Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Unganisha imani na maisha yako kupitia 🙏 Sala, 📜 Masomo ya Misa, 📖 Mafundisho, 💡 Tafakari, 📰 Makala, na 🔐 My System kwa usimamizi wa maisha binafsi. Tunakukaribisha kwenye safari ya kiroho na kimwili!.
Updated at: 2024-05-25 17:07:36 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
SWALI: Nini maana ya matatizo..?
JIBU: matatizo ni pale unapopewa adhabu na mwanajeshi then akakuruhusu uondoke, lakini ukarukia pikipiki yako halafu ukapayuka..!!!!! Mwanajeshi, wee boya Tu
Updated at: 2024-05-25 18:10:15 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kakubaliana vizuri na msichana fulani hivi kuwa aibuke gheto, mchizi kajipanga vizuri kabisa…. mara saa nne hivi mdada kasema hana nauli. Mshkaji kajikunja kamtumia Elfu tano maana mwenye shida alikuwa ni yeye…… Baada ya nusu saa yule dada akamtumia meseji. "Jamani mpenzi, kumbe baba hatoki nilijua atatoka… sorry bae sitaweza kuja kwa leo… sooo sorry!" Mshkaji jiii! hajajibu kitu…..
Baada ya muda kidogo meseji ikaingia katika simu ya binti, akajua mchizi kajibu. Mh! kutazama ni meseji kutoka Mpesa.
"CA90F0511 IMETHIBITISHWA Tshs 5000 ILIYOTUMWA KIMAKOSA KATIKA ACCOUNT YAKO IMETOLEWA SALIO LAKO NI Tshs 5"
Halafu ndo ikaingia meseji ya mshkaji. "BASI POA SIKU NYINGINE KAMA VIPI"
#dada wa watu mashavu yakamshuka… hakuamini kilichotokea…. yaani jamaa keshawapigia Voda na pesa fasta imezuiliwa……
MZEE:"sasa huyu mgeni sijui alale wap?"
MKE:"saa hizi ni usiku akalale na Bebi."
jamaa akaona huyo Bebi pengne mtoto anakojoa kitandani au akalia asije msumbua usiku
Updated at: 2024-05-25 18:02:06 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
MZEE:"sasa huyu mgeni sijui alale wap?"
MKE:"saa hizi ni usiku akalale na Bebi."
jamaa akaona huyo Bebi pengne mtoto anakojoa kitandani au akalia asije msumbua usiku
JAMAA:"msipate tabu mi ntalala hapa kwenye kochi" akalala
asubh wanakunywa chai akaibuka mrembo,jamaa akapigwa bumbuwazi almanusra ajimwagie chai.
BINTI:"Naitwa BEBI,we unaitwa nani?"
Jamaa akasema mimi naitwa Fara…..!
Updated at: 2024-05-25 17:13:21 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
UNATOKA SEBULENI UNAENDA ZAKO CHOONI UNAINGIA TU HIVI GHAFLA UNAKUTANA NA MZIGO MKUBWA WA MAVI JUU YA CHOO ALAFU UNAAMUA KURUDI ZAKO ILE UNATOKA TU UNAMUONA DEMU MZURI ULIYEMTONGOZA JANA ANAKUJA KUINGIA CHOO ULICHOTOKA WW NA KINA MZIGO WA MAVI JUU NA AMEKUONA WW NDIO UMETOKA MLE NDANI ..unaamua kurudi ili uka flash bahat mby maji hakuna.!!!
😁😁😁HAPO NDIO UTAJUA KWANINI SIKU HIZI HATUPENDI UJINGA😆😆😆😆
Huyu bwana leo kapatikana, Jamani nyodo nyingine mbaya
Baada ya kumaliza Degree yake ya sheria Bwana Rwegashora aliamua kurudi nyumbani Bukoba mjini na kufungua ofisi yake kwa ajili ya huduma kwa wateja.
Siku moja akiwa ndani ya ofisi yake alimuona mtanashati na mdada mmoja mrembo anakuja ofisini kwake akajua ni mteja anamletea kesi.
Ndipo akanyanyua mkoni wa wa simu ya TTCL na kuanza kuongea huku anajizunguusha kwenye kiti cha kuzunguuka.
Updated at: 2023-04-29 22:52:17 (1 year ago by Melkisedeck Leon Shine)
Baada ya kumaliza Degree yake ya sheria Bwana Rwegashora aliamua kurudi nyumbani Bukoba mjini na kufungua ofisi yake kwa ajili ya huduma kwa wateja. Siku moja akiwa ndani ya ofisi yake alimuona mtanashati na mdada mmoja mrembo anakuja ofisini kwake akajua ni mteja anamletea kesi.
Ndipo akanyanyua mkoni wa wa simu ya TTCL na kuanza kuongea huku anajizunguusha kwenye kiti cha kuzunguuka. Wakati mdada alipokaribia Rwegashora alimkaribisha kwa ishara maana alijifanya yupo busy na kuongea na simu ya umuhimu. Wakati anaongea na simu akisikika akisema No, No, No….. Absolutely No. Wajuulishe hao lay person wa New York kua siwezi kushuhulika na kesi ambayo itanilipa chini ya 50 million. Mimi ni profesional lawyer and im crossing the border to sarve international community.
Aka pose kidogo na akanywa maji kisha akaendelea….. Naweza kuanza kukusanya primary evidence next weak but tell them watume kwanza ten million kwa kuanza… Hahahahaha you dont know my Account Mr Roger. Ok waambie watume kwenye Account ileile walionitumia million 100 last month…
Aka pose tena akameza fundo la maji na kurekebisha tai yake kisha akaendelea… Ok usisahau kumueleza muendesha mashtaka mkuu wa marekani kua nitakuja New York mwezi ujao maana nitapita kwanza Amsterdam kuwasilisha utetezi wa yule mteja wangu mholanzi kisha nitaenda Tokyo kulipia ile gari yangu niloagiza.
Wakati anaongea hayo yote yule mdada alikua ametulia na anamuangalia Bwana Rwegashora anavyojizunguusha kwenye kiti chake huku akiongea kwa tambo kwenye ile simu ya TTCL. Baada ya kumaliza kuongea na simu Bwana Rwegashora aliweka mkono wa simu yake ya TTCL chini kisha akamgeukia mdada mrembo.
Samahan sana kwa kukupotezea muda wako unajua tena kazi zetu zinaumiza kichwa sana kama unavyoona mwenyewe yaani niko busy sana ninapokea simu sana mpaka nimechoka na simu nyingi ni za wateja wa njee ya nchi.
Anyway nikusaidie nn? Mdada akajibu mimi ni mfanyakazi wa kampuni ya TTCL nimekuja kuunganisha line yako ya simu kwani haipo hewani tangu wiki iliyopita…!!!
Namna wazazi wanavyoongea na mabinti katika umri tofauti
Updated at: 2024-05-25 17:57:54 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Miaka 13: Usipende wavulana ni wabaya. Miaka 18: Sitaki nikuone na yule mvulana tena! Miaka 23: Lini utatuletea mchumba wako? Miaka 26: Wenzio wanaolewa. Miaka 30: Tumekuambia kwamba acha kuchagua sana wanaume, hutaki kusikia! Miaka 33: Kuna mtu wa Mungu yupo kule anaombea unaweza kupata mchumba Miaka 36: At least pata mtoto mmoja. Miaka 39: We will take care of all the wedding bills…yeyote ni sawa sisi tutagharamia kila kitu mwanetu wee mlete tu . Miaka 45: hivi kweli nani alikuroga.?
MLEVI; "Nakunywa bia tano! MCHUNGAJI; "Bia moja bei gani!? MLEVU; "2500/ MCHUNGAJI; "Ulianza lini kunywa bia!? MLEVI; "Miaka 18 iliyopita!
MCHUNGAJI; "Kwa hiyo kwa siku unatumia zaidi ya 10,000?? MLEVI; "Ndio! MCHUNGAJI; "Kama u gekuwa unatunza hiyo pesa 10,000 kwa siku leo hii si ungekuwa na Range Rover!? MLEVI; "Samahani, naweza kukuuliza swali!? MCHUNGAJI; "Uliza! MLEVI; "Unakunywa bia!? MCHUNGAJI; "Hapana! MLEVI; "Nionyeshe Range Rover yako! MCHUNGAJI; "akasepa"