SOMO 1
Isa. 65:17-21
Β
Bwana asema: Tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni. Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.
Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza. Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa. Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake.
Β
Neno la Bwana⦠Tumshukuru Mungu.
Β
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 30:1, 3-5, 10-12 (K) 1
Β
(K) Nitakutukuza, ee Bwana, kwa maana umeniinua.
Β
Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua,
Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
Umeniinua nafsi yangu,
Ee Bwana, kutoka kuzimu.
Umenihuisha na kunitoa
Miongoni mwao washukao shimoni. (K)
Β
Mwimbieni Bwana zaburi,
Enyi watauwa wake.
Na kufanya shukrani.
Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.
Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo,
Katika radhi yake mna uhai.
Huenda kilio huja kukaa usiku,
Lakini asubuhi huwa furaha. (K)
Β
Ee Bwana, usikie, unirehemu,
Bwana, uwe msaidizi wangu.
Uligeuza matanga yangu kuwa machezo;
Ulinivua gunia, ukanivika furaha.
Ee Bwana, mungu wangu,
Nitakushukuru milele. (K)
Β
SHANGILIO
Eze. 33:11
Β
Sikufurahii kufa kwake mtu mwovu, asema Bwana, bali aiache njia yake mbaya, akaishi.
Β
INJILI
Yn. 4:43-54
Β
Baada ya siku mbili hizo Yesu aliondoka huko, akaenda Galilaya. Kwa maana Yesu mwenyewe alishuhudia ya kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe. Basi alipofika Galilaya, Wagalilaya walimpokea; kwa kuwa wameyaona mambo yote aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu; maana hao nao waliiendea sikukuu.
Basi alifika tena Kana ya Galilaya, hapo alipoyafanya yale maji kuwa divai. Na palikuwa na diwani mmoja ambaye mwanawe hawezi huko Kapernaumu. Huyo aliposikia ya kwamba Yesu amekuja kutoka Uyahudi mpaka Galilaya, alimwendea, akamsihi ashuke na kumponya mwanawe; kwa maana alikuwa kufani. Basi Yesu akamwambia, Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa? Yule diwani akamwambia, Bwana, ushuke asijakufa mtoto wangu. Yesu akamwambia, Enenda; mwanao yu hai. Mtu yule akalisadiki lile neno aliloambiwa na Yesu, naye akashika njia. Hata alipokuwa akishuka, watumwa wake walimlaki, wakisema ya kwamba mtoto wake yu hai. Basi akawauliza habari ya saa alipoanza kuwa hajambo; nao wakamwambia, jana, saa saba, homa ilimwacha. Basi babaye akafahamu ya kuwa ni saa ile ile alipoambiwa na Yesu, Mwanao yu hai. Akaamini yeye na wote wa nyumbani mwake.
Hiyo ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu, alipokuwa ametoka Uyahudi kufika Galilaya.
Β
Neno la Bwana⦠Sifa kwako Ee Kristo.
Edward Chepkoech (Guest) on May 23, 2024
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Janet Mwikali (Guest) on April 18, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Betty Akinyi (Guest) on October 8, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
David Kawawa (Guest) on September 9, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Mary Mrope (Guest) on June 5, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Francis Mrope (Guest) on May 17, 2023
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Grace Njuguna (Guest) on May 8, 2023
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Lucy Mushi (Guest) on November 30, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
Benjamin Masanja (Guest) on August 3, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Diana Mallya (Guest) on July 18, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
David Chacha (Guest) on May 10, 2022
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Charles Wafula (Guest) on March 17, 2022
Mungu akubariki!
Simon Kiprono (Guest) on March 6, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
David Kawawa (Guest) on March 6, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Richard Mulwa (Guest) on February 16, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rose Kiwanga (Guest) on August 26, 2021
Nakuombea π
Lydia Wanyama (Guest) on October 27, 2020
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Sharon Kibiru (Guest) on June 24, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
Kenneth Murithi (Guest) on June 7, 2020
Rehema zake hudumu milele
Jane Malecela (Guest) on May 9, 2020
Baraka kwako na familia yako.
Edwin Ndambuki (Guest) on January 31, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Charles Mrope (Guest) on October 26, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Faith Kariuki (Guest) on August 31, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Nora Kidata (Guest) on March 13, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Isaac Kiptoo (Guest) on February 9, 2019
Endelea kuwa na imani!
Lydia Wanyama (Guest) on November 13, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
Stephen Amollo (Guest) on October 5, 2018
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Kenneth Murithi (Guest) on August 28, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
James Kimani (Guest) on August 10, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Andrew Mchome (Guest) on July 15, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
John Mushi (Guest) on June 27, 2018
Mwamini Bwana; anajua njia
Alice Jebet (Guest) on April 16, 2018
Mwamini katika mpango wake.
David Sokoine (Guest) on March 9, 2018
Dumu katika Bwana.
James Kawawa (Guest) on February 11, 2018
Rehema hushinda hukumu
David Nyerere (Guest) on January 4, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Raphael Okoth (Guest) on December 26, 2017
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Alex Nyamweya (Guest) on October 12, 2017
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
George Tenga (Guest) on June 6, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Jacob Kiplangat (Guest) on May 18, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Mary Njeri (Guest) on April 17, 2017
Neema na amani iwe nawe.
Josephine Nekesa (Guest) on January 1, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Charles Mchome (Guest) on May 29, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Paul Ndomba (Guest) on April 11, 2016
Neema ya Mungu inatosha kwako
Jacob Kiplangat (Guest) on February 17, 2016
Sifa kwa Bwana!
Joyce Mussa (Guest) on December 31, 2015
Nguvu hutoka kwa Bwana
Paul Kamau (Guest) on December 1, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Ann Awino (Guest) on November 6, 2015
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Stephen Kangethe (Guest) on September 30, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Alex Nyamweya (Guest) on September 15, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Joy Wacera (Guest) on June 16, 2015
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe