SOMO 1
Β
Dan.13:41-62
Β
Palikuwa na mtu mmoja jina lake Yoakimu, akikaa Babeli, naye ameoa mke jina lake Susana binti Helkia, mwanamke mzuri sana na mcha Mungu. Wazee wake nao walikuwa wenye haki, pia wamemfundisha binti yao sawasawa na Torati ya Musa. Basi Yoakimu alikuwa mwungwana tajiri, na karibu na nyumba yake alikuwa na bustani nzuri; hivyo Wayahudi humwendea, maana alikuwa ni mwenye heshima kupita wengineo wote. Mwaka ule ule wakaamriwa wawili miongoni mwa wazee wa watu ili kuamua, watu wa namna ile ambao Bwana aliwanena, ya kama ufisadi ulitoka Babeli kwa wazee waamuzi waliohesabiwa kuwa wanatawala watu. Hao walikuwa wakienda mara nyingi kuzuru kwenye nyumba yake Yoakimu; na wote wenye mashtaka yoyote desturi yao wakawajia huko. Basi watu walipoondoka kwenda zao panapo saa sita, Susana huingia katika bustani ya mumewe ili kutembea. Nao wale wazee humwona kila siku anakwenda kutembea; hata wakawaka tamaa kwa sababu yake. Ndipo walipozipotosha nia zao, wakayageuza upande macho yao wasiweze kutazama mbinguni wala kukumbuka hukumu za haki. Ikawa walipongoja wakati wa kufaa, yeye aliingia bustanini kama ilivyokuwa desturi yake pamoja na wajakazi wawili, naye alitaka kuoga kwa sababu kulikuwa na joto. Wala hapakuwa na mtu yeyote isipokuwa wale wazee wawili, ambao wamejificha wakimvizia. Basi akawaambia wajakazi wake, Nileteeni mafuta na sabuni, mkaifunge milango ya bustani ili nioge . Mara wale wajakazi walipokwishas kutoka, wale wazee wawili waliondoka wakamwendea mbio, wakasema, Tazama, milango ya bustani imefungwa asiweze kutuona mtu yeyote nasi tunakupenda sana; haya! Basi, utukubali na ulale nasi. La! Hutaki tutakushuhudia ya kuwa hapa palikuwapo na kijana pamoja nawe, ndiyo sababu uliwaruhusu wajakazi wako. Basi Susana aliugua akasema, Nimesongwa pande zote, maana nikilitenda hilo ni mauti yangu; nisipolitenda siwezi kuokoka mikononi mwenu. Ni afadhali niangukie katika mikono yenu na kukataa, kuliko kutenda dhambi machoni pa Mungu. Mara Susana akapiga kelele kwa sauti kuu; nao wale wazee wawili wakampigia kelele pia. Kisha mmoja wao akakimbia, akaifungua milango ya bustani. Hivyo watumishi wa nyumbani waliposikia kelele bustanini, wao waliingia kwa kasi kwa mlango wa nyuma ili waone ni nini iliyompata. Lakini wale wazee waliisimulia hadith yao nao watumishi wakaona aibu kabisa, kwa maana Susana hakuchongelewa habari ya namna hiyo wakati wowote.
Ikawa kesho yake watu walipokusanyika kwa Yoakimu mumewe, wale wazee wawili wakaja nao, wamejaa kusudi lao ovu juu ya Susana la kumfisha. Wakasema mbele ya watu, "Mwiteni Susana binti Helkia, mkewe Yoakim, aje hapa". Basi akaenda kuitwa; naye akaja pamoja na baba yake na mama yake, na watoto wake, na jamaa zake wote. Naye huyo Susana alikuwa mwanamke mwenye adabu, mzuri wa uso; basi hao watu wabaya waliamuru afunuliwe uso, maana alifunikwa utaji, ili washibe uzuri wake. Kwa hiyo rafiki zake na wote waliomtazama wakasikitika. Ndipo wale wazee wawili waliposimama katikati ya watu, wakaweka mikono yao juu ya kichwa chake. Naye akatoka machozi, akatazama juu mbinguni, kwa maana moyo wake ulimtumaini Mungu. Wale wazee wakasema, Sisi tulipokuwa tukitembea bustanini peke yetu, huyu aliingia pamoja na wajakazi wawili, wakaifunga milango ya bustani, naye mara akawaruhusu wajakazi. Kisha kukatokea kijana, ambaye amejificha humo, akamwendea akalala naye. Walakini sisi tungaliko pembeni mwa bustani, tuliona ubaya huo, tukamwendea mbio. Hata tukiwa tumewaona pamoja, yule kijana hatukuweza kumkamata, maana alikuwa mwenye nguvu kuliko sisi, akifungua milango akaepuka. Bali huyu tulimkamata, tukauliza yule kijana yu nani, asikubali kutuambia. Hayo basi, tunashuhudu. Basi waliohudhuria wakawasadiki, wakiwa wazee wa watu na waamuzi; hivyo wakahukumu auawe. Mara Susana akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Mungu wa milele, Wewe wajua yaliyositirika, wajua mambo yote yasijekuwako, Wewe wajua ya kwamba wananishuhudia uongo, na tazama, imenipasa kufa; walakini sikufanya mambo kama hayo, ambayo watu hawa wameyabuni juu yangu kwa ukorofi.
