Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Vile unavyoweza kuwa DARAJA au KIKWAZO kwa wengine

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Kwa namna unayoishi unaweza ukawa daraja au kikwazo cha wengine kuishi maisha ya Amani raha na fanaka.
Unaweza ukawa daraja kwa maana kwamba wewe unaweza kuwa sababu ya wengine kupata Baraka na neema za Mungu.
Unaweza kuwa kikwazo kwa maana kwamba unaweza kuwa wewe ni sababu ya wengine kutokupata Baraka na Neema za Mungu.

Kwa jinsi unavyoishi unaweza ukawa chanzo cha Baraka kwa wengine au chanzo cha matatizo na vikwazo kwa wengine.

Vile unavyoweza kuwa Daraja kwa Wengine

Unaweza kuwa daraja au njia ya wengine kupata neema na Baraka katika maisha yao kulingana na matendo yako mema na Ibada yako kwa Mungu.

Kwa ucha Mungu wako, watu wako unaowapenda sana wanaweza kubarikiwa na kupata neema za Mungu Pamoja na wewe. Wale watu unaochangamana nao watabarikiwa kwa sababu na wewe umebarikiwa.
Kwa mfano wewe kama ni mzazi mcha Mungu unaweza ukawa chanzo cha Baraka na neema kwa watoto wako na kwa mwenzi wako wa ndoa. Vivyo hivyo na kwa watoto, mtoto anaweza kuwa chanzo cha Baraka kwa wazazi wake.

Inawezekana kuna Amani katika familia yako kwa sababu tuu wewe ni miongoni mwa wanafamilia hiyo na hivyo Mungu ameachilia Amani katika familia yako kwa sababu tuu wewe upo pale na wewe ni mcha Mungu.

Unaweza kuona sasa wewe ni chanzo cha Baraka kwa wale watu wako wa karibu. Kwa sababu tuu wewe ni mcha Mungu, na wao wanabarikiwa pamoja na wewe. Mungu anapobariki familia yako na wao pia wanabarikiwa.

Kwa hiyo basi, unapolegalega katika ucha Mungu wako unaweza pia kusababisha kulegalega au kikwazo cha Baraka za wengine.

Vile unavyoweza kuwa Kikwazo kwa Wengine

Unaweza kuwa kikwazo au kizuizi cha wengine kupata neema na Baraka katika maisha yao kulingana na matendo yako mabaya na kukosa kwako kumcha Mungu.

Kwa kuacha kumcha Mungu, watu wako unaowapenda sana wanaweza kukosa kubarikiwa na kukosa neema za Mungu kwa sababu wewe unazuia Baraka hizo. Wale watu unaochangamana nao watakosa Baraka kwa sababu umeandikiwa kutokubarikiwa na wanachanganyikana na asiyestahili kubarikiwa.

Kwa mfano wewe kama ni mzazi asiyemcha Mungu unaweza ukasababisha watoto wako wakashindwa kubarikiwa kwa sababu tuu kwa udhambi wako unazuia Baraka kwa familia yako yote wakiwemo watoto wako. Vivyo hivyo na wazazi wanaweza wakashindwa kubarikiwa kwa sababu watoto wao wanawazuilia Baraka zao.

Inawezekana hakuna Amani katika familia yako kwa sababu tuu wewe ni miongoni mwa wanafamilia hiyo. Kunakosekana Amani katika familia yako kwa sababu tuu wewe upo pale na wewe ni mdhambi/ mtu asiyemcha Mungu.

Unaweza kuona sasa wewe ni chanzo cha kukosekana Baraka kwa wale watu wako wa karibu. Kwa sababu tuu wewe ni mtu asiye mcha Mungu, na wao wanazuiliwa baraka pamoja na wewe. Mungu anapoacha kuibariki familia yako na wao pia wanakosa baraka. Kwa mfano unapokosa Amani na Mafanikio ukae ukijua kuwa wale unaowapenda na wanaokutegemea nao watakosa Amani na hawatanufaika kwa sababu hauna mafanikio.

Mwisho

Wewe ni kama Kiungo cha myororo wa Baraka au laana kwa wale uwapendao hasa familia yako. Ukibarikiwa unabarikiwa pamoja nao, ukilaaniwa unalaaniwa pamoja nao.

Kwa sababu hiyo, mara zote chagua kuishi kwa kumcha Mungu kwa sababu huwezi jua ni wangapi walioko nyuma yako na wanaobarikiwa kwa sababu ya ucha Mungu wako.

Mche Mungu kwa juhudi zote kwa sababu hujui ni wangapi wanaonufaika na ucha Mungu wako. Vilevile jitahidi usiwe mdhambi sana kwa sababu huwezi kujua ni wangapi wanaokosa Baraka za Mungu kwa udhambi wako.

Kumcha Mungu kuna faida kwako na kwa wengine, hasa unaowapenda. Kuto kumcha Mungu ni hasara kwako na kwa wale unaowapenda hasa familia yako

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 101

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Sep 14, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Victor Kamau Guest Aug 5, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Aug 2, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest Jul 22, 2019
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Apr 29, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Kevin Maina Guest Apr 2, 2019
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ James Mduma Guest Mar 10, 2019
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest Dec 1, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest Nov 6, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Nov 3, 2018
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Sep 13, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Aug 11, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Jul 15, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Jul 1, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest May 2, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Mar 16, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Feb 24, 2018
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Jan 31, 2018
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Jane Malecela Guest Jan 16, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest Dec 22, 2017
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Dec 13, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Jun 24, 2017
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Jun 20, 2017
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Apr 23, 2017
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ James Kawawa Guest Apr 14, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Jan 11, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Dec 24, 2016
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest Dec 19, 2016
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Nov 7, 2016
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Ann Wambui Guest Oct 12, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Aug 18, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Jun 10, 2016
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Feb 11, 2016
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Alice Mwikali Guest Feb 10, 2016
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Emily Chepngeno Guest Dec 7, 2015
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Sep 1, 2015
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Aug 29, 2015
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Jul 24, 2015
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Jul 12, 2015
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest May 12, 2015
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest May 8, 2015
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About