuishi mbali na mama yangu. Nifanye nini?





Yule mwalimu mwenye hekima ambaye alikuwa anajua tabu alizopitia mama wa kijana yule, alimjibu kwa kumwambia: Kabla ya kukueleza uchague yupi kati ya wawili hao, rudi nyumbani, na leo usifanye chochote, ila kuikosha mikono ya mama yako. Yule kijana alifanya kama alivyotakiwa na mwalimu wake. Alipofika nyumbani aliomba idhini kwa mama yake amruhusu kuikosha mikono yake, na yule mama alimkubalia bila ya ajizi yoyote. Yule kijana alipoanza kuikosha mikono ya mama yake na kuona jinsi ilivyogugutaa kwa kazi za sulubu, alilia sana. Muda wote huu alikuwa hajawahi kuangalia viganja vya mama yake. *Je, na wewe umewahi kukaa na kuangalia viganja vya mama au baba yako kuona tabu walizopitia kukulea?* Kumbe baba wa yule kijana alifariki dunia yeye akiwa bado mdogo, yule mama aliamua kusamehe kila kitu kwa ajili ya mustakbali wa mwanawe. Alijitolea kufanya kazi za sulubu.





Alikubali kuwa mtumishi wa ndani, kukosha nguo, kupiga deki na kila kazi ambayo alihisi ingelimletea chumo la halali bila ya kujali ugumu wa jkazu hiyo. Juhudi zake zilizaa matunda na kufanikiwa kumlea na kumsomesha mwanawe hadi chuo kikuu na sasa ni daktari ambaye ana mustakbali mzuri. Baada ya yule kijana kukumbuka yote hayo, alifanya haraka kumpigia simu mwalimu wake huku macho yakiendelea kububujikwa na machozi akimwambia, siwezi kusubiri hadi kesho. Jibu nimeshalipata. Siwezi kumtupa mama yangu kwa ajili ya mtu asiyejua thamani ya mama. Ahsante sana kwa kunionesha njia sahihi! Kamwe siwezi kumuuza mama yangu kwa ajili ya leo yangu wakati yeye ameuza maisha yake yote kwa ajili ya mustakbali wangu.
NANI KAMA MAMA?!? Maa! Tabasamu lako ni ufunguo wangu wa ufanisi.
Kama umeipenda, itume kwa wengine ili nao wazinduke.


AckySHINE Solutions

Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_196aa780770fd8942fb487ab63a361b3, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/katoliki/comments.php on line 4

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/katoliki/comments.php on line 4

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Maina (Guest) on July 21, 2024

Hdithi Nzuri,

Adam (Guest) on July 21, 2024

Nimeipenda,

Paul (Guest) on July 21, 2024

Hadithi tamu,

Musa (Guest) on July 21, 2024

Asnte

Maina (Guest) on July 21, 2024

Hdithi Nzuri,

Adam (Guest) on July 21, 2024

Nimeipenda,

Adam (Guest) on July 21, 2024

Hadithi tamu,

Adam (Guest) on July 21, 2024

Asnte

Related Posts

Huruma ya mama kwa mwanae ilivyomtesa

Huruma ya mama kwa mwanae ilivyomtesa

Alikuwepo mama mmoja aliyekuwa chongo na mwanae alimchukia kwa sababu ya ku... Read More

Maisha magumu ya changamoto ya mke na mme

Maisha magumu ya changamoto ya mke na mme

Nilianza kujisikia vibaya hata kabla ya kufunga ndoa. Nakumbuka miezi mitat... Read More

Kisa cha baba mzee na mwanae

Kisa cha baba mzee na mwanae

Mtoto alifanya maamuzi ya kumpeleka baba yake ambaye alikuwa Mzee sana kwen... Read More

Stori inayogusa!!

Stori inayogusa!!

Habari ya mama aliyeuguliwa ghafla na mtoto wake majira ya SAA 2 usiku, mtot... Read More

Kisa kilichombadilisha mume tabia

Kisa kilichombadilisha mume tabia

Mume alirejea nyumbani na kukuta ujumbe juu ya meza umeandikwa "NIMEONDOKA"... Read More

Kisa cha kusisimua cha mama mjane

Kisa cha kusisimua cha mama mjane

Mimi ni mwanamke mjane ninaishi mjini Arusha. Huu ni ushuhuda wangu wa mais... Read More

Majuto ni mjukuu. Angalia kisa cha huyu dada

Majuto ni mjukuu. Angalia kisa cha huyu dada

Dada mmoja aliyejulikana kwa jina
la Angel, alikuwa anafanya
biashara... Read More


Warning: session_start(): open(/var/cpanel/php/sessions/ea-php81/sess_196aa780770fd8942fb487ab63a361b3, O_RDWR) failed: No such file or directory (2) in /home/ackyshine/katoliki/bottom_menu.php on line 3

Warning: session_start(): Failed to read session data: files (path: /var/cpanel/php/sessions/ea-php81) in /home/ackyshine/katoliki/bottom_menu.php on line 3
📘 About 🔒 Login 📝 Register 📞 Contact