SOMO 1
Kut. 19 :2-6
Waisraeli walipokuwa wameondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, wakatua katika lile jangwa; wakapiga kambi huko wakiukabili mlima. Musa akapanda kwa Mungu, na Bwana akamwita toka mlima ule, akisema, Utawaambia nyumba ya Yakobo, na kuwaarifu wana wa Israeli, maneno haya: Mmeona jinsi nilivyowatendea Wamisri, na jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi. Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu, nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 100 :2-3, 5 (K) 3
(K) Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.
Mtumikieni Bwana kwa furaha;
Njoni mbele zake kwa kuimba. (K)
Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu;
Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;
Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)
Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)
SOMO 2
Rum. 5 : 6-11
Wapendwa, hapo tulipokuwa hatuna nguvu, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu. Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema. Bali Mungu aonyesha pendo lake veye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake, zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake. Wala si hivyo tu, ila pia twajifurahisha katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo, am have kwa yeye sasa tumeupokea huo upatanisho.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.
SHANG1LIO
Yn. 15 :15
Aleluya, aleluya, Ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.
Aleluya.
INJILI
Mt. 9:36-10:8
Yesu alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji. Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake. Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza
magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Na majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya; Wa kwanza Simoni aliyeitwa Petro, na Andrea nduguye; Yakobo wa Zebedayo, na Yohane nduguye; Filipo, na Bartholomayo; Tomaso, na Mathayo mtoza ushuru; Yakobo wa Alfayo, na Thadayo; Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote, naye ndiye mwenye kumsaliti. Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie. Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.
Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.
Elizabeth Mrema (Guest) on June 28, 2024
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Irene Makena (Guest) on July 1, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
David Kawawa (Guest) on January 10, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Mary Sokoine (Guest) on December 24, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Grace Majaliwa (Guest) on September 11, 2022
Mwamini katika mpango wake.
Nora Lowassa (Guest) on September 4, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Josephine Nekesa (Guest) on July 27, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mercy Atieno (Guest) on June 13, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
John Mwangi (Guest) on April 9, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Victor Sokoine (Guest) on March 9, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Ruth Wanjiku (Guest) on January 13, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Andrew Mchome (Guest) on December 6, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Esther Cheruiyot (Guest) on December 4, 2021
Neema na amani iwe nawe.
Benjamin Masanja (Guest) on November 21, 2021
Sifa kwa Bwana!
Paul Kamau (Guest) on November 1, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Nicholas Wanjohi (Guest) on September 14, 2021
Endelea kuwa na imani!
Sarah Karani (Guest) on April 1, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Monica Nyalandu (Guest) on March 16, 2021
Katika imani, yote yanawezekana
Esther Cheruiyot (Guest) on February 2, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Ruth Kibona (Guest) on December 27, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
David Musyoka (Guest) on November 9, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
Samuel Were (Guest) on February 2, 2020
Mungu akubariki!
Samson Tibaijuka (Guest) on January 5, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Peter Mbise (Guest) on July 11, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
Nancy Komba (Guest) on June 29, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Wilson Ombati (Guest) on June 28, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Michael Mboya (Guest) on June 11, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Sharon Kibiru (Guest) on June 5, 2019
Baraka kwako na familia yako.
Charles Mchome (Guest) on April 20, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Paul Ndomba (Guest) on January 24, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
Catherine Mkumbo (Guest) on December 5, 2018
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Nora Lowassa (Guest) on October 20, 2018
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Charles Mrope (Guest) on September 9, 2018
Rehema zake hudumu milele
John Lissu (Guest) on August 25, 2018
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Nicholas Wanjohi (Guest) on July 3, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Nancy Kabura (Guest) on June 28, 2018
Nakuombea π
Isaac Kiptoo (Guest) on February 27, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Victor Malima (Guest) on December 28, 2017
Imani inaweza kusogeza milima
Bernard Oduor (Guest) on August 28, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Lydia Mutheu (Guest) on March 6, 2017
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Anna Malela (Guest) on February 27, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
Janet Wambura (Guest) on December 20, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Chris Okello (Guest) on August 21, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Agnes Njeri (Guest) on August 8, 2016
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Jane Muthoni (Guest) on March 27, 2016
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Josephine Nekesa (Guest) on January 10, 2016
Dumu katika Bwana.
Joseph Kitine (Guest) on November 9, 2015
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Moses Kipkemboi (Guest) on August 30, 2015
Rehema hushinda hukumu
Janet Mwikali (Guest) on July 23, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Victor Sokoine (Guest) on April 27, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako