Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

MASOMO YA MISA, MACHI 20, 2022: JUMAPILI YA 3 YA KWARESIMA

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1 - Kut. 3:1-8a, 13-15

Basi, Musa alikuwa akilichunga kunda la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpka mlima wa Mungu, hata Horebu. Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei. Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa. Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu. Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu.Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali.Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini? Mungu akamwambia Musa, Mimi niko ambaye niko, akasema, Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli; Mimi niko amenituma kwenu. Tena Mungu akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli maneno haya, Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu; hili ndilo jina langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata vizazi vyote.Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI - Zab. 103:1-4, 6-8, 11 (K) 8

(K) Bwana amejaa huruma na neema.Ee nafsi yangu umhimidi Bwana.Naam, vyote vilivyo ndani yanguVilihimidi jina lake takatifu.

Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,Wala usizisahau fadhili zake zote.

(K)Akusamehe maovu yako yote,Akuponya magonywa yako yote,Aukomboa uhai wako na kaburi,Akutia taji ya fadhili na rehema.

(K)

Bwana ndiye afanyaye mambo ya haki,Na hukumu kwa wote wanaoonewa.Alimjulisha Musa njia zake.Wana wa Israeli matendo yake. (K)

Bwana amejaa huruma na neema,Haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili.Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi,Kadiri ileile rehema zake ni kuu kwa wamchao. (K)

SOMO 2 - 1 Kor. 10:1-6, 10-12

Ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; wote wakabatizwa wawe na Musa katika wingu na katika bahari; wote wakala chakula kile kile cha roho; wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani.Wala msinung’unike kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO - Zab. 95:8

Msifanye migumu mioyo yenu; Lakini msikie sauti yake Bwana.

INJILI - Lk. 13:1-9

Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha Yesu habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichangaya damu yao na dhabihu zao. Akawajibu akawaambia.Je! Mwadahni ya kwamba Wagalilaya hao walikuwa wenye dhambi kuliko Wagalilaya wote, hata wakapatwa na mambo hayo? Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo. Au wale kumi na wanane, walioangukiwa na mnara huko Siloamu, ukawaua, mwadhani ya kwamb awao walikuwa wakosaji kuliko watu wote waliokaa Yerusalemu? Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate. Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu? Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi; nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate.Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Rose Lowassa Guest Jan 6, 2024
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Janet Wambura Guest Sep 5, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Nancy Akumu Guest Aug 21, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Elizabeth Mtei Guest May 9, 2023
Nakuombea 🙏
👥 Janet Mbithe Guest Jan 13, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 James Malima Guest Dec 14, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Alice Mrema Guest Sep 15, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Jane Muthui Guest Jul 27, 2022
Endelea kuwa na imani!
👥 Anthony Kariuki Guest Apr 26, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Nancy Komba Guest Apr 11, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Anna Mchome Guest Feb 11, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Jackson Makori Guest Feb 7, 2022
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 George Ndungu Guest Jan 8, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Betty Kimaro Guest Dec 19, 2021
Neema na amani iwe nawe.
👥 Mercy Atieno Guest Jul 9, 2021
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 James Kimani Guest May 23, 2021
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Andrew Odhiambo Guest May 16, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Ruth Wanjiku Guest Apr 11, 2021
Rehema hushinda hukumu
👥 Jane Malecela Guest Nov 16, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Elizabeth Malima Guest Aug 30, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 David Sokoine Guest Jun 24, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Richard Mulwa Guest Mar 7, 2020
Sifa kwa Bwana!
👥 Hellen Nduta Guest Dec 29, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Esther Cheruiyot Guest Nov 18, 2019
Rehema zake hudumu milele
👥 George Wanjala Guest Sep 16, 2019
Baraka kwako na familia yako.
👥 Mary Kendi Guest Aug 12, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 George Ndungu Guest Jun 17, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Benjamin Kibicho Guest Apr 13, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Frank Sokoine Guest Apr 10, 2019
Mwamini katika mpango wake.
👥 Joseph Mallya Guest Feb 15, 2019
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Michael Onyango Guest Nov 30, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Margaret Mahiga Guest Jun 24, 2018
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Lucy Kimotho Guest Jan 3, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Nora Kidata Guest Nov 30, 2017
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Irene Makena Guest Nov 30, 2017
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Andrew Mahiga Guest Oct 13, 2017
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Anna Sumari Guest Aug 28, 2017
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Lydia Mzindakaya Guest Aug 22, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
👥 John Malisa Guest Dec 10, 2016
Mungu akubariki!
👥 Mary Kidata Guest Sep 12, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Joyce Aoko Guest Jun 11, 2016
Dumu katika Bwana.
👥 Sharon Kibiru Guest May 25, 2016
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Emily Chepngeno Guest Nov 6, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 John Malisa Guest Nov 6, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Nancy Kawawa Guest Sep 24, 2015
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Lucy Mushi Guest Sep 14, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Edward Lowassa Guest Aug 16, 2015
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Moses Mwita Guest Jul 24, 2015
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Monica Adhiambo Guest Jun 12, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Carol Nyakio Guest Apr 17, 2015
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About