Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Swala la Mapadri kutooa limeandikwa wapi katika Biblia?

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

JE,SHERIA YA MAPADRE KUTOOA NA KUISHI USEJA IMEANDIKWA WAPI KATIKA BIBLIA AU IMETUNGWA TU NA PAPA?

Pengine umewahi kuulizwa swali hili wakati fulani.Na jibu lake ni kama ifuayavyo:
Mtu anapouliza kila kitu kimeandikwa wapi katika Biblia ni kudhihirisha kutokuijua au kuielewa vizuri Biblia Takatifu na historia yake.Mtu anapong'ang'ania "nionyeshe kitu fulani kimeandikwa wapi kwenye Biblia"ni kutaka kujiona ya kwamba yeye anaielewa sana Biblia na ameisoma yote kwa hiyo kila kitu kilichopo kwenye Biblia anakifahamu kumbe haijui Biblia bali anakariri Biblia!
Na hili suala la kushupalia swala la kuoa linadhihirisha jinsi gani tulivyo kizazi cha zinaa,ni kama tunadhani kuwa UZIMA upo katika kujamiiana!La hasha.
Paulo anasema "Kwasababu ya zinaa ni bora kuoa na kuolewa"(1Wakorintho 7:2.9) haya sio maneno ya kufurahia na kuchekelea tu maana "YANAWALENGA WALE WALIOSHINDIKANA KATIKA YALE YAPENDEZAYO"(1Wakorintho 7:1.8)sasa ni lazima tujiulize je tumeshindikana kiasi hicho?,hiyo sio sifa!
1Wakorintho 7:1.8
"Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika,ni heri mwanaume asimguse mwanamke,8.Lakini nawaambia wale wasiooa bado na wajane heri wakae kama mimi nilivyo"
Na Paulo Mtume anasema "Ni bora kuoa au kuolewa" lakini hakusema "Ni LAZIMA kuoa au kuolewa"
Suala la kutooa kwa mapadre kadiri ya historia lilianza tangu zamani kabisa mwanzoni mwa milenia ya pili katika mtagusi wa pili wa Laterani mwaka wa 1139 ili waweze kumtumikia Mungu kwa uhuru na bila mawaa wala pasipo vikwazo(1wakorintho 7:32-35)
1wakorintho 7:32-35
"32Lakini nataka msiwe na masumbufu.Yeye asiyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya Bwana ampendezeje Bwana;33.bali yeye aliyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendeza mkewe.34-Tena iko tofauti kati ya mke na mwanamwali.Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana ili apate kuwa mtakatifu mwili na Roho.Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendezesha mumewe.,35.Nasema hayo niwafaidie ninyi,si kwamba niwategee tanzi,bali kwaajili ya vile vipendezavyo,tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine"
Maandiko hayo hapo juu yanajieleza wala sidhani kama yanahitaji kufafanuliwa zaidi ya yanavyojifafanua yenyewe.
Watu wengine wanafikiri kwamba kutooa ni dhambi,kama ni hivyo basi hata Yesu mwenyewe alikosa maana hata yeye mwenyewe hakuoa.
Yesu mwenyewe anafundisha kuhusu ubikira(Mathayo 19:10-12)
Mathayo 19:10-12,
"Wanafunzi wake wakamwambia,kama mambo ya mme na mke yakiwa hivyo ni afadhali kutuooa kabisa.Lakini Yeye akawaambia 'SI WOTE WAWEZAO KULIPOKEA NENO HILO,ILA TU WALE WALIOJALIWA,maana wako MATOWASHI waliozaliwa katika hali hiyo toka matumboni mwa mama zao;tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi,tena wako Matowashi WALIOJIFANYA WENYEWE KUWA MATOWASHI KWAAJILI YA UFALME WA MBINGUNI',awezaye kulipokea neno hili na alipokee"
Yesu mwenyewe analifafanua jambo hili kwa mapana,katika orodha ya matowashi Yesu aliowataja,Mapadre ni Matowashi waliojifanya hivyo kwaajili ya huduma ya kanisa na ufalme wa Mungu.
Tena Yesu anatuambia waziwazi kwamba"sio wote wawezao kulipokea neno hilo"yaani sasa sio wote wawezao kuwa Matowashi(Mapadre)bali ni wale tu waliojaliwa na Mungu neema hiyo.wale wasioweza kuishi upadre huoa na kuwa na familia.Tena Yesu anamalizia kwa kusema "Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee",kwa maana nyingine ni kusema "Fundisho au Utowashi huu sio wa lazima"anayeweza kuishi maisha hayo basi na ayapokee na yule asiyeweza basi aache!
Vilevile Mitume ili kumfuata Yesu kikamilifu waliyaacha yote waliokuwa nayo ikiwepo familia zao ili wamtumikie Bwana(Mathayo 19:27.29)
Mathayo 19:27.29:
"Ndipo Petro akajibu akamwambia 'Tazama sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe,tutapata nini basi?29.Amini nawaambia,kila mtu aliyeacha nyumba au ndugu wa kiume au wakike,au baba au mama au watoto au mashamba KWAAJILI YA JINA LANGU,atapokea mara mia zaidi na kuurithi uzima wa milele"
katika injili hiyo,Yesu anadhihirisha kwamba aliyeacha hayo yaliotajwa si kwasababu hawezi kuyapata la hasha,bali ameyaacha hayo yote KWAAJILI YA JINA LA YESU atapokea mengi hapa duniani halafu tena ataurithi ufalme wa mbinguni.
Mapadre wameyaacha hayo yote,wameacha nyumba,familia zao na kila kitu SIO KWASABABU HAWANA UWEZO AU HAWAWEZI KUPATA MAMBO HAYO bali WAMEACHA KWASABABU YA KUMTUMIKIA MUNGU KWA KADIRI YA MAANDIKO MATAKATIFU na kwakutaka kwao kuyaishi kimamilifu MASHAURI YA INJILI ikiwepo USEJA.
Maneno ya Paulo na yale ya Yesu mwenyewe kuhusu kumtumikia Mungu bila kuoa sio ya bahati mbaya bali ndiyo njia bora na inayofaa sana na kukubalika mbele ya Mungu.
Kwahiyo unapowaona mapadre hawaoi ujue sababu yake ni hiyo kwamba "Wamejitoa kwaajili ya kulihudumia kanisa"
(Na pia huwa nawashangaa mno watu wanaowapiga vita Mapadre kwamba kwanini hawaoi,najiuliza je,hao Mapadre wamewakataza wao kwamba wasioe?.)..na kama jibu ni hapana,sasa Je,"Pilipili ya shamba usiyoila inakuwashia nini?"
TUMSIFU YESU KRISTO!
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest May 22, 2024
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest Apr 26, 2024
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Feb 28, 2024
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest Nov 19, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Oct 8, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Sep 15, 2023
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Jun 27, 2023
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Jun 17, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Apr 8, 2023
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Feb 17, 2023
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Dec 31, 2022
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Dec 20, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Francis Njeru Guest Oct 11, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Jan 7, 2022
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Emily Chepngeno Guest Nov 7, 2021
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Oct 31, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Sep 16, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Jun 23, 2021
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest May 14, 2021
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Mar 12, 2021
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Nov 27, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Nov 12, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Sep 4, 2020
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Violet Mumo Guest Jul 23, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ David Sokoine Guest May 31, 2020
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Apr 30, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Apr 10, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Nov 7, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Sep 9, 2018
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Aug 21, 2018
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Aug 5, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Jul 8, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ John Lissu Guest Jul 6, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Apr 27, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Dec 28, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest Dec 10, 2017
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Oct 19, 2017
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Jul 2, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest May 26, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Feb 18, 2017
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Joseph Mallya Guest Sep 8, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Jun 13, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Apr 17, 2016
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ David Nyerere Guest Mar 7, 2016
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ John Lissu Guest Feb 10, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Stephen Amollo Guest Jul 17, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Jun 10, 2015
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Apr 23, 2015
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest Apr 13, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Peter Mwambui Guest Apr 9, 2015
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About