Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Ufafanuzi wa Sala ya Baba yetu

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Baba Yetu uliye mbinguni,
jina lako litukuzwe;
ufalme wako ufike,
utakalo lifanyike
duniani kama mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku,
utusamehe makosa yetu,
kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea.
Usitutie katika kishawishi,
lakini utuopoe maovuni.
Amina

Ufafanuzi wake uliotumiwa na Fransisko wa Asizi

BABA YETUΒ mtakatifu kabisa: muumba, mkombozi, mfariji na mwokozi wetu.
ULIYE MBINGUNI:Β katika malaika na katika watakatifu, ukiwaangazia wawe na ufahamu, kwa sababu wewe Bwana ni mwanga; ukiwawasha wawe na upendo, kwa sababu wewe Bwana ni upendo; ukikaa ndani mwao na kuwajaza furaha, kwa sababu wewe Bwana ni wema mkuu kabisa, wema wa milele, ambaye kwako hutoka mema yote, na bila yako hakuna jema.
JINA LAKO LITUKUZWE:Β ujuzi wetu juu yako uwe wazi zaidi na zaidi, tuweze kujua upana wa baraka zako, urefu wa ahadi zako, kimo cha ukuu wako, kina cha hukumu zako.
UFALME WAKO UFIKE:Β utawale ndani yetu kwa njia ya neema yako na kutuwezesha kuingia katika ufalme wako ambapo unaonekana kama ulivyo, unapendwa kikamilifu, unatia heri ya kukaa nawe, unatia raha ya kukufurahia milele.
UTAKALO LIFANYIKE DUNIANI KAMA MBINGUNI:Β tuweze kukupenda kwa moyo wetu wote, kwa kukuwaza wewe daima; kwa roho yetu yote, kwa kukutamani wewe daima; kwa akili yetu yote, kwa kuelekeza nia zetu zote kwako na kwa kutafuta utukufu wako katika yote; kwa nguvu zetu zote pia, kwa kutumia uwezo na hisia zote za roho na mwili katika kuhudumia upendo wako na si chochote kingine; na tuweze kuwapenda majirani wetu kama tunavyojipenda, kwa kuwavuta wote kwa nguvu zetu zote kwenye upendo wako, tukifurahia mema ya wengine kama tunavyofurahia ya kwetu, na tukihuzunika pamoja na wengine kwa mabaya yanayowafikia, bila ya kumuudhi yeyote.
MKATE WETU WA KILA SIKU:Β Mwanao mpendwa Bwana wetu Yesu Kristo.
UTUPE LEO:Β kwa ukumbusho, ufahamu na heshima ya upendo ule aliokuwanao kwetu sisi na ya mambo yale ambayo alisema na kutenda na kuteseka kwa ajili yetu.
UTUSAMEHE MAKOSA YETU:Β kwa huruma yako isiyosemeka, kwa nguvu ya mateso ya Mwanao mpendwa, pamoja na stahili na maombezi ya Bikira mbarikiwa daima na ya wateule wako wote.
KAMA TUNAVYOWASAMEHE NA SISI WALIOTUKOSEA:Β na lolote tusilosamehe kikamilifu, wewe Bwana utuwezeshe kulisamehe kabisa, tuwapende kweli maadui wetu kwa ajili yako, na tuwaombee kwa bidii mbele zako, bila ya kumlipa yeyote ovu kwa ovu, bali tukijitahidi kumsaidia kila mmoja katika wewe.
NA USITUTIE KATIKA VISHAWISHI: kilichofichika au cha wazi, cha ghafla au cha muda mrefu.
LAKINI UTUOPOE MAOVUNI: yaliyopita, ya sasa na yajayo.
ATUKUZWE BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU KAMA MWANZO, NA SASA NA MILELE.Β AMINA.
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest Mar 13, 2024
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Feb 9, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Grace Minja Guest Jan 6, 2024
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ John Mushi Guest Dec 10, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Sep 25, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest May 15, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ George Mallya Guest Mar 26, 2023
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ James Kimani Guest Mar 20, 2023
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Jan 17, 2023
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Jan 12, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Jan 2, 2023
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Betty Akinyi Guest Dec 1, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest Nov 22, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Jul 23, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Jul 22, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Apr 10, 2022
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Mar 4, 2022
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Lydia Mahiga Guest Dec 25, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Edward Chepkoech Guest Nov 12, 2021
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Sep 16, 2021
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Jun 26, 2021
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Jun 22, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Jan 26, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Philip Nyaga Guest Jan 19, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Nov 4, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Oct 19, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Aug 28, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ George Tenga Guest Jul 20, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Jun 12, 2020
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Apr 29, 2020
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Mar 14, 2020
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Victor Mwalimu Guest Nov 27, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Nov 25, 2019
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Oct 21, 2019
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Anna Mahiga Guest Oct 11, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ David Sokoine Guest Jun 20, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Emily Chepngeno Guest Mar 9, 2019
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Faith Kariuki Guest Sep 7, 2018
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Michael Mboya Guest Aug 7, 2018
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Peter Otieno Guest May 27, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Apr 7, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Thomas Mtaki Guest Jan 1, 2018
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Sep 9, 2017
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Jul 23, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest May 17, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest May 4, 2017
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Feb 28, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Mary Sokoine Guest Oct 9, 2016
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Sep 22, 2015
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Andrew Mahiga Guest Sep 12, 2015
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About