Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

JE,SHERIA YA MAPADRE KUTOOA NA KUISHI USEJA IMEANDIKWA WAPI KATIKA BIBLIA AU IMETUNGWA TU NA PAPA?

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Pengine umewahi kuulizwa swali hili wakati fulani.Na jibu lake ni kama ifuayavyo:
Mtu anapouliza kila kitu kimeandikwa wapi katika Biblia ni kudhihirisha kutokuijua au kuielewa vizuri Biblia Takatifu na historia yake.Mtu anapong'ang'ania "nionyeshe kitu fulani kimeandikwa wapi kwenye Biblia"ni kutaka kujiona ya kwamba yeye anaielewa sana Biblia na ameisoma yote kwa hiyo kila kitu kilichopo kwenye Biblia anakifahamu kumbe haijui Biblia bali anakariri Biblia!
Na hili suala la kushupalia swala la kuoa linadhihirisha jinsi gani tulivyo kizazi cha zinaa,ni kama tunadhani kuwa UZIMA upo katika kujamiiana!La hasha.
Paulo anasema "Kwasababu ya zinaa ni bora kuoa na kuolewa"(1Wakorintho 7:2.9) haya sio maneno ya kufurahia na kuchekelea tu maana "YANAWALENGA WALE WALIOSHINDIKANA KATIKA YALE YAPENDEZAYO"(1Wakorintho 7:1.8)sasa ni lazima tujiulize je tumeshindikana kiasi hicho?,hiyo sio sifa!
1Wakorintho 7:1.8
"Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika,ni heri mwanaume asimguse mwanamke,8.Lakini nawaambia wale wasiooa bado na wajane heri wakae kama mimi nilivyo"
Na Paulo Mtume anasema "Ni bora kuoa au kuolewa" lakini hakusema "Ni LAZIMA kuoa au kuolewa"
Suala la kutooa kwa mapadre kadiri ya historia lilianza tangu zamani kabisa mwanzoni mwa milenia ya pili katika mtagusi wa pili wa Laterani mwaka wa 1139 ili waweze kumtumikia Mungu kwa uhuru na bila mawaa wala pasipo vikwazo(1wakorintho 7:32-35)
1wakorintho 7:32-35
"32Lakini nataka msiwe na masumbufu.Yeye asiyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya Bwana ampendezeje Bwana;33.bali yeye aliyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendeza mkewe.34-Tena iko tofauti kati ya mke na mwanamwali.Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana ili apate kuwa mtakatifu mwili na Roho.Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendezesha mumewe.,35.Nasema hayo niwafaidie ninyi,si kwamba niwategee tanzi,bali kwaajili ya vile vipendezavyo,tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine"
Maandiko hayo hapo juu yanajieleza wala sidhani kama yanahitaji kufafanuliwa zaidi ya yanavyojifafanua yenyewe.
Watu wengine wanafikiri kwamba kutooa ni dhambi,kama ni hivyo basi hata Yesu mwenyewe alikosa maana hata yeye mwenyewe hakuoa.
Yesu mwenyewe anafundisha kuhusu ubikira(Mathayo 19:10-12)
Mathayo 19:10-12,
"Wanafunzi wake wakamwambia,kama mambo ya mme na mke yakiwa hivyo ni afadhali kutuooa kabisa.Lakini Yeye akawaambia 'SI WOTE WAWEZAO KULIPOKEA NENO HILO,ILA TU WALE WALIOJALIWA,maana wako MATOWASHI waliozaliwa katika hali hiyo toka matumboni mwa mama zao;tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi,tena wako Matowashi WALIOJIFANYA WENYEWE KUWA MATOWASHI KWAAJILI YA UFALME WA MBINGUNI',awezaye kulipokea neno hili na alipokee"
Yesu mwenyewe analifafanua jambo hili kwa mapana,katika orodha ya matowashi Yesu aliowataja,Mapadre ni Matowashi waliojifanya hivyo kwaajili ya huduma ya kanisa na ufalme wa Mungu.
