Sidebar with Floating Button
AckySHINE Katoliki
☰
AckyShine

MASOMO YA MISA, JUNI 18, 2023: JUMAPILI, JUMA LA 11 LA MWAKA

Featured Image

SOMO 1 





Kut. 19 :2-6





Waisraeli walipokuwa wameondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, wakatua katika lile jangwa; wakapiga kambi huko wakiukabili mlima. Musa akapanda kwa Mungu, na Bwana akamwita toka mlima ule, akisema, Utawaambia nyumba ya Yakobo, na kuwaarifu wana wa Israeli, maneno haya: Mmeona jinsi nilivyowatendea Wamisri, na jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi. Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu, nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.





Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.





WIMBO WA KATIKATI 





Zab. 100 :2-3, 5 (K) 3





(K) Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.





Mtumikieni Bwana kwa furaha;





Njoni mbele zake kwa kuimba. (K)





Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu;





Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;





Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)





Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;





Rehema zake ni za milele;





Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)





SOMO 2 





Rum. 5 : 6-11





Wapendwa, hapo tulipokuwa hatuna nguvu, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu. Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema. Bali Mungu aonyesha pendo lake veye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake, zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake. Wala si hivyo tu, ila pia twajifurahisha katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo, am have kwa yeye sasa tumeupokea huo upatanisho.





Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.





SHANG1LIO 





Yn. 15 :15





Aleluya, aleluya, Ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.





Aleluya.





INJILI 





Mt. 9:36-10:8





Yesu alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji. Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake. Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza





magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Na majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya; Wa kwanza Simoni aliyeitwa Petro, na Andrea nduguye; Yakobo wa Zebedayo, na Yohane nduguye; Filipo, na Bartholomayo; Tomaso, na Mathayo mtoza ushuru; Yakobo wa Alfayo, na Thadayo; Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote, naye ndiye mwenye kumsaliti. Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie. Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.





Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.


AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Elizabeth Mrema (Guest) on June 28, 2024

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Irene Makena (Guest) on July 1, 2023

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

David Kawawa (Guest) on January 10, 2023

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Mary Sokoine (Guest) on December 24, 2022

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Grace Majaliwa (Guest) on September 11, 2022

Mwamini katika mpango wake.

Nora Lowassa (Guest) on September 4, 2022

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Josephine Nekesa (Guest) on July 27, 2022

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Mercy Atieno (Guest) on June 13, 2022

Kwa Mungu, yote yanawezekana

John Mwangi (Guest) on April 9, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Victor Sokoine (Guest) on March 9, 2022

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Ruth Wanjiku (Guest) on January 13, 2022

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Andrew Mchome (Guest) on December 6, 2021

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Esther Cheruiyot (Guest) on December 4, 2021

Neema na amani iwe nawe.

Benjamin Masanja (Guest) on November 21, 2021

Sifa kwa Bwana!

Paul Kamau (Guest) on November 1, 2021

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Nicholas Wanjohi (Guest) on September 14, 2021

Endelea kuwa na imani!

Sarah Karani (Guest) on April 1, 2021

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Monica Nyalandu (Guest) on March 16, 2021

Katika imani, yote yanawezekana

Esther Cheruiyot (Guest) on February 2, 2021

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Ruth Kibona (Guest) on December 27, 2020

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

David Musyoka (Guest) on November 9, 2020

Nguvu hutoka kwa Bwana

Samuel Were (Guest) on February 2, 2020

Mungu akubariki!

Samson Tibaijuka (Guest) on January 5, 2020

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Peter Mbise (Guest) on July 11, 2019

Mwamini Bwana; anajua njia

Nancy Komba (Guest) on June 29, 2019

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Wilson Ombati (Guest) on June 28, 2019

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Michael Mboya (Guest) on June 11, 2019

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Sharon Kibiru (Guest) on June 5, 2019

Baraka kwako na familia yako.

Charles Mchome (Guest) on April 20, 2019

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Paul Ndomba (Guest) on January 24, 2019

Mungu ni mwema, wakati wote!

Catherine Mkumbo (Guest) on December 5, 2018

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Nora Lowassa (Guest) on October 20, 2018

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Charles Mrope (Guest) on September 9, 2018

Rehema zake hudumu milele

John Lissu (Guest) on August 25, 2018

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Nicholas Wanjohi (Guest) on July 3, 2018

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Nancy Kabura (Guest) on June 28, 2018

Nakuombea πŸ™

Isaac Kiptoo (Guest) on February 27, 2018

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Victor Malima (Guest) on December 28, 2017

Imani inaweza kusogeza milima

Bernard Oduor (Guest) on August 28, 2017

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Lydia Mutheu (Guest) on March 6, 2017

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Anna Malela (Guest) on February 27, 2017

Tumaini ni nanga ya roho

Janet Wambura (Guest) on December 20, 2016

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Chris Okello (Guest) on August 21, 2016

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Agnes Njeri (Guest) on August 8, 2016

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Jane Muthoni (Guest) on March 27, 2016

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Josephine Nekesa (Guest) on January 10, 2016

Dumu katika Bwana.

Joseph Kitine (Guest) on November 9, 2015

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Moses Kipkemboi (Guest) on August 30, 2015

Rehema hushinda hukumu

Janet Mwikali (Guest) on July 23, 2015

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Victor Sokoine (Guest) on April 27, 2015

Neema ya Mungu inatosha kwako

Related Posts

MASOMO YA MISA, MACHI 23, 2022: JUMATANO JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 23, 2022: JUMATANO JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 23, 2022: JUMATANO JUMA LA 3 LA KWARESI

SOMO 1 - Kumb. 4:1, 5-9

... Read More
MASOMO YA MISA,Β JUNI 25, 2023: JUMAPILI YA 12 YA MWAKA

MASOMO YA MISA,Β JUNI 25, 2023: JUMAPILI YA 12 YA MWAKA

SOMO 1

SOMO 1

SOMO IRead More

MASOMO YA MISA, APRILI 4, 2022: JUMATATU, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, APRILI 4, 2022: JUMATATU, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

SOMO 1

Β 

Dan.13:41-62

Β 

Palikuwa na mtu mmoja jina lake Yoakimu, ak... Read More

MASOMO YA MISA, MACHI 17, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 2 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 17, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 2 LA KWARESIMA

SOMO 1

Yer. 17:5-10

Bwana asema hivi: Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, a... Read More
MASOMO YA MISA, MACHI 26, 2022: JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 26, 2022: JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SOMO 1

Hos. 5... Read More

πŸ“˜ About πŸ”’ Login πŸ“ Register πŸ“ž Contact