MASOMO YA MISA, MACHI 23, 2022: JUMATANO JUMA LA 3 LA KWARESI
SOMO 1 - Kumb. 4:1, 5-9
Musa aliwaambia makutano: Ee Israeli, zisikilizeni amri na hukumu niwafundishazo, ili mmzitende; mpate kuishi na kuingia na kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wa baba zenu.
Angalieni nimewafundisha amri na hukumu, vile vile kama Bwana, Mungu wangu, alivyoniamuru, ili mzitende katika nchi mwmingiayo ili kuimiliki. Zishikeni basi, mkazitende, maana hii ndiyo hekima yenu na akili zenu, machoni pa mataifa watakaozisikia amri hizi zote, nao watasema, Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na akili. Kwa maana liko taifa gani kubwa, lililo na Mungu aliye karibu nao, kama Bwana, Mungu wetu, alivyo, kila tumwitapo? Tena liko taifa gani kubwa, lililo na amri na hukumu zenye haki kama torati hii yote, ninayoiweka mbele yenu leo.
Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa watoto wako.
Neno la Bwana⦠Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI - Zab. 147:12-13, 15-16, 19-20 (K) 12
(K) Msifu Bwana, Ee Yerusalemu.
Msifu Bwana, Ee Yerusalemu;
Msifu Mungu wako, Ee Sayuni.
Maana ameyakaza mapingo ya malango yako,
Amewabariki wanao ndani yako. (K)
Huipeleka amri yake juu ya nchi,
Neno lake lapiga mbio sana.
Ndiye atoaye theluji kama sufu,
Huimwaga barafu yake kama majivu. (K)
Humhubiri Yakobo neno lake,
Na Israeli amri zake na hukumu zake.
Hakulitendea taifa lolote mambo kama hayo,
Wala hukumu zake hawakuzijua. (K)
SHANGILIO
Mbegu neno la Mungu, mpanzi lakini ni Kristu; Yeyote ampataye, ataishi milele.
INJILI - Mt. 5:17-19
Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Msidhani kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme mbinguni.
Neno la Bwana⦠Sifa kwako Ee Kristo.
Ruth Wanjiku (Guest) on June 23, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
Robert Okello (Guest) on April 23, 2024
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Victor Kimario (Guest) on April 23, 2024
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Lucy Mushi (Guest) on June 12, 2023
Mungu ni mwema, wakati wote!
Lydia Mzindakaya (Guest) on June 8, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
John Lissu (Guest) on February 10, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Philip Nyaga (Guest) on January 30, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
Peter Mugendi (Guest) on January 6, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Stephen Amollo (Guest) on December 20, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Rose Mwinuka (Guest) on October 27, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Francis Mtangi (Guest) on June 26, 2022
Endelea kuwa na imani!
Joseph Mallya (Guest) on June 23, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Joseph Njoroge (Guest) on June 2, 2022
Baraka kwako na familia yako.
Henry Sokoine (Guest) on February 19, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
Margaret Mahiga (Guest) on December 30, 2021
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Diana Mumbua (Guest) on September 19, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mary Njeri (Guest) on September 7, 2021
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Alice Jebet (Guest) on August 25, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Violet Mumo (Guest) on April 5, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
Janet Sumaye (Guest) on February 2, 2020
Rehema hushinda hukumu
Irene Akoth (Guest) on January 5, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Ruth Mtangi (Guest) on October 2, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
Wilson Ombati (Guest) on September 27, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Joseph Njoroge (Guest) on August 12, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Linda Karimi (Guest) on July 25, 2019
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Carol Nyakio (Guest) on July 2, 2019
Dumu katika Bwana.
Frank Macha (Guest) on February 20, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Irene Akoth (Guest) on December 28, 2018
Mungu akubariki!
Thomas Mwakalindile (Guest) on June 18, 2018
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Janet Wambura (Guest) on March 20, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Carol Nyakio (Guest) on March 10, 2018
Nakuombea π
Moses Mwita (Guest) on March 6, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Margaret Anyango (Guest) on October 2, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Isaac Kiptoo (Guest) on September 3, 2017
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Rose Mwinuka (Guest) on June 24, 2017
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Raphael Okoth (Guest) on March 17, 2017
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Alex Nakitare (Guest) on January 19, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Josephine Nekesa (Guest) on August 25, 2016
Neema na amani iwe nawe.
Irene Akoth (Guest) on July 6, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Betty Kimaro (Guest) on June 27, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Nancy Kabura (Guest) on May 6, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Janet Mwikali (Guest) on April 24, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Andrew Odhiambo (Guest) on April 23, 2016
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
David Musyoka (Guest) on April 12, 2016
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Samson Mahiga (Guest) on February 6, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mercy Atieno (Guest) on January 22, 2016
Sifa kwa Bwana!
Peter Mbise (Guest) on December 22, 2015
Tumaini ni nanga ya roho
James Malima (Guest) on December 11, 2015
Mwamini katika mpango wake.
Anthony Kariuki (Guest) on November 3, 2015
Rehema zake hudumu milele
James Mduma (Guest) on April 27, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona