Sidebar with Floating Button
AckySHINE Katoliki
☰
AckyShine

MASOMO YA MISA, APRILI 4, 2022: JUMATATU, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

Featured Image

SOMO 1

Β 

Dan.13:41-62

Β 

Palikuwa na mtu mmoja jina lake Yoakimu, akikaa Babeli, naye ameoa mke jina lake Susana binti Helkia, mwanamke mzuri sana na mcha Mungu. Wazee wake nao walikuwa wenye haki, pia wamemfundisha binti yao sawasawa na Torati ya Musa. Basi Yoakimu alikuwa mwungwana tajiri, na karibu na nyumba yake alikuwa na bustani nzuri; hivyo Wayahudi humwendea, maana alikuwa ni mwenye heshima kupita wengineo wote. Mwaka ule ule wakaamriwa wawili miongoni mwa wazee wa watu ili kuamua, watu wa namna ile ambao Bwana aliwanena, ya kama ufisadi ulitoka Babeli kwa wazee waamuzi waliohesabiwa kuwa wanatawala watu. Hao walikuwa wakienda mara nyingi kuzuru kwenye nyumba yake Yoakimu; na wote wenye mashtaka yoyote desturi yao wakawajia huko. Basi watu walipoondoka kwenda zao panapo saa sita, Susana huingia katika bustani ya mumewe ili kutembea. Nao wale wazee humwona kila siku anakwenda kutembea; hata wakawaka tamaa kwa sababu yake. Ndipo walipozipotosha nia zao, wakayageuza upande macho yao wasiweze kutazama mbinguni wala kukumbuka hukumu za haki. Ikawa walipongoja wakati wa kufaa, yeye aliingia bustanini kama ilivyokuwa desturi yake pamoja na wajakazi wawili, naye alitaka kuoga kwa sababu kulikuwa na joto. Wala hapakuwa na mtu yeyote isipokuwa wale wazee wawili, ambao wamejificha wakimvizia. Basi akawaambia wajakazi wake, Nileteeni mafuta na sabuni, mkaifunge milango ya bustani ili nioge . Mara wale wajakazi walipokwishas kutoka, wale wazee wawili waliondoka wakamwendea mbio, wakasema, Tazama, milango ya bustani imefungwa asiweze kutuona mtu yeyote nasi tunakupenda sana; haya! Basi, utukubali na ulale nasi. La! Hutaki tutakushuhudia ya kuwa hapa palikuwapo na kijana pamoja nawe, ndiyo sababu uliwaruhusu wajakazi wako. Basi Susana aliugua akasema, Nimesongwa pande zote, maana nikilitenda hilo ni mauti yangu; nisipolitenda siwezi kuokoka mikononi mwenu. Ni afadhali niangukie katika mikono yenu na kukataa, kuliko kutenda dhambi machoni pa Mungu. Mara Susana akapiga kelele kwa sauti kuu; nao wale wazee wawili wakampigia kelele pia. Kisha mmoja wao akakimbia, akaifungua milango ya bustani. Hivyo watumishi wa nyumbani waliposikia kelele bustanini, wao waliingia kwa kasi kwa mlango wa nyuma ili waone ni nini iliyompata. Lakini wale wazee waliisimulia hadith yao nao watumishi wakaona aibu kabisa, kwa maana Susana hakuchongelewa habari ya namna hiyo wakati wowote.

Ikawa kesho yake watu walipokusanyika kwa Yoakimu mumewe, wale wazee wawili wakaja nao, wamejaa kusudi lao ovu juu ya Susana la kumfisha. Wakasema mbele ya watu, "Mwiteni Susana binti Helkia, mkewe Yoakim, aje hapa". Basi akaenda kuitwa; naye akaja pamoja na baba yake na mama yake, na watoto wake, na jamaa zake wote. Naye huyo Susana alikuwa mwanamke mwenye adabu, mzuri wa uso; basi hao watu wabaya waliamuru afunuliwe uso, maana alifunikwa utaji, ili washibe uzuri wake. Kwa hiyo rafiki zake na wote waliomtazama wakasikitika. Ndipo wale wazee wawili waliposimama katikati ya watu, wakaweka mikono yao juu ya kichwa chake. Naye akatoka machozi, akatazama juu mbinguni, kwa maana moyo wake ulimtumaini Mungu. Wale wazee wakasema, Sisi tulipokuwa tukitembea bustanini peke yetu, huyu aliingia pamoja na wajakazi wawili, wakaifunga milango ya bustani, naye mara akawaruhusu wajakazi. Kisha kukatokea kijana, ambaye amejificha humo, akamwendea akalala naye. Walakini sisi tungaliko pembeni mwa bustani, tuliona ubaya huo, tukamwendea mbio. Hata tukiwa tumewaona pamoja, yule kijana hatukuweza kumkamata, maana alikuwa mwenye nguvu kuliko sisi, akifungua milango akaepuka. Bali huyu tulimkamata, tukauliza yule kijana yu nani, asikubali kutuambia. Hayo basi, tunashuhudu. Basi waliohudhuria wakawasadiki, wakiwa wazee wa watu na waamuzi; hivyo wakahukumu auawe. Mara Susana akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Mungu wa milele, Wewe wajua yaliyositirika, wajua mambo yote yasijekuwako, Wewe wajua ya kwamba wananishuhudia uongo, na tazama, imenipasa kufa; walakini sikufanya mambo kama hayo, ambayo watu hawa wameyabuni juu yangu kwa ukorofi.

Naye Bwana akaisikia sauti yake. Kwa hiyo, alipochukuliwa huyo kwenda kuuawa, Mungu alimchocheleza roho kijana mmoja, jina lake Danieli; naye akapaza sauti akasema, Mimi simo; mimi sina hatia kwa habari ya damu yake mwanamke huyu. Mara wote wakamgeukia, wakasema, Maneno hayo uyasemayo, maana yake nini? Akasimama katikati, akasema, Enyi bani Israeli, mmekuwa wapumbavu, hata kumhukumu binti Israeli bila kuhoji wala kupata hakika ya kweli? Rudini hukumuni; mradi hao wanamshuhudia uongo.

Basi watu wote walirejea kwa haraka, nao wale wazee wakamwambia, Njoo uketi kati yetu, utujulishe habari hiyo, endapo Mungu amekupa wewe heshima yam zee. Hapo Danieli aliwaambia, Watu hawa wawili watengwe, nami nitawahoji. Basi wakiisha kutengwa, akamwita mmoja wao akamwambia, Ewe uliyepata kuwa mzee katika uovu, sasa dhambi zako zimekukalia, ulizozitenda zamani kwa kuhukumu isivyo haki, kumpatiliza asiye na hatia na kumwachilia mwovu; lakini Bwana asema, Asiye na hatia, mwenye haki, usimwue. Haya! Basi, wewe ulimwona kwa macho; useme; Chini ya mti gani ulipowaona wakikaa pamoja? Naye akajibu, Chini ya msandarusi. Danieli akasema, Hakika umesema uongo juu ya kichwa chako mwenyewe; maana sas hivi malaika wa Mungu amepokea hukumu ya Mungu, akukate vipande viwili. akamtenga huyo tena, akaamuru kumleta yule mwingine, akamwambia, Ewe mzao wa Kanaani, wala si wa Yuda, uzuri umekudanganya, na tamaa imeupotosha moyo wako. Hivyo ndivyo ulivyowafanyia binti za Israeli, na kwa hofu walitembea nawe; bali huyu binti Yuda hakuweza kuustahimili uovu wako. Haya! Basi, nawe useme; Chini ya mti gani ulipowaona wakikaa pamoja? Naye akajibu, Chini ya mkwaju. Danieli akamwambia, Hakika wewe nawe umesema uongo juu ya kichwa chako mwenyewe; maana malaika wa Mungu yu tayari, anakungoja mwenye upanga, akukate vipande viwili; ili awaangamize nyote wawili.

