Sidebar with Floating Button
AckySHINE Katoliki
☰
AckyShine

MASOMO YA MISA, MACHI 30, 2022, JUMATANO: JUMA LA 4 LA KWARESIMA

Featured Image

SOMO 1

Β 

Isa. 49:8-15
Bwana asema hivi, Wakati uliokubalika nimekujibu, na siku ya wokovu nimekusaidia; nami nitakuhifadhi, nitakutoa uwe agano la watu hawa, ili kuiinua nchi hii, na kuwarithisha urithi uliokuwa ukiwa; kuwaambia waliofungwa, Haya, tokeni; na hao walio katika giza, Jionyesheni.
Watajilisha katika njia, na juu ya majabali watapata malisho. Hawataona njaa, wala hawataona kiu; hari haitawapiga, wala jua; kwa maana yeye aliyewarehemu atawatangulia, naam, karibu na chemchemi za maji atawaongoza. Nami nitafanya milima yangu yote kuwa njia, na njia kuu zangu zitatukuzwa zote.
Tazama, hawa watakuja kutoka mbali; na tazama, hawa kutoka kaskazini, na kutoka magharibi, na hawa kutoka nchi ya sinimu. Imbeni, enyi mbingu; ufurahi, Ee nchi; pazeni sauti ya kuimba, enyi milima; kwa kuwa Bwana amewafariji watu wake, naye atawahurumia watu wake walioteswa.
Bali Sayuni alisema, Yehova ameniacha, Bwana amenisahau. Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Β 

Zab. 145:8-9, 13-14, 17-18 (K)

(K) Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma.

Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma,
Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema.
Bwana ni mwema kwa watu wote,

Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote. (K)
Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote,
Ni mamlaka yako ni ya vizazi vyote.
Bwana huwategemeza wote waangukao,
Huwainua wote walioinama chini. (K)

Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote,
Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
Bwana yu karibu na wote wamwitao,
Wote wamwitao kwa uaminifu. (K)

SHANGILIO

Mt. 4:4

Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

INJILI

Yn. 5:17-30
Yesu aliwajibu Wayahudi: Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi. Basi kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kutaka kumwua, kwa kuwa hakuivunja sabato tu, bali pamoja na hayo alimwita Mungu Baba yake, akijifanya sawa na Mungu.
Basi Yesu akajibu, akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile. Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizi atamwonyesha ili ninyi mpate kustaajabu. Maana kama Baba awafufuavyo wafu na kuwahuisha, vivyo hivyo na Mwana ahuisha wale awatakao. Tena Baba hamhukumu mtu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote, ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba aliyempeleka.
Amin, amin, nawaambia, yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani. Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.
Maana kam avile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake. Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. Msistaajabie maneno hayo; kwa maana sasa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu. Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Robert Ndunguru (Guest) on June 16, 2024

Baraka kwako na familia yako.

Paul Ndomba (Guest) on February 11, 2024

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Isaac Kiptoo (Guest) on December 9, 2023

Mwamini katika mpango wake.

Mariam Kawawa (Guest) on October 7, 2023

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Lydia Wanyama (Guest) on July 3, 2023

Neema na amani iwe nawe.

Dorothy Mwakalindile (Guest) on June 26, 2023

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Margaret Mahiga (Guest) on June 13, 2023

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Grace Wairimu (Guest) on February 21, 2023

Imani inaweza kusogeza milima

Jane Muthui (Guest) on December 20, 2022

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Edwin Ndambuki (Guest) on November 27, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Frank Sokoine (Guest) on May 15, 2022

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Mary Sokoine (Guest) on April 2, 2022

Katika imani, yote yanawezekana

Charles Wafula (Guest) on December 25, 2021

Tumaini ni nanga ya roho

Bernard Oduor (Guest) on December 17, 2021

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Patrick Akech (Guest) on November 16, 2021

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Victor Kamau (Guest) on August 11, 2021

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Rose Mwinuka (Guest) on June 12, 2021

Mungu ni mwema, wakati wote!

