Sidebar with Floating Button
AckySHINE Katoliki
☰
AckyShine

MASOMO YA MISA, MACHI 28, 2022: JUMATATU: JUMA LA 4 LA KWARESIMA

Featured Image

SOMO 1

Isa. 65:17-21

Β 

Bwana asema: Tazama, mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya, na mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni. Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha.

Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza. Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa. Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake.

Β 

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

Β 

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 30:1, 3-5, 10-12 (K) 1

Β 

(K) Nitakutukuza, ee Bwana, kwa maana umeniinua.

Β 

Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua,

Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.

Umeniinua nafsi yangu,

Ee Bwana, kutoka kuzimu.

Umenihuisha na kunitoa

Miongoni mwao washukao shimoni. (K)

Β 

Mwimbieni Bwana zaburi,

Enyi watauwa wake.

Na kufanya shukrani.

Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.

Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo,

Katika radhi yake mna uhai.

Huenda kilio huja kukaa usiku,

Lakini asubuhi huwa furaha. (K)

Β 

Ee Bwana, usikie, unirehemu,

Bwana, uwe msaidizi wangu.

Uligeuza matanga yangu kuwa machezo;

Ulinivua gunia, ukanivika furaha.

Ee Bwana, mungu wangu,

Nitakushukuru milele. (K)

Β 

SHANGILIO

Eze. 33:11

Β 

Sikufurahii kufa kwake mtu mwovu, asema Bwana, bali aiache njia yake mbaya, akaishi.

Β 

INJILI

Yn. 4:43-54

Β 

Baada ya siku mbili hizo Yesu aliondoka huko, akaenda Galilaya. Kwa maana Yesu mwenyewe alishuhudia ya kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe. Basi alipofika Galilaya, Wagalilaya walimpokea; kwa kuwa wameyaona mambo yote aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu; maana hao nao waliiendea sikukuu.

Basi alifika tena Kana ya Galilaya, hapo alipoyafanya yale maji kuwa divai. Na palikuwa na diwani mmoja ambaye mwanawe hawezi huko Kapernaumu. Huyo aliposikia ya kwamba Yesu amekuja kutoka Uyahudi mpaka Galilaya, alimwendea, akamsihi ashuke na kumponya mwanawe; kwa maana alikuwa kufani. Basi Yesu akamwambia, Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa? Yule diwani akamwambia, Bwana, ushuke asijakufa mtoto wangu. Yesu akamwambia, Enenda; mwanao yu hai. Mtu yule akalisadiki lile neno aliloambiwa na Yesu, naye akashika njia. Hata alipokuwa akishuka, watumwa wake walimlaki, wakisema ya kwamba mtoto wake yu hai. Basi akawauliza habari ya saa alipoanza kuwa hajambo; nao wakamwambia, jana, saa saba, homa ilimwacha. Basi babaye akafahamu ya kuwa ni saa ile ile alipoambiwa na Yesu, Mwanao yu hai. Akaamini yeye na wote wa nyumbani mwake.

Hiyo ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu, alipokuwa ametoka Uyahudi kufika Galilaya.

Β 

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Edward Chepkoech (Guest) on May 23, 2024

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Janet Mwikali (Guest) on April 18, 2024

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Betty Akinyi (Guest) on October 8, 2023

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

David Kawawa (Guest) on September 9, 2023

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Mary Mrope (Guest) on June 5, 2023

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Francis Mrope (Guest) on May 17, 2023

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Grace Njuguna (Guest) on May 8, 2023

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Lucy Mushi (Guest) on November 30, 2022

Mungu ni mwema, wakati wote!

Benjamin Masanja (Guest) on August 3, 2022

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Diana Mallya (Guest) on July 18, 2022

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

David Chacha (Guest) on May 10, 2022

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Charles Wafula (Guest) on March 17, 2022

Mungu akubariki!

