Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA,ย JUMAPILI, AGOSTI 20, 2023: JUMA LA 20 LA MWAKAย 

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO I

Isa. 56:1, 6-7

Bwana asema hivi, Shikeni hukumu, mkatenda haki; kwa maana wokovu wangu u karibu kuja, na haki yangu kufunuliwa. Na wageni, walioandamana na Bwana ili wamhudumu, na kulipenda jina la Bwana, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu; Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu

WIMBO WA KATIKATIย 

Zab. 67:1-2, 4-5, 7 (K) 5

(K) Watu na wakushukuru, Ee Mungu,ย 
Watu wote na wakushukuru.

Mungu na atufadhili na kutubariki,

na kutuangazia uso wake.
Njia yake ijulikane duniani,
wokovu wake katikati ya mataifa yote. (K)

mataifa na washangilia,

naam, waimbe kwa furaha.
Maana kwa haki utawahukumu watu,
na kuwaongoza mataifa walioko duniani. (K)

watu na wakushukuru, Ee Mungu,

watu wote na wakushukuru.
Mungu atatubariki sisi;
miisho yote ya dunia itamcha Yeye. (K)

SOMO 2

Rum. 11:13-15, 29-32

Nasema na ninyi, mlio watu wa Mataifa. Basi, kwa kadiri nilivyo mtume wa watu wa Mataifa. Basi, naitukuza huduma iliyo yangu? Huenda nikapata kuwapatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao. Maana ikiwa kutupwa kwao kumeleta upatanisho kwa ulimwengu, je! Kukubaliwa kwao kutakuwa nini kama si uhai baada ya kufa. Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake. Kwa maana kama ninyi zamani mlivyomwasi Mungu, lakini sasa mmepata rehema kwa kuasi kwao; kadhalika na hao wameasi sasa, ili kwa kupata rehema kwenu wao nao wapate rehema. Maana Mungu amewafunga wote pamoja katika kuasi ili awarehemu wote.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu

SHANGILIO

Mdo. 16:14


Aleluya, aleluya,

Fungua mioyo yetu, Ee Bwana,ย 
Ili tuyatuze maneno ya Mwanao.
Aleluya

INJILIย 

Mt. 15:21-28

Yesu aliondoka huko, akaenda kando pande za tiro na Sidoni. Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo. Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu. Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Naye akaja akamsujudia, akisema, Bwana unisaidie. Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao. Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Patrick Kidata Guest Mar 10, 2024
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Sarah Karani Guest Mar 4, 2024
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Moses Kipkemboi Guest Dec 27, 2023
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Edward Chepkoech Guest Oct 11, 2023
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Josephine Nduta Guest Apr 8, 2023
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Alice Mwikali Guest Jan 5, 2023
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Peter Otieno Guest Dec 5, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mahiga Guest Oct 15, 2022
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ David Chacha Guest Sep 9, 2022
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ John Malisa Guest Aug 17, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Sharon Kibiru Guest Jul 29, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Frank Macha Guest Jan 2, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Grace Wairimu Guest Oct 29, 2021
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Mary Kidata Guest Jun 4, 2021
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Violet Mumo Guest May 10, 2021
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Daniel Obura Guest Mar 17, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Nancy Kawawa Guest Dec 22, 2020
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest Sep 7, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Grace Majaliwa Guest Aug 21, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Linda Karimi Guest Aug 5, 2020
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Joseph Mallya Guest Jul 21, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Philip Nyaga Guest Jan 1, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ David Ochieng Guest Dec 7, 2019
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Jane Muthoni Guest Sep 8, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Stephen Malecela Guest Mar 27, 2019
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Nancy Kawawa Guest Mar 24, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ John Malisa Guest Mar 24, 2019
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Samuel Were Guest Mar 12, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Irene Makena Guest Mar 7, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ John Mushi Guest Feb 15, 2019
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Fredrick Mutiso Guest Dec 19, 2018
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Rose Mwinuka Guest Nov 18, 2018
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Majaliwa Guest Oct 13, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ John Lissu Guest Sep 9, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Victor Mwalimu Guest Aug 6, 2018
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Peter Mugendi Guest Jun 23, 2018
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Janet Mbithe Guest May 31, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Peter Mugendi Guest Apr 14, 2018
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Sharon Kibiru Guest Jan 13, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Alice Mrema Guest Nov 10, 2017
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Esther Nyambura Guest Oct 23, 2017
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Jane Muthui Guest Jul 26, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Grace Minja Guest Apr 13, 2017
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Richard Mulwa Guest Dec 23, 2016
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Rose Kiwanga Guest Nov 9, 2016
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Monica Adhiambo Guest Jul 4, 2016
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mchome Guest Mar 5, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Ruth Kibona Guest Dec 26, 2015
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Simon Kiprono Guest Dec 4, 2015
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Sarah Karani Guest Jul 8, 2015
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About