Mara hiyo makusanyiko yote wakapaza sauti kwa nguvu, wakamhimidi Mungu awaokoaye wamtumainio. Wakawaondokea wale wazee wawili, kwa maana Danieli ameuhakikisha ushuhuda wao wa uongo hata vinywani mwao wenyewe. Wakawatenda kwa Torati ya Musa kama vile walivyokusudia kwa ukorofi kumfanyia jirani yao; wakawaua; na mwenye damu isiyo na hatia aliokolewa siku ile.

Β 

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

Β 

WIMBO WA KATIKATI

Β 

Zab. 23 (K) 4

Β 

(K) Nijapopita katika bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami.

Β 

Bwana ndiye mchungaji wangu,

Sitapungukiwa na kitu.

Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,

Kando ya maji ya utulivu huniongoza. (K)

Β 

Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza,

Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

Naam, nijapopita kati aya bonde la uvuli wa mauti

Sitaogopa mabaya; kwa maana Wewe upo pamoja nami,

Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (K)

Β 

Waandaa meza mbele yangu,

Machoni pa watesi wangu.

Umenipaka mafuta kichwani pangu,

Na kikombe change kinafurika. (K)

Β 

Hakika wema na fadhili zinanifuata,

Siku zote za maisha yangu,

Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. (K)

Β 

SHANGILIO

Β 

Yn. 6:64, 69

Β 

Maneno yako, Ee Bwana, ni roho, tena ni uzima, Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.

Β 

INJILI

Β 

Yn. 8:12-20

Β 

Yesu aliwaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.

Basi Mafarisayo wakamwambia, Wewe unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako si kweli.

Yesu akajibu, akawaambia, Mimi ningawa ninajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ndio kweli; kwa sababu najua nilikotoka na niendako; lakini ninyi hamjui nilikotoka wala niendako. Ninyi mwahukumu kwa kufuata mambo ya mwili; mimi simhukumu mtu. Nami nijapohukumu, hukumu yangu ni kweli; kwa kuwa mimi si peke yangu, bali ni mimi nay eye aliyenipeleka. Tena katika torati yenu imeandikwa kwamba, Ushuhuda wa watu wawili ni kweli. Mimi ndimi ninayejishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenipeleka ananishuhudia.

Basi wakamwambia, Yuko wapi Baba yako? Yesu akajibu, Mimi hamnijui, wala Baba yangu hammjui kama mngalinijijua mimi, mngalimjua na Baba yangu.

Maneno hayo aliyasema alipokuwa akifundisha hekaluni, katika chumba cha hazina; wala hakuna mtu aliyemkamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.

Β 

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Rose Mwinuka (Guest) on July 12, 2024

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Carol Nyakio (Guest) on July 1, 2024

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Joseph Kiwanga (Guest) on March 2, 2024

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Lydia Mzindakaya (Guest) on January 19, 2024

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Sarah Achieng (Guest) on October 5, 2023

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Catherine Mkumbo (Guest) on March 12, 2023

Dumu katika Bwana.

Sharon Kibiru (Guest) on January 6, 2023

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Ann Awino (Guest) on January 1, 2023

Rehema hushinda hukumu

Mary Mrope (Guest) on December 23, 2022

Mungu ni mwema, wakati wote!

Patrick Akech (Guest) on October 28, 2022

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Betty Kimaro (Guest) on October 28, 2022

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Mary Sokoine (Guest) on September 7, 2022

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Benjamin Masanja (Guest) on August 7, 2022

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Mary Mrope (Guest) on March 14, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Lydia Mzindakaya (Guest) on December 18, 2021

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Hellen Nduta (Guest) on December 13, 2021

Imani inaweza kusogeza milima

Kenneth Murithi (Guest) on May 4, 2021

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Rose Waithera (Guest) on June 22, 2020

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Moses Kipkemboi (Guest) on June 4, 2020

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Miriam Mchome (Guest) on January 27, 2020

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Mercy Atieno (Guest) on January 1, 2020

Kwa Mungu, yote yanawezekana

John Mwangi (Guest) on November 27, 2019

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Susan Wangari (Guest) on November 25, 2019

Tumaini ni nanga ya roho

Anna Malela (Guest) on July 30, 2019

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

James Kawawa (Guest) on June 23, 2019

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Grace Wairimu (Guest) on April 24, 2019

Neema na amani iwe nawe.

Ruth Mtangi (Guest) on January 17, 2019

Mwamini katika mpango wake.

Elijah Mutua (Guest) on August 15, 2018

Neema ya Mungu inatosha kwako

Dorothy Nkya (Guest) on July 18, 2018

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Peter Mwambui (Guest) on June 8, 2018

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

George Wanjala (Guest) on May 20, 2018

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Anna Malela (Guest) on April 20, 2018

Sifa kwa Bwana!

David Chacha (Guest) on March 31, 2018

Katika imani, yote yanawezekana

David Sokoine (Guest) on March 19, 2018

Rehema zake hudumu milele

Benjamin Masanja (Guest) on December 13, 2017

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Alice Mrema (Guest) on June 27, 2017

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Daniel Obura (Guest) on March 22, 2017

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Kevin Maina (Guest) on March 19, 2017

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Joseph Kitine (Guest) on February 16, 2017

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Rose Kiwanga (Guest) on July 4, 2016

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

John Kamande (Guest) on June 30, 2016

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Margaret Anyango (Guest) on April 30, 2016

Mwamini Bwana; anajua njia

David Nyerere (Guest) on January 31, 2016

Baraka kwako na familia yako.

Nora Kidata (Guest) on January 28, 2016

Mungu akubariki!

Joseph Njoroge (Guest) on January 20, 2016

Nguvu hutoka kwa Bwana

Rose Mwinuka (Guest) on October 12, 2015

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Nicholas Wanjohi (Guest) on October 6, 2015

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Janet Sumari (Guest) on September 30, 2015

Nakuombea πŸ™

Richard Mulwa (Guest) on September 11, 2015

Endelea kuwa na imani!

Mercy Atieno (Guest) on May 20, 2015

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Related Posts

MASOMO YA MISA, APRILI 2, 2022: JUMAMOSI: JUMA LA 4 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, APRILI 2, 2022: JUMAMOSI: JUMA LA 4 LA KWARESIMA

SOMO 1

Β 

Yer. 11:18-20

Β 

Bwana akanijulisha haya, nami nikayajua; n... Read More

MASOMO YA MISA, APRILI 1, 2022: IJUMAA, JUMA LA 4 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, APRILI 1, 2022: IJUMAA, JUMA LA 4 LA KWARESIMA

Β 

SOMO 1


Hek. 2:1, 12-22

Wasiomsadikia Mungu walisema hivi, huku wak... Read More

MASOMO YA MISA,Β JUMAPILI, AGOSTI 20, 2023: JUMA LA 20 LA MWAKAΒ 

MASOMO YA MISA,Β JUMAPILI, AGOSTI 20, 2023: JUMA LA 20 LA MWAKAΒ 

SOMO IRead More

MASOMO YA MISA, JUNI 04, 2023: SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU - Jumapili baada ya Pentekoste

MASOMO YA MISA, JUNI 04, 2023: SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU - Jumapili baada ya Pentekoste

MWANZO:

SOMO 1

2 Fal.... Read More

MASOMO YA MISA, MEI 21, 2023:<br>DOMINIKA YA 7 YA PASAKA<br>SHEREHE YA KUPAA BWANA

MASOMO YA MISA, MEI 21, 2023:<br>DOMINIKA YA 7 YA PASAKA<br>SHEREHE YA KUPAA BWANA

MWANZO:
Mdo. 1:11