Tena Yesu anatuambia waziwazi kwamba"sio wote wawezao kulipokea neno hilo"yaani sasa sio wote wawezao kuwa Matowashi(Mapadre)bali ni wale tu waliojaliwa na Mungu neema hiyo.wale wasioweza kuishi upadre huoa na kuwa na familia.Tena Yesu anamalizia kwa kusema "Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee",kwa maana nyingine ni kusema "Fundisho au Utowashi huu sio wa lazima"anayeweza kuishi maisha hayo basi na ayapokee na yule asiyeweza basi aache!
Vilevile Mitume ili kumfuata Yesu kikamilifu waliyaacha yote waliokuwa nayo ikiwepo familia zao ili wamtumikie Bwana(Mathayo 19:27.29)
Mathayo 19:27.29:
"Ndipo Petro akajibu akamwambia 'Tazama sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe,tutapata nini basi?29.Amini nawaambia,kila mtu aliyeacha nyumba au ndugu wa kiume au wakike,au baba au mama au watoto au mashamba KWAAJILI YA JINA LANGU,atapokea mara mia zaidi na kuurithi uzima wa milele"
katika injili hiyo,Yesu anadhihirisha kwamba aliyeacha hayo yaliotajwa si kwasababu hawezi kuyapata la hasha,bali ameyaacha hayo yote KWAAJILI YA JINA LA YESU atapokea mengi hapa duniani halafu tena ataurithi ufalme wa mbinguni.
Mapadre wameyaacha hayo yote,wameacha nyumba,familia zao na kila kitu SIO KWASABABU HAWANA UWEZO AU HAWAWEZI KUPATA MAMBO HAYO bali WAMEACHA KWASABABU YA KUMTUMIKIA MUNGU KWA KADIRI YA MAANDIKO MATAKATIFU na kwakutaka kwao kuyaishi kimamilifu MASHAURI YA INJILI ikiwepo USEJA.
Maneno ya Paulo na yale ya Yesu mwenyewe kuhusu kumtumikia Mungu bila kuoa sio ya bahati mbaya bali ndiyo njia bora na inayofaa sana na kukubalika mbele ya Mungu.
Kwahiyo unapowaona mapadre hawaoi ujue sababu yake ni hiyo kwamba "Wamejitoa kwaajili ya kulihudumia kanisa"
(Na pia huwa nawashangaa mno watu wanaowapiga vita Mapadre kwamba kwanini hawaoi,najiuliza je,hao Mapadre wamewakataza wao kwamba wasioe?.)..na kama jibu ni hapana,sasa Je,"Pilipili ya shamba usiyoila inakuwashia nini?"
TUMSIFU YESU KRISTO!
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Jul 12, 2024
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest May 22, 2024
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Apr 25, 2024
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Monica Lissu Guest Jan 10, 2024
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Dec 19, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Agnes Njeri Guest Nov 20, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Kevin Maina Guest Aug 25, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Jun 8, 2023
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest May 10, 2023
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Apr 25, 2023
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest Mar 25, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Mar 10, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Mary Sokoine Guest Feb 2, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Jan 6, 2023
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Dec 31, 2022
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Alice Mwikali Guest Dec 7, 2022
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Nov 20, 2022
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Paul Ndomba Guest Jun 18, 2022
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest May 13, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Faith Kariuki Guest Apr 27, 2022
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Moses Mwita Guest Nov 10, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Catherine Mkumbo Guest Jun 26, 2021
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Jun 6, 2021
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Edward Lowassa Guest Jun 3, 2021
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest May 3, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Dec 13, 2020
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Oct 15, 2020
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Aug 18, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Jun 26, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Jan 31, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Aug 31, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Jun 10, 2019
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Betty Akinyi Guest Mar 24, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Mar 16, 2019
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Violet Mumo Guest Jan 11, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ James Kawawa Guest Dec 30, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest Aug 4, 2018
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Apr 18, 2018
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Jane Muthoni Guest Apr 18, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Francis Mtangi Guest Feb 25, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Dec 12, 2017
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Nov 30, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Edward Chepkoech Guest Oct 15, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Sep 14, 2016
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest May 11, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Mar 18, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Mar 17, 2016
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Mar 4, 2016
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest Jan 17, 2016
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Janet Mbithe Guest Apr 30, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About