Naye Bwana akaisikia sauti yake. Kwa hiyo, alipochukuliwa huyo kwenda kuuawa, Mungu alimchocheleza roho kijana mmoja, jina lake Danieli; naye akapaza sauti akasema, Mimi simo; mimi sina hatia kwa habari ya damu yake mwanamke huyu. Mara wote wakamgeukia, wakasema, Maneno hayo uyasemayo, maana yake nini? Akasimama katikati, akasema, Enyi bani Israeli, mmekuwa wapumbavu, hata kumhukumu binti Israeli bila kuhoji wala kupata hakika ya kweli? Rudini hukumuni; mradi hao wanamshuhudia uongo.
Basi watu wote walirejea kwa haraka, nao wale wazee wakamwambia, Njoo uketi kati yetu, utujulishe habari hiyo, endapo Mungu amekupa wewe heshima yam zee. Hapo Danieli aliwaambia, Watu hawa wawili watengwe, nami nitawahoji. Basi wakiisha kutengwa, akamwita mmoja wao akamwambia, Ewe uliyepata kuwa mzee katika uovu, sasa dhambi zako zimekukalia, ulizozitenda zamani kwa kuhukumu isivyo haki, kumpatiliza asiye na hatia na kumwachilia mwovu; lakini Bwana asema, Asiye na hatia, mwenye haki, usimwue. Haya! Basi, wewe ulimwona kwa macho; useme; Chini ya mti gani ulipowaona wakikaa pamoja? Naye akajibu, Chini ya msandarusi. Danieli akasema, Hakika umesema uongo juu ya kichwa chako mwenyewe; maana sas hivi malaika wa Mungu amepokea hukumu ya Mungu, akukate vipande viwili. akamtenga huyo tena, akaamuru kumleta yule mwingine, akamwambia, Ewe mzao wa Kanaani, wala si wa Yuda, uzuri umekudanganya, na tamaa imeupotosha moyo wako. Hivyo ndivyo ulivyowafanyia binti za Israeli, na kwa hofu walitembea nawe; bali huyu binti Yuda hakuweza kuustahimili uovu wako. Haya! Basi, nawe useme; Chini ya mti gani ulipowaona wakikaa pamoja? Naye akajibu, Chini ya mkwaju. Danieli akamwambia, Hakika wewe nawe umesema uongo juu ya kichwa chako mwenyewe; maana malaika wa Mungu yu tayari, anakungoja mwenye upanga, akukate vipande viwili; ili awaangamize nyote wawili.
Mara hiyo makusanyiko yote wakapaza sauti kwa nguvu, wakamhimidi Mungu awaokoaye wamtumainio. Wakawaondokea wale wazee wawili, kwa maana Danieli ameuhakikisha ushuhuda wao wa uongo hata vinywani mwao wenyewe. Wakawatenda kwa Torati ya Musa kama vile walivyokusudia kwa ukorofi kumfanyia jirani yao; wakawaua; na mwenye damu isiyo na hatia aliokolewa siku ile.
Β
Neno la Bwana⦠Tumshukuru Mungu.
Β
WIMBO WA KATIKATI
Β
Zab. 23 (K) 4
Β
(K) Nijapopita katika bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami.
Β
Bwana ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza. (K)
Β
Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza,
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
Naam, nijapopita kati aya bonde la uvuli wa mauti
Sitaogopa mabaya; kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (K)
Β
Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe change kinafurika. (K)
Β
Hakika wema na fadhili zinanifuata,
Siku zote za maisha yangu,
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. (K)
Β
SHANGILIO
Β
Yn. 6:64, 69
Β
Maneno yako, Ee Bwana, ni roho, tena ni uzima, Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.
