Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, JULAI 26, 2021 JUMATATU, JUMA LA 17 LA MWAKA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Kut. 32:15-24, 30-34

Musa aligeuka akashuka katika mlima, na zile mbao mbili za mawe mikononi mwake; mbao ziliandikwa pande zote mbili, upande huu na upande huu ziliandikwa. Na zile mbao zilikuwa kazi ya Mungu, nayo maandiko yalikuwa maandiko ya Mungu, yaliyochorwa katika zile mbao.

Na Yoshua aliposikia kelele za watu walipokuwa wakipiga kelele, akamwambia Musa, Kuna kelele ya vita maragoni. Akasema, Hiyo si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushinda vitani, wala si sauti ya watu wapigao kelele kwa sababu ya kushindwa; bali kelele za watu waimbao nizo ninazozisikia mimi.

Hata alipyakaribia marago akaiona ile ndama, na ile michezo. Hasira ya Musa ikawaka, akazitupa zile mbao mikononi mwake, akazivunja chini ya mlima. Akaitwaa ile ndama walioifanya, akaichoma moto, akaisaga hata ikawa mavumbi, akainyunyiza juu ya maji, akawanywesha wana wa Israeli. Musa akamwambia Haruni; Watu hawa wamekufanyani hata ukaleta dhambi hii kuu juu yao? Haruni akasema, Hasira ya bwana wangu isiwake; wewe unawajua watu hawa, ya kuwa wamejielekeza kwa mabaya. Maana waliniambia, Katufanyie miungu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana mtu huyo Musa, aliyetutoa katika nchi ya Misri, hatujui yaliyompata. Nikawaambia, Mtu yeyote aliye na dhahabu na aivunje; basi wakanipa, nami nikaitupa ndani ya moto, akatoka ndama huyu.

Basi asubuhi yake Musa akawaambia watu, Mmetenda dhambi kuu; na sasa nitakwenda juu kwa Bwana, labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu. Musa akarejea kwa Bwana akasema, Aa! Watu hawa wametenda dhambi kuu, wamejifanyia miungu ya dhahabu. Walakini sasa ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichokiandika. Bwana akamwambia Musa, Mtu yoyote aliyenitenda dhambi, ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu. Basi sasa uende ukawaongoze watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekuambia habari zake; tazama, malaika wangu atakutangulia; pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi yao.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 106:19-23 (K) 1

(K) Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema.

Walifanya ndama huko Horebu,

Wakaisujudia sanamu ya kuyeyuka.

Wakaubadili utukufu wao,

Kuwa mfano wa ng’ombe mla majani. (K)

Wakamsahau Mungu, mwokozi wao,

Aliyetenda makuu katika Misri.

Matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu,

Mambo ya kutisha penye bahari ya Shamu. (K)

Akasema ya kuwa atawaangamiza,

Kama Musa, mteule wake, asingalisimama,

Mbele zake kama mahali palipobomoka,

Ili aigeuze hasira yake asije akawaharibu. (K)

SHANGILIO

Efe. 1:17, 18

Aleluya, aleluya,

Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristu, awape roho ya hekima mjue tumaini la mwito wake.

Aleluya.

INJILI

Mt. 13:31 – 35

Yesu aliwatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake; nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.

Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia.

Hayo yote Yesu aliwaambia makutano kwa mifano; wala pasipo mfano hakuwaambia neno; ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, Nitayatamka yaliyositirika tangu awali.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Jun 25, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest Apr 21, 2024
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Mar 8, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Jan 7, 2024
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Dec 15, 2023
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest Jul 3, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest May 24, 2023
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Mary Mrope Guest Jan 24, 2023
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Jan 3, 2023
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Chris Okello Guest Dec 18, 2022
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Nov 1, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Jan 25, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Dec 16, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Nov 4, 2021
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ John Lissu Guest Oct 7, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Aug 30, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Aug 30, 2021
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Aug 13, 2021
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Jul 11, 2021
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Jun 28, 2021
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Apr 5, 2021
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Edward Lowassa Guest Feb 22, 2021
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Dec 3, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Alice Jebet Guest Nov 30, 2020
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Aug 30, 2020
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Aug 16, 2020
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest May 15, 2020
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Andrew Mahiga Guest Apr 20, 2020
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Jan 27, 2020
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Jan 15, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Janet Wambura Guest Dec 6, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Jun 21, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Mar 30, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ David Ochieng Guest Mar 20, 2019
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Nov 11, 2018
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Sep 7, 2018
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Jul 25, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ George Mallya Guest Jul 17, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Faith Kariuki Guest Feb 22, 2018
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Sep 27, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest Aug 13, 2017
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Aug 8, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Samuel Were Guest May 2, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Apr 19, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Feb 12, 2017
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Jun 19, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Mar 2, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Feb 20, 2016
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Nov 18, 2015
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Jun 22, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About