SOMO 1
Β
Isa. 49:8-15
Bwana asema hivi, Wakati uliokubalika nimekujibu, na siku ya wokovu nimekusaidia; nami nitakuhifadhi, nitakutoa uwe agano la watu hawa, ili kuiinua nchi hii, na kuwarithisha urithi uliokuwa ukiwa; kuwaambia waliofungwa, Haya, tokeni; na hao walio katika giza, Jionyesheni.
Watajilisha katika njia, na juu ya majabali watapata malisho. Hawataona njaa, wala hawataona kiu; hari haitawapiga, wala jua; kwa maana yeye aliyewarehemu atawatangulia, naam, karibu na chemchemi za maji atawaongoza. Nami nitafanya milima yangu yote kuwa njia, na njia kuu zangu zitatukuzwa zote.
Tazama, hawa watakuja kutoka mbali; na tazama, hawa kutoka kaskazini, na kutoka magharibi, na hawa kutoka nchi ya sinimu. Imbeni, enyi mbingu; ufurahi, Ee nchi; pazeni sauti ya kuimba, enyi milima; kwa kuwa Bwana amewafariji watu wake, naye atawahurumia watu wake walioteswa.
Bali Sayuni alisema, Yehova ameniacha, Bwana amenisahau. Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.
Neno la Bwana⦠Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Β
Zab. 145:8-9, 13-14, 17-18 (K)
(K) Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma.
Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma,
Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema.
Bwana ni mwema kwa watu wote,
Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote. (K)
Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote,
Ni mamlaka yako ni ya vizazi vyote.
Bwana huwategemeza wote waangukao,
Huwainua wote walioinama chini. (K)
Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote,
Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
Bwana yu karibu na wote wamwitao,
Wote wamwitao kwa uaminifu. (K)
SHANGILIO
Mt. 4:4
Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
INJILI
Yn. 5:17-30
Yesu aliwajibu Wayahudi: Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi. Basi kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kutaka kumwua, kwa kuwa hakuivunja sabato tu, bali pamoja na hayo alimwita Mungu Baba yake, akijifanya sawa na Mungu.
Basi Yesu akajibu, akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile. Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizi atamwonyesha ili ninyi mpate kustaajabu. Maana kama Baba awafufuavyo wafu na kuwahuisha, vivyo hivyo na Mwana ahuisha wale awatakao. Tena Baba hamhukumu mtu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote, ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba aliyempeleka.
Amin, amin, nawaambia, yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani. Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.
Maana kam avile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake. Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. Msistaajabie maneno hayo; kwa maana sasa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu. Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka.
Neno la Bwana⦠Sifa kwako Ee Kristo.
Robert Ndunguru (Guest) on June 16, 2024
Baraka kwako na familia yako.
Paul Ndomba (Guest) on February 11, 2024
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Isaac Kiptoo (Guest) on December 9, 2023
Mwamini katika mpango wake.
Mariam Kawawa (Guest) on October 7, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Lydia Wanyama (Guest) on July 3, 2023
Neema na amani iwe nawe.
Dorothy Mwakalindile (Guest) on June 26, 2023
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Margaret Mahiga (Guest) on June 13, 2023
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Grace Wairimu (Guest) on February 21, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
Jane Muthui (Guest) on December 20, 2022
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Edwin Ndambuki (Guest) on November 27, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Frank Sokoine (Guest) on May 15, 2022
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mary Sokoine (Guest) on April 2, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
Charles Wafula (Guest) on December 25, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
Bernard Oduor (Guest) on December 17, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Patrick Akech (Guest) on November 16, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Victor Kamau (Guest) on August 11, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Rose Mwinuka (Guest) on June 12, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
Rose Amukowa (Guest) on June 6, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Dorothy Nkya (Guest) on March 2, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Nora Lowassa (Guest) on December 24, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Wilson Ombati (Guest) on November 23, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Francis Mrope (Guest) on July 30, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Rose Amukowa (Guest) on July 10, 2020
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Peter Mbise (Guest) on May 11, 2020
Dumu katika Bwana.
Hellen Nduta (Guest) on April 3, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Martin Otieno (Guest) on July 29, 2019
Nakuombea π
Daniel Obura (Guest) on July 26, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Esther Nyambura (Guest) on July 6, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
David Nyerere (Guest) on February 7, 2019
Rehema zake hudumu milele
Monica Nyalandu (Guest) on November 25, 2018
Nguvu hutoka kwa Bwana
Dorothy Majaliwa (Guest) on August 21, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Josephine Nekesa (Guest) on February 28, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Charles Mchome (Guest) on February 27, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
James Kawawa (Guest) on January 17, 2018
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Linda Karimi (Guest) on January 1, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Ruth Wanjiku (Guest) on November 23, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
Michael Mboya (Guest) on September 23, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Betty Kimaro (Guest) on July 28, 2017
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Grace Majaliwa (Guest) on March 3, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Chris Okello (Guest) on November 29, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mariam Kawawa (Guest) on November 15, 2016
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Janet Mwikali (Guest) on July 12, 2016
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rose Lowassa (Guest) on March 23, 2016
Mungu akubariki!
Stephen Kangethe (Guest) on December 26, 2015
Endelea kuwa na imani!
Irene Akoth (Guest) on November 10, 2015
Rehema hushinda hukumu
Sarah Karani (Guest) on August 28, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mary Mrope (Guest) on June 10, 2015
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Carol Nyakio (Guest) on May 28, 2015
Sifa kwa Bwana!
Nancy Akumu (Guest) on May 5, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Alex Nyamweya (Guest) on April 26, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni