Sidebar with Floating Button
AckySHINE Katoliki
☰
AckyShine

Maswali na Majibu kuhusu Kuabudu kwa Wakatoliki

Featured Image

Wakatoliki tunamwabudu Mungu kwa namna gani?


Tunamwabudu Mungu kwa sala , sadaka na matendo mema







Je, tuna ruhusa ya kuwaabudu Watakatifu?


Hatuna ruhusa ya kuwaabudu Watakatifu tunawaheshimu tu.







Je sanamu zimekatazwa?


Sanamu hazijakatazwa, ila tunaziheshimu kwa sababu zinatukumbusha Mungu na Watakatifu. (Kut 25:18-22).

18 Nawe fanya makerubi mawili ya dhahabu; uyafanye ya kazi ya kufua, katika hiyo miisho ya kiti cha rehema, huku na huku. 19 Weka kerubi moja mwisho mmoja, na kerubi la pili mwisho wa pili; fanya hayo makerubi ya kitu kimoja na kiti cha rehema, mwisho huku na mwisho huku. 20 Na hayo makerubi yatainua mabawa yao juu, na kukifunika hicho kiti cha rehema kwa mabawa yao, na nyuso zao zitaelekeana hili na hili; nyuso za hayo makerubi zitaelekea kiti cha rehema. 21 Weka kiti cha rehema juu ya hilo sanduku, kisha utie huo ushuhuda nitakaokupa ndani ya sanduku. 22 Nami nitaonana nawe hapo, na kuzungumza nawe pale nilipo juu ya kiti cha rehema, katikati ya hayo makerubi mawili yaliyo juu ya sanduku la ushuhuda, katika mambo yote nitakayokuagiza kwa ajili ya wana wa Israeli. Kutoka 25 :18-22.

Vile vile Mungu alishawahi kuwaagiza Waisraeli Wachonge sanamu ya nyoka na yeyote atakayeumwa na nyoka akiiangalia atapona.







Mfano wa sanamu takatifu ni zipi?


Sanamu ya Bikira Maria, Mtoto Yesu, Mt. Yosefu, Moyo wa Yesu na za Watakatifu.







Ni nanai ana kosa kumuabudu Mungu?


Anayekosa kumuabudu Mungu ni yule;

1. Anayeacha kusali au anayesali hovyo
2. Anayemkufuru Mungu
3. Anayeamini na kushika mambo ya kipagani







Ni nini maana ya kuabudu sanamu?


Kuabudu sanamu ni kukipa kiumbe chochote heshima au upendo anaostahili Mungu peke yake.







Kutokumuabudu Mungu ni kwa namna gani?


Ni kuruhusu kitu chochote kimtawale mtu badala ya Mungu, mfano cheo, pombe, mali, shetani, tuisheni, kazi, na kutoadhimisha Jumapili au kutoshiriki.







Mkatoliki anaabuduje?


Mkatoliki anaabudu kwa kupiga goti au magoti mawili na ni mbele ya sakramenti ya Ekaristi Takatifu tuu hasa wakati wa kuingia na kutoka kanisani







Je magoti yanayopigwa wakati mwingine tofauti na wakati wa kuabudu yana maana gani?


Magoti yanayopigwa wakati wa sala mfano kanisani, nyumbani, mbele ya sanamu, jumuiyani, shuleni yanaitwa Mkao wa sala







Kwa nini wakatoliki wanaweka sanamu Kanisani?


Tunaweka sanamu Kanisani kwa sababu tunaheshimu anayewakilishwa na sanamu hiyo kwa mfano Yesu Kristo, Mama Bikira Maria, Malaika na Watakatifu; na kamwe hatuziabudu. (Kutoka 25:18-22)

Hata Waisraeli kwenye hekalu lao walikua na sanamu kama tunavyosoma hapa;

"18 Nawe fanya makerubi mawili ya dhahabu; uyafanye ya kazi ya kufua, katika hiyo miisho ya kiti cha rehema, huku na huku. 19 Weka kerubi moja mwisho mmoja, na kerubi la pili mwisho wa pili; fanya hayo makerubi ya kitu kimoja na kiti cha rehema, mwisho huku na mwisho huku.20 Na hayo makerubi yatainua mabawa yao juu, na kukifunika hicho kiti cha rehema kwa mabawa yao, na nyuso zao zitaelekeana hili na hili; nyuso za hayo makerubi zitaelekea kiti cha rehema. 21 Weka kiti cha rehema juu ya hilo sanduku, kisha utie huo ushuhuda nitakaokupa ndani ya sanduku. 22 Nami nitaonana nawe hapo, na kuzungumza nawe pale nilipo juu ya kiti cha rehema, katikati ya hayo makerubi mawili yaliyo juu ya sanduku la ushuhuda, katika mambo yote nitakayokuagiza kwa ajili ya wana wa Israeli. (Kutoka 25 :18-22.)"

Kwa hiyo kama Mungu mwenyewe aliagiza Sanamu za Malaika zichongwe na kusema atakua hapo na kuongea na watu wake. Je sio vyema zaidi kuwa na sanamu na Picha ya Mwanae wa Pekee Yesu Kristo na kuongea na Mungu mbele yake kama alitaka ya malaika ambao sio Mungu?

Mfano mwingine ni pale Mungu alivyomwabia Musa achonge Sanamu ya Nyoka wa shaba.

"BWANA akamwambia Mose, β€œTengeneza nyoka wa shaba na umweke juu ya mti, ye yote aliyeumwa na nyoka anaweza kumtazama na akaishi tena.’’ 9Kwa hiyo Mose akatengeneza nyoka wa shaba na kumweka juu ya mti. Kisha wakati mtu ye yote alipoumwa na nyoka, naye akamtazama yule nyoka wa shaba, aliishi." (Hesabu 21:8-9).

Kwa Mfano huu Je tunaweza kusema kuwa sanamu ya nyoka ina nguvu ya uponyaji kuliko ya Yesu aliye Mungu? Kumbuka hapa watu walioona sanamu hii ya nyoka hawakukoponywa na nguvu ya sanamu ya shaba bali kwa nguvu ya neema ya Mungu kupitia Imani kwa Mungu. Kwa hiyo unaposali mbele ya picha au sanamu hautegemei nguvu ya sanamu bali unategemea neema ya Mungu kwa njia ya Imani yako kwa Mungu.

Kama vile Sanamu hii ya nyoka aliyoagiza Mungu iwekwe ilivyowekwa kwa nia ya uponyaji kwa yule aitazamaye vivyo hivyo Sanamu na Picha za Kanisani zinawekwa kwa nia maalumu na kwa neema maalumu. Ndiyo maana hazifanani. Na zinabarikiwa kwa kuombewa Baraka Ili zizae neema kwa wanaozitumia.

Sanamu au picha sio haramu bali maana ya hiyo sanamu au picha ndio inaiharamisha.


Kuna tofauti kati ya kuabudu na kuheshimu. Wakatoliki wanaweka sanamu kwa heshima na sio kwa kuabudu, ndio maana unaposali mbele ya picha ya Yesu hausali ee sanamu nisaidie bali unasema ee Yesu nisaidie.

Je tuseme tunamwabudu Raisi kwa kuheshimu picha yake kwa kuiinamia? Je tunaabudu bendera kwa kuheshimu na kupigia saluti? Je taratibu zabunge za kutoa heshima na taratibu za mahakama ni kuabudu?. Je kuapa mbele ya picha ya Raisi ni kumuabudu Raisi? Je kuapa na Biblia ni kuabudu Biblia? Je tunapobusu Biblia na kuitunza kwa heshima tunaiabudu? Tofauti ya Biblia na sanamu ni nini? Je, kwenye Biblia kinachoheshimiwa ni karatasi au maana ya yale maneno kwenye karatasi. Pengine usingeheshimu kama hujajua kuyasoma.

Kuna tofauti gani kati ya biblia yenye Maandishi na msalaba wa kuchonga wenye kuonyesha kile kinachosemwa na biblia? kama unaweza kuheshimu biblia yenye karatasi tena pale unapoweza kuzisoma na pengine ungeizarau kama ni ya lugha tofauti na hujui kilichoandikwa? Je Msalaba uliobeba maana ya kile kilichoandikwa kwenye Biblia unaona si kitu? Kama Kinachoheshimiwa kwenye Biblia sio karatasi bali maana maneno yaliyoandikwa vivyo hivyo kinachoheshimiwa kwenye picha au sanamu sio chuma yake au mti ukiochongwa bali ni maana ya hiyo sanamu.

Hii ndio maana nasema kuna tofauti ya kuabudu na kuheshimu.

Kumbuka kuwa picha au sanamu yoyote ya Kikatoliki lazima ibarikiwe kwanza ndio uweze Kusali mbele yake. Inapobarikiwa inaombewa uwepo wa yule anayewakilishwa na picha/sanamu hiyo uwe pale sanamu ilipo na anayesali pale sala yake Ifike kwa mlengwa anayeonekana kwa ishara ya sanamu/picha. Kwa Mfano askofu au padri anapobariki sanamu ya Yesu anaomba kuwa "Yesu awepo pale kwenye sanamu na Neema zake", kwa hiyo yeyote anayesali mbele ya sanamu hiyo anaamini kuwa Yesu yuko pale na anasali Mbele yake. Kwa hiyo kinachopewa heshima sio ile sanamu bali ni yule anayeonekana kwa ishara ya ile sanamu au picha.

Tofauti ya Sanamu za Kikatoliki na za kipagani ni Kwamba,


Sanamu za Kipagani: Sanamu hizi huchukuliwa kama Mungu na huabudiwa na kutolewa Sadaka kama Mungu Mwenyewe.


Sanamu za Kikatoliki: Sanamu hizi huchukuliwa kama ishara ya kile inachokiwakilisha, haiabudiwi kamwe bali inaheshimiwa tuu.


Daima Tumia Sanamu na Picha zilizobarikiwa kwani zimenuiwa uwepo wa yule inayemuwakilisha na utaongea naye hapo. Sisi tunaamini kwamba kwenye Sanamu ya Yesu kuna uwepo wa Yesu. Kama vile Mungu anavyowaambia Waisraeli katika (Kutoka 25 :22) baada ya kuwaagiza wachonge sanamu za Makerubi (Malaika) 22 Nami nitaonana nawe hapo, na kuzungumza nawe pale nilipo juu ya kiti cha rehema, katikati ya hayo makerubi mawili yaliyo juu ya sanduku la ushuhuda, katika mambo yote nitakayokuagiza kwa ajili ya wana wa Israeli. (Kutoka 25 :22)Sanamu au picha ni ishara wazi ya uwepo wa kile kisichoonekana.

Jifunze kupitia Sanduku la Agano na Msalaba wa Yesu


Kwenye Agano la kale: Ndani ya hekalu la Waisraeli walikua na Sanduku la agano, sanduku hilo lilikua na vibao vya Amri za Mungu ambavyo ni Ishara ya Agano lao na Mungu na ndani ya sanduku kulikuwepo pia Mfano wa Kiti ambacho kimezugukwa na sanamu za viumbe kama malaika nyuso zao zikielekea kiti hicho Kutoka 25:10-22. Waisraeli walikua wanasali kuelekea sanduku la Agano wanapokuwa Hekaluni na hata wakiwa majumbani mwao walisali kuelekea upande lilipo Hekalu. Waisraeli walisali kuelekea Sanduku la Agano wakiamini kwamba Mungu yupo kati ya sanduku lile. Lakini sanduku lile halikuwa Mungu. Waisraeli waliona fahari juu ya Sanduku lile na walilithamini na kuliheshimu kwa kuwa lilionyesha uwepo wa Mungu na popote lilipokuwa waliamini Mungu yupo.

Kwenye Agano jipya: Wakristu wanasali Mbele ya Msalaba wa Yesu ambao unaonyesha kazi ya wokovu alioufanya Yesu kwa wanadamu ya Kuwakomboa watu kwa kifo chake Msalabani. Na Msalaba huo ni Ishara ya Ukombozi wa Agano jipya na la Milele. Kama ilivyokuwa kwa Sanduku la Agano, Wakristu wanaheshimu msalaba ambao ni ishara ya wokovu wao na wanaamini kuwa Mungu yupo kati ya Msalaba huo lakini Msalaba huo sio Mungu. Wakristu wanaona fahari juu ya msalaba wa Yesu kwa kuwa ndio ishara ya wokovu wao.

FUNZO:Kupitia Mfano wa Sanduku la Agano na Msalaba tunajifunza kuwa Vyote havikuwa Mungu ila vinaheshimiwa kwa Imani kuwa Mungu yupo pale. Vilevile, vyote ni ishara ya wazi ya Agano la Mungu na Wanadamu.

Kwa nini tunasali mbele ya Picha/Sanamu na Hasa kufanya Ishara ya msalaba?


Tunasali mbela ya sanamu kwa sababu tunaamini sanamu inaakisi uwepo wa mhusika aliyechorwa au kuchongwa kwenye hiyo sanamu/picha. Ndio maana wakatoliki wanasali kwenye picha au sanamu iliyobarikiwa tuu kwa sababu Sanamu inapobarikiwa inaombewa uwepo wayule anayewakilishwa pale.

Tunafanya ishara ya msalaba kwenye sanamu kama sala ya utangulizi ambayo inathibitisha kuwa hatuabudu kile kilichoko pale bali kile tunachokifanya tunakifanya huku tukikiri Umungu na Heshima ya Utatu Mtakatifu (Mungu; Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.). Vile vile tunamtukuza Mungu katika Utatu Mtakatifu kwa sababu ya yule anayewakilishwa na picha au sanamu.

Kwa nini watu wanabusu picha na sanamu?


Hii ni ishara ya Upendo kwa yule anayewakilishwa kwenye picha au sanamu husika. Hata katika maisha ya kawaida watu hubusu picha za wazazi na wapendwa wao. Maana ni ile ile.







Mungu akiwa Roho, viungo ambavyo pengine anapewa vina maana gani?


Mungu akiwa Roho, viungo ambavyo pengine anapewa vinamaanisha tu sifa fulani: k.mf. macho ujuzi wake, mikono uwezo wake, mabawa ulinzi wake, n.k. β€œRoho haina mwili na mifupa” (Lk 24:39).







Je, ni halali kuheshimu sanamu?


Ndiyo, ni halali kuheshimu sanamu kama viwakilishi vya Yesu, Mama yake na watakatifu wake, ambao zinaleta sura zao.

Kwa msingi huo walimsihi Yesu β€œwaguse hata pindo la vazi lake tu. Na wote waliogusa wakaponywa kabisa” (Math 14:36).

β€œMimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu chochote il msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo” (Gal 6:14).

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Janet Mbithe (Guest) on March 23, 2024

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

David Ochieng (Guest) on March 21, 2024

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Anna Mahiga (Guest) on January 27, 2024

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Rose Lowassa (Guest) on May 28, 2023

Sifa kwa Bwana!

Moses Kipkemboi (Guest) on March 14, 2023

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

John Lissu (Guest) on February 18, 2023

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Rose Amukowa (Guest) on September 14, 2022

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Samson Mahiga (Guest) on January 31, 2022

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Nancy Akumu (Guest) on January 1, 2022

Wakati wa Mungu ni kamilifu

James Malima (Guest) on November 5, 2021

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Alice Mrema (Guest) on July 8, 2021

Neema na amani iwe nawe.