Simon Kiprono (Guest) on March 6, 2022

Imani inaweza kusogeza milima

David Kawawa (Guest) on March 6, 2022

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Richard Mulwa (Guest) on February 16, 2022

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Rose Kiwanga (Guest) on August 26, 2021

Nakuombea πŸ™

Lydia Wanyama (Guest) on October 27, 2020

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Sharon Kibiru (Guest) on June 24, 2020

Katika imani, yote yanawezekana

Kenneth Murithi (Guest) on June 7, 2020

Rehema zake hudumu milele

Jane Malecela (Guest) on May 9, 2020

Baraka kwako na familia yako.

Edwin Ndambuki (Guest) on January 31, 2020

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Charles Mrope (Guest) on October 26, 2019

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Faith Kariuki (Guest) on August 31, 2019

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Nora Kidata (Guest) on March 13, 2019

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Isaac Kiptoo (Guest) on February 9, 2019

Endelea kuwa na imani!

Lydia Wanyama (Guest) on November 13, 2018

Tumaini ni nanga ya roho

Stephen Amollo (Guest) on October 5, 2018

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Kenneth Murithi (Guest) on August 28, 2018

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

James Kimani (Guest) on August 10, 2018

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Andrew Mchome (Guest) on July 15, 2018

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

John Mushi (Guest) on June 27, 2018

Mwamini Bwana; anajua njia

Alice Jebet (Guest) on April 16, 2018

Mwamini katika mpango wake.

David Sokoine (Guest) on March 9, 2018

Dumu katika Bwana.

James Kawawa (Guest) on February 11, 2018

Rehema hushinda hukumu

David Nyerere (Guest) on January 4, 2018

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Raphael Okoth (Guest) on December 26, 2017

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Alex Nyamweya (Guest) on October 12, 2017

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

George Tenga (Guest) on June 6, 2017

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Jacob Kiplangat (Guest) on May 18, 2017

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Mary Njeri (Guest) on April 17, 2017

Neema na amani iwe nawe.

Josephine Nekesa (Guest) on January 1, 2017

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Charles Mchome (Guest) on May 29, 2016

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Paul Ndomba (Guest) on April 11, 2016

Neema ya Mungu inatosha kwako

Jacob Kiplangat (Guest) on February 17, 2016

Sifa kwa Bwana!

Joyce Mussa (Guest) on December 31, 2015

Nguvu hutoka kwa Bwana

Paul Kamau (Guest) on December 1, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Ann Awino (Guest) on November 6, 2015

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Stephen Kangethe (Guest) on September 30, 2015

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Alex Nyamweya (Guest) on September 15, 2015

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Joy Wacera (Guest) on June 16, 2015

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Related Posts

MASOMO YA MISA, MACHI 24, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 24, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SOMO 1

Yer. 7:23-28

Read More

MASOMO YA MISA, JULAI 24, 2021: JUMAMOSI, JUMA LA 16 LA MWAKA

MASOMO YA MISA, JULAI 24, 2021: JUMAMOSI, JUMA LA 16 LA MWAKA

SOMO 1

Kut. 24:3-8

Musa aliwambia watu maneno yote ya Bwana, na hukumu zake zote;... Read More

MASOMO YA MISA, MACHI 21, 2022: JUMATATU , JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 21, 2022: JUMATATU , JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SOMO 1

2 Fal.... Read More

MASOMO YA MISA, JUNI 11, 2023: SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU

MASOMO YA MISA, JUNI 11, 2023: SHEREHE YA MWILI NA DAMU TAKATIFU YA BWANA WETU YESU KRISTU

SOMO 1

SOMO 1

Hos. 5... Read More

MASOMO YA MISA,Β JUNI 25, 2023: JUMAPILI YA 12 YA MWAKA

MASOMO YA MISA,Β JUNI 25, 2023: JUMAPILI YA 12 YA MWAKA

SOMO 1

SOMO IRead More

MASOMO YA MISA, JULAI 26, 2021 JUMATATU, JUMA LA 17 LA MWAKA

MASOMO YA MISA, JULAI 26, 2021 JUMATATU, JUMA LA 17 LA MWAKA

SOMO 1

Kut. 32:15-24, 30-34

Musa aligeuka akashuka katika mlima, na zile mbao mbi... Read More

πŸ“˜ About πŸ”’ Login πŸ“ Register πŸ“ž Contact