Rose Amukowa (Guest) on June 6, 2021

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Dorothy Nkya (Guest) on March 2, 2021

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Nora Lowassa (Guest) on December 24, 2020

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Wilson Ombati (Guest) on November 23, 2020

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Francis Mrope (Guest) on July 30, 2020

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Rose Amukowa (Guest) on July 10, 2020

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Peter Mbise (Guest) on May 11, 2020

Dumu katika Bwana.

Hellen Nduta (Guest) on April 3, 2020

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Martin Otieno (Guest) on July 29, 2019

Nakuombea πŸ™

Daniel Obura (Guest) on July 26, 2019

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Esther Nyambura (Guest) on July 6, 2019

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

David Nyerere (Guest) on February 7, 2019

Rehema zake hudumu milele

Monica Nyalandu (Guest) on November 25, 2018

Nguvu hutoka kwa Bwana

Dorothy Majaliwa (Guest) on August 21, 2018

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Josephine Nekesa (Guest) on February 28, 2018

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Charles Mchome (Guest) on February 27, 2018

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

James Kawawa (Guest) on January 17, 2018

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Linda Karimi (Guest) on January 1, 2018

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Ruth Wanjiku (Guest) on November 23, 2017

Mwamini Bwana; anajua njia

Michael Mboya (Guest) on September 23, 2017

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Betty Kimaro (Guest) on July 28, 2017

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Grace Majaliwa (Guest) on March 3, 2017

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Chris Okello (Guest) on November 29, 2016

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Mariam Kawawa (Guest) on November 15, 2016

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Janet Mwikali (Guest) on July 12, 2016

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Rose Lowassa (Guest) on March 23, 2016

Mungu akubariki!

Stephen Kangethe (Guest) on December 26, 2015

Endelea kuwa na imani!

Irene Akoth (Guest) on November 10, 2015

Rehema hushinda hukumu

Sarah Karani (Guest) on August 28, 2015

Neema ya Mungu inatosha kwako

Mary Mrope (Guest) on June 10, 2015

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Carol Nyakio (Guest) on May 28, 2015

Sifa kwa Bwana!

Nancy Akumu (Guest) on May 5, 2015

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Alex Nyamweya (Guest) on April 26, 2015

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Related Posts

MASOMO YA MISA, MARCHI 31, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 4 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MARCHI 31, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 4 LA KWARESIMA

SOMO 1

Hek. 2:1, 12-22

Wasiomsadikia Mungu walisema hivi, huku wakimfikiri yasiyo... Read More

MASOMO YA MISA, MACHI 18, 2022:  IJUMAA, JUMA LA 2 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 18, 2022: IJUMAA, JUMA LA 2 LA KWARESIMA

SOMO 1

Mwa. 37:3-4, 12-13, 17-28

Β 

Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe ... Read More

MASOMO YA MISA, APRILI 4, 2022: JUMATATU, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, APRILI 4, 2022: JUMATATU, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

SOMO 1

Β 

Dan.13:41-62

Β 

Palikuwa na mtu mmoja jina lake Yoakimu, ak... Read More

MASOMO YA MISA, JUNI 18, 2023: JUMAPILI, JUMA LA 11 LA MWAKA

MASOMO YA MISA, JUNI 18, 2023: JUMAPILI, JUMA LA 11 LA MWAKA

SOMO 1 

SOMO 1

SHEREHE YA MT. YOSEFU, MUME WA BIKIRA MARIA

SOMO 1

SOMO 1

SOMO 1

Yer. 18-18-20

... Read More
MASOMO YA MISA, MACHI 26, 2022: JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 26, 2022: JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SOMO 1

Hos. 5... Read More

MASOMO YA MISA, MACHI 25, 2022: IJUMAA, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 25, 2022: IJUMAA, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 25, 2022
IJUMAA, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SHEREHE YA KUPASHWA HAB... Read More

πŸ“˜ About πŸ”’ Login πŸ“ Register πŸ“ž Contact