Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, APRILI 2, 2022: JUMAMOSI: JUMA LA 4 LA KWARESIMA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Β 

Yer. 11:18-20

Β 

Bwana akanijulisha haya, nami nikayajua; ndipo uliponionyesha matendo yao. Lakini mimi nalikuwa kama mwana-kondoo mpole, achukuliwaye kwenda kuchinjwa; wala sikujua ya kuwa wamefanya mashauri kinyume changu, wakisema, Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali atoke katika nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.

Lakini, Ee Bwana wa majeshi, uhukumuye haki ujaribuye viuno na moyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu.

Β 

Neno la Bwana… Tumshukuru Bwana.

Β 

WIMBO WA KATIKATI

Β 

Zab. 7:1-2, 8-12 (K) 1

Β 

(K) Bwana, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe.

Β 

Bwana, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe,

Uniokoe na wote wanaonifuatia, uniponye.

Asije akaipapura nafsi yangu kama samba,

Akiivunja-vunja pasipokuwa na wa kuponya. (K)

Β 

Bwana, unihukumu mimi,

Kwa kadiri ya haki yangu,

Sawasawa na unyofu nilio nao.

Ubaya wao wasio haki na ukome,

Lakini umthibitishe mwenye haki. (K)

Β 

Ngao yangu ina Mungu,

Awaokoaye wanyofu wa moyo.

Mungu ni mwamuzi mwenye haki,

Naam, Mungu aghadhibikaye kila siku. (K)

Β 

SHANGILIO

Β 

Lk. 15:18

Β 

Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia: Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako.

Β 

INJILI

Β 

Yn. 7:40-52

Β 

Wengine katika mkutano walipoyasikia maneno ya Yesu, walisema, Hakika huyu ndiye nabii yule. Wengine walisema, Huyu ndiye Kristo. Wengine wakasema, Je! Kristo atoka Galilaya? Andiko halikusema ya kwamba Kristo atoka katika uzao wa Daudi, na kutoka Bethlehemu, mji ule alioukaa Daudi? Basi kukaingia matengano katika mkutano kwa ajili yake. Baadhi yao wakataka kumkamata, alkini hakuna mtu aliyenyosha mikono yake ili kumshika.

Basi wale watumishi wakawaendea wakuu wa makuhani na Mafarisayo. Nao wakawaambia, Mbona hamkumleta? Wale watumishi wakajibu, Hajanena kamwe mtu yeyote kama huyu anavyonena. Basi Mafarisayo wakawajibu, Je! Ninyi nanyi mmedanganyika? Ni nani katika wakuu amwaminiye, au katika Mafarisayo? Lakini makutano hawa wasioifahamu torati wamelaaniwa.

Akawaambia Nikodemo, (naye ni yule aliyemwendea zamani, maana ni mmoja wao), Je! Torati yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza, na kujua atendavyo? Wakajibu, wakamwambia, Je! Wewe nawe umetoka Galilaya! Tafuta, ukaone ya kuwa kutoka Galilaya hakutokea nabii.

Β 

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Agnes Lowassa Guest Jul 4, 2024
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Jun 13, 2024
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest May 12, 2024
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Jan 5, 2024
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest May 10, 2023
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Dec 31, 2022
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Nov 28, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Jul 16, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Apr 29, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Apr 12, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest Mar 26, 2022
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Thomas Mtaki Guest Mar 8, 2022
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Agnes Njeri Guest Mar 7, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ James Mduma Guest Sep 1, 2021
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Mar 1, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Mariam Hassan Guest Feb 18, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest Jan 30, 2021
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ John Lissu Guest Jan 19, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ John Lissu Guest Dec 11, 2020
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Nov 21, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Mariam Hassan Guest Jun 3, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Frank Macha Guest May 30, 2020
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Apr 11, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Apr 2, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Jan 29, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Lydia Mzindakaya Guest Jan 27, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Jan 21, 2020
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest Jan 1, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Josephine Nduta Guest Dec 13, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Aug 21, 2019
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Mary Sokoine Guest Jun 22, 2019
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Jun 8, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Apr 8, 2019
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ David Ochieng Guest Jul 1, 2018
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Jun 23, 2018
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Grace Mligo Guest Jun 7, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ George Mallya Guest May 7, 2018
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Apr 28, 2018
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Feb 23, 2018
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Feb 22, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest Dec 12, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ James Kawawa Guest Aug 9, 2017
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Oct 9, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Agnes Njeri Guest Aug 17, 2016
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Jun 2, 2016
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest May 28, 2016
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ John Lissu Guest Feb 14, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Peter Tibaijuka Guest Feb 5, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Michael Mboya Guest Jan 20, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Dec 1, 2015
Rehema hushinda hukumu

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About