Sidebar with Floating Button
AckySHINE Katoliki
☰
AckyShine

MASOMO YA MISA,Β JUMAPILI, AGOSTI 27, 2023: JUMA LA 21 LA MWAKA

Featured Image

SOMO I





Isa. 22:19-23





Bwana, Bwana wa majeshi, asema hivi: Nami nitakusukuma na kukutoa katika mahali pako, naye atakushusha utoke hapa usimamapo. Na itakuwa katika siku ile nitamwita mtumishi wangu Eliakimu, mwana wa Hilkia; nami nitamvika vazi lako, nitamtia nguvu kwa mshipi wako, nami nitamkabidhi yeye mamlaka yako; naye atakuwa baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nvumba ya Yuda. Na ufunguo wa nvumba ya Daudi nitauweka begani mwake; yeye atafungua wala hapana atakayefunga. Nami nitamkaza kanta msumari mahali palipo imara; naye atakuwa kiti cha utukufu kwa nyumba ya baba yake.

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu





WIMBO WA KATIKATIΒ 





Zab. 138: 1-3, 6, 9 (K) 9





(K) Ee Bwana, fadhili zako ni za milele,Β 
Usiziache kazi za mikono yako.

Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,

Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu. (K)

Nitalishukuru jina lako,

Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,
Kwa maana umeikuza ahadi yako,
Kuliko jina lako lote.
Siku ile niliyokuita ulinitikia,
Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu. (K)

Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu,Β 

Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.
Ee Bwana, fadhili zako ni za milele;
Usiziache kazi za mikono yako. (K)





SOMO 2Β 





Rum 11: 33-36





Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani! Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake? Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena? Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.





Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu





SHANGILIO





Mt 11: 25





Aleluya, aleluya,
Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi,Β 
kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye
hekima na akili. ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya





INJILIΒ 





Ml 16:13-20





Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipo, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? Wakasema, Wengine hunena Yohane Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. Akawaa- mbia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia. Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikufunulia hili, bali Baba vangu aliye mbinguni. Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. Ndipo alipowakataza sana wanafunziΒ wake wasimwambie mtu ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.





Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo





Β 


AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Kevin Maina (Guest) on June 2, 2024

Neema na amani iwe nawe.

Grace Mligo (Guest) on February 22, 2024

Nakuombea πŸ™

Stephen Malecela (Guest) on December 19, 2023

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

James Malima (Guest) on August 18, 2023

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Nicholas Wanjohi (Guest) on July 17, 2023

Mungu ni mwema, wakati wote!

Grace Mligo (Guest) on January 21, 2023

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Vincent Mwangangi (Guest) on December 17, 2022

Rehema zake hudumu milele

Edwin Ndambuki (Guest) on July 2, 2022

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

David Kawawa (Guest) on May 22, 2022

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Philip Nyaga (Guest) on December 1, 2021

Nguvu hutoka kwa Bwana

Lucy Mushi (Guest) on March 8, 2021

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Lucy Mahiga (Guest) on February 1, 2021

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Margaret Mahiga (Guest) on January 7, 2021

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Charles Mboje (Guest) on January 1, 2021

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Emily Chepngeno (Guest) on December 23, 2020

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Philip Nyaga (Guest) on November 27, 2020

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Stephen Malecela (Guest) on November 1, 2020

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Alice Mrema (Guest) on August 15, 2020

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Henry Sokoine (Guest) on May 13, 2020

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Anna Kibwana (Guest) on April 30, 2020

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Jane Malecela (Guest) on April 17, 2020

Tumaini ni nanga ya roho

George Mallya (Guest) on February 4, 2020

Katika imani, yote yanawezekana

Henry Mollel (Guest) on January 12, 2020

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Patrick Mutua (Guest) on January 12, 2020

Dumu katika Bwana.

John Malisa (Guest) on December 28, 2019

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Stephen Malecela (Guest) on November 13, 2019

Endelea kuwa na imani!

Daniel Obura (Guest) on November 2, 2019

Mwamini Bwana; anajua njia

Joseph Njoroge (Guest) on February 24, 2019

Sifa kwa Bwana!

George Wanjala (Guest) on February 7, 2019

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Victor Kamau (Guest) on December 2, 2018

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Charles Mchome (Guest) on August 28, 2018

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Edward Chepkoech (Guest) on July 28, 2018

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Nora Lowassa (Guest) on March 14, 2018

Imani inaweza kusogeza milima

Margaret Mahiga (Guest) on November 7, 2017

Baraka kwako na familia yako.

Paul Kamau (Guest) on October 8, 2017

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Bernard Oduor (Guest) on September 17, 2017

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Patrick Kidata (Guest) on June 29, 2017

Mungu akubariki!

Anna Malela (Guest) on April 16, 2017

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Diana Mallya (Guest) on February 19, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Monica Nyalandu (Guest) on February 18, 2017

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Margaret Mahiga (Guest) on January 11, 2017

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Victor Mwalimu (Guest) on May 31, 2016

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Margaret Mahiga (Guest) on March 2, 2016

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Sarah Achieng (Guest) on February 11, 2016

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Fredrick Mutiso (Guest) on December 11, 2015

Rehema hushinda hukumu

David Kawawa (Guest) on December 1, 2015

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Samson Tibaijuka (Guest) on November 8, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Robert Ndunguru (Guest) on April 25, 2015

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Joyce Aoko (Guest) on April 14, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Anna Kibwana (Guest) on April 4, 2015

Mwamini katika mpango wake.

Related Posts

MASOMO YA MISA, JUNI 18, 2023: JUMAPILI, JUMA LA 11 LA MWAKA

MASOMO YA MISA, JUNI 18, 2023: JUMAPILI, JUMA LA 11 LA MWAKA

SOMO 1 

SHEREHE YA MT. YOSEFU, MUME WA BIKIRA MARIA

SOMO 1 - Kumb. 4:1, 5-9

... Read More

MASOMO YA MISA, APRILI 5, 2022: JUMANNE JUMA LA 5 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, APRILI 5, 2022: JUMANNE JUMA LA 5 LA KWARESIMA

SOMO 1

Hes. 21:4-9

Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya Shamu; i... Read More

MASOMO YA MISA,Β JUNI 25, 2023: JUMAPILI YA 12 YA MWAKA

MASOMO YA MISA,Β JUNI 25, 2023: JUMAPILI YA 12 YA MWAKA

SOMO 1

SOMO 1

Hos. 5... Read More

MASOMO YA MISA, MACHI 18, 2022:  IJUMAA, JUMA LA 2 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 18, 2022: IJUMAA, JUMA LA 2 LA KWARESIMA

SOMO 1

Mwa. 37:3-4, 12-13, 17-28

Β 

Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe ... Read More

MASOMO YA MISA, APRILI 1, 2022: IJUMAA, JUMA LA 4 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, APRILI 1, 2022: IJUMAA, JUMA LA 4 LA KWARESIMA

Β 

SOMO 1


Hek. 2:1, 12-22

Wasiomsadikia Mungu walisema hivi, huku wak... Read More

πŸ“˜ About πŸ”’ Login πŸ“ Register πŸ“ž Contact