George Mallya (Guest) on June 17, 2021

Rehema hushinda hukumu

Elizabeth Mrope (Guest) on June 13, 2021

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Grace Mligo (Guest) on March 4, 2021

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

John Lissu (Guest) on January 6, 2021

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Philip Nyaga (Guest) on October 9, 2020

Katika imani, yote yanawezekana

Samson Mahiga (Guest) on August 6, 2020

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Moses Mwita (Guest) on July 14, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

James Malima (Guest) on April 14, 2020

Endelea kuwa na imani!

Anna Sumari (Guest) on December 13, 2019

Tumaini ni nanga ya roho

George Ndungu (Guest) on October 24, 2019

Baraka kwako na familia yako.

Sharon Kibiru (Guest) on September 23, 2019

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Edward Chepkoech (Guest) on June 8, 2019

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Patrick Akech (Guest) on May 27, 2019

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Chris Okello (Guest) on March 23, 2019

Mungu ni mwema, wakati wote!

Mary Kendi (Guest) on January 18, 2019

Dumu katika Bwana.

Betty Kimaro (Guest) on September 14, 2018

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Stephen Amollo (Guest) on September 11, 2018

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Frank Macha (Guest) on June 12, 2018

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Jacob Kiplangat (Guest) on March 13, 2018

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Wilson Ombati (Guest) on March 12, 2018

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Charles Mboje (Guest) on January 11, 2018

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

James Malima (Guest) on October 27, 2017

Nguvu hutoka kwa Bwana

Jane Malecela (Guest) on August 23, 2017

Mwamini katika mpango wake.

Frank Sokoine (Guest) on August 11, 2017

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Grace Njuguna (Guest) on June 7, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Frank Sokoine (Guest) on May 28, 2017

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Michael Mboya (Guest) on March 28, 2017

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

John Lissu (Guest) on December 24, 2016

Nakuombea πŸ™

David Musyoka (Guest) on October 12, 2016

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Richard Mulwa (Guest) on June 11, 2016

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Philip Nyaga (Guest) on February 6, 2016

Mwamini Bwana; anajua njia

Grace Wairimu (Guest) on February 4, 2016

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Margaret Mahiga (Guest) on January 8, 2016

Imani inaweza kusogeza milima

Kenneth Murithi (Guest) on December 27, 2015

Rehema zake hudumu milele

Francis Njeru (Guest) on September 18, 2015

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Thomas Mtaki (Guest) on September 6, 2015

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Edward Chepkoech (Guest) on September 1, 2015

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Vincent Mwangangi (Guest) on June 9, 2015

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Monica Nyalandu (Guest) on April 16, 2015

Mungu akubariki!

Related Posts

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi uadilifu wa kijamii na kupinga ubaguzi na ukosefu wa haki katika jamii?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi uadilifu wa kijamii na kupinga ubaguzi na ukosefu wa haki katika jamii?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi uadilifu wa kijamii na kupinga ubaguzi na ukosefu... Read More

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili? Ji... Read More

Mafundisho kuhusu Neema

Mafundisho kuhusu Neema

Read More
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu matakwa ya Mungu na mapenzi ya binadamu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu matakwa ya Mungu na mapenzi ya binadamu?

Kanisa Katoliki linatambua kuwa Mungu aliumba ulimwengu na binadamu kwa mapenzi yake, lakini pia ... Read More

Amri ya nne ya Mungu: Kuheshimu Wazazi

Amri ya nne ya Mungu: Kuheshimu Wazazi

Katika Amri ya nne ya Mungu tumeamriwa nini?Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu upendo na huruma?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu upendo na huruma?

Karibu kwenye makala yangu kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu upendo na huruma. Katika kanisa... Read More

Maswali yanayoulizwa sana kuhusu Ibada ya Kanisa Katoliki

Maswali yanayoulizwa sana kuhusu Ibada ya Kanisa Katoliki

Read More

Amri Kumi za Mungu: Mambo ya Msingi unayopaswa kufahamu

Amri Kumi za Mungu: Mambo ya Msingi unayopaswa kufahamu

Amri kumi za Mungu ni zipi?