Β
INJILI
Β
Yn. 8:12-20
Β
Yesu aliwaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
Basi Mafarisayo wakamwambia, Wewe unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako si kweli.
Yesu akajibu, akawaambia, Mimi ningawa ninajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ndio kweli; kwa sababu najua nilikotoka na niendako; lakini ninyi hamjui nilikotoka wala niendako. Ninyi mwahukumu kwa kufuata mambo ya mwili; mimi simhukumu mtu. Nami nijapohukumu, hukumu yangu ni kweli; kwa kuwa mimi si peke yangu, bali ni mimi nay eye aliyenipeleka. Tena katika torati yenu imeandikwa kwamba, Ushuhuda wa watu wawili ni kweli. Mimi ndimi ninayejishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenipeleka ananishuhudia.
Basi wakamwambia, Yuko wapi Baba yako? Yesu akajibu, Mimi hamnijui, wala Baba yangu hammjui kama mngalinijijua mimi, mngalimjua na Baba yangu.
Maneno hayo aliyasema alipokuwa akifundisha hekaluni, katika chumba cha hazina; wala hakuna mtu aliyemkamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.
Β
Neno la Bwana⦠Sifa kwako Ee Kristo.
Rose Mwinuka (Guest) on July 12, 2024
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Carol Nyakio (Guest) on July 1, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Joseph Kiwanga (Guest) on March 2, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Lydia Mzindakaya (Guest) on January 19, 2024
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Sarah Achieng (Guest) on October 5, 2023
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Catherine Mkumbo (Guest) on March 12, 2023
Dumu katika Bwana.
Sharon Kibiru (Guest) on January 6, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Ann Awino (Guest) on January 1, 2023
Rehema hushinda hukumu
Mary Mrope (Guest) on December 23, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
Patrick Akech (Guest) on October 28, 2022
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Betty Kimaro (Guest) on October 28, 2022
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Mary Sokoine (Guest) on September 7, 2022
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Benjamin Masanja (Guest) on August 7, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mary Mrope (Guest) on March 14, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Lydia Mzindakaya (Guest) on December 18, 2021
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Hellen Nduta (Guest) on December 13, 2021
Imani inaweza kusogeza milima
Kenneth Murithi (Guest) on May 4, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Rose Waithera (Guest) on June 22, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Moses Kipkemboi (Guest) on June 4, 2020
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Miriam Mchome (Guest) on January 27, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mercy Atieno (Guest) on January 1, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
John Mwangi (Guest) on November 27, 2019
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Susan Wangari (Guest) on November 25, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
Anna Malela (Guest) on July 30, 2019
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
James Kawawa (Guest) on June 23, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Grace Wairimu (Guest) on April 24, 2019
Neema na amani iwe nawe.
Ruth Mtangi (Guest) on January 17, 2019
Mwamini katika mpango wake.
Elijah Mutua (Guest) on August 15, 2018
Neema ya Mungu inatosha kwako
Dorothy Nkya (Guest) on July 18, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Peter Mwambui (Guest) on June 8, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
George Wanjala (Guest) on May 20, 2018
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Anna Malela (Guest) on April 20, 2018
Sifa kwa Bwana!
David Chacha (Guest) on March 31, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
David Sokoine (Guest) on March 19, 2018
Rehema zake hudumu milele
Benjamin Masanja (Guest) on December 13, 2017
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Alice Mrema (Guest) on June 27, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Daniel Obura (Guest) on March 22, 2017
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Kevin Maina (Guest) on March 19, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Joseph Kitine (Guest) on February 16, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rose Kiwanga (Guest) on July 4, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
John Kamande (Guest) on June 30, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Margaret Anyango (Guest) on April 30, 2016
Mwamini Bwana; anajua njia
David Nyerere (Guest) on January 31, 2016
Baraka kwako na familia yako.
Nora Kidata (Guest) on January 28, 2016
Mungu akubariki!
Joseph Njoroge (Guest) on January 20, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
Rose Mwinuka (Guest) on October 12, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Nicholas Wanjohi (Guest) on October 6, 2015
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Janet Sumari (Guest) on September 30, 2015
Nakuombea π
Richard Mulwa (Guest) on September 11, 2015
Endelea kuwa na imani!
Mercy Atieno (Guest) on May 20, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha