SOMO 1
Yer. 17:5-10
Bwana asema hivi: Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake, na moyoni mwake amemwacha Bwana. Maana atakuwa kama fukara nyikani, hataona yatakapotokea mema; bali atakaa jangwani palipo na ukame, katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.
Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, ambaye Bwana ni tumaini lake. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, uenezao mizizi yake karibu na mto; hautaona hofu wakati wa hari ujapo, bali jani lake litakuwa bichi; wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, wala hautaacha kuzaa matunda.
Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua? Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.
Neno la Bwana⦠Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 1:1-4, 6 (K) 40:4
(K) Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake.
Heri mtu yule asiyekwenda
Katika shauri la wasio haki;
Wala hakusimama katika njia ya wakosaji;
Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo,
Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. (K)
Naye atakuwa kama mti uliopandwa
Kandokando ya vijito vya maji,
Uzaao matunda yake kwa majira yake,
Wala jani lake halinyauki;
Na kila alitendalo litafanikiwa. (K)
Sivyo walivyo wasio haki;
Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Kw akuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki,
Bali njia ya wasio haki itapotea. (K)
SHANGILIO
Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako.
INJILI
Lk. 16:19-31
Yesu aliwaambia Mafarisayo: Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa. Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake. Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.
Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu. Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.
Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu, kwa kuwaninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao piawakafika mahali hapa pa mateso. Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao. Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea atokaye kwa wafu, watatubu. Akamwambia wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.
Neno la Bwana⦠Sifa kwako Ee Kristo.
Andrew Mahiga (Guest) on December 22, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Peter Tibaijuka (Guest) on November 27, 2023
Baraka kwako na familia yako.
Lucy Kimotho (Guest) on October 7, 2023
Mwamini Bwana; anajua njia
Grace Majaliwa (Guest) on October 5, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
John Malisa (Guest) on June 18, 2023
Mungu akubariki!
Francis Mrope (Guest) on November 30, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Thomas Mwakalindile (Guest) on September 26, 2022
Neema na amani iwe nawe.
Ruth Mtangi (Guest) on August 8, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Rose Mwinuka (Guest) on July 30, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Elizabeth Malima (Guest) on May 1, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Hellen Nduta (Guest) on February 26, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Andrew Mchome (Guest) on September 21, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Joy Wacera (Guest) on September 17, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Ruth Kibona (Guest) on September 6, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Richard Mulwa (Guest) on September 4, 2021
Katika imani, yote yanawezekana
Janet Mwikali (Guest) on July 20, 2021
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Moses Mwita (Guest) on July 13, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Andrew Mchome (Guest) on April 23, 2021
Rehema zake hudumu milele
Edwin Ndambuki (Guest) on March 17, 2021
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Josephine Nekesa (Guest) on March 4, 2021
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Janet Mwikali (Guest) on January 23, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Janet Mwikali (Guest) on November 29, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Nicholas Wanjohi (Guest) on July 18, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Elizabeth Mtei (Guest) on June 20, 2020
Rehema hushinda hukumu
Samuel Were (Guest) on June 13, 2020
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Joyce Mussa (Guest) on December 24, 2019
Sifa kwa Bwana!
Stephen Amollo (Guest) on April 17, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
James Kawawa (Guest) on April 16, 2019
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Grace Mushi (Guest) on February 17, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
James Malima (Guest) on December 18, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mercy Atieno (Guest) on November 25, 2018
Endelea kuwa na imani!
Simon Kiprono (Guest) on January 22, 2018
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Faith Kariuki (Guest) on November 29, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Charles Mchome (Guest) on September 11, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Joseph Kawawa (Guest) on June 22, 2017
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Paul Kamau (Guest) on June 13, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Grace Minja (Guest) on May 10, 2017
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Joyce Nkya (Guest) on March 19, 2017
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Victor Malima (Guest) on January 3, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Victor Sokoine (Guest) on October 24, 2016
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Dorothy Nkya (Guest) on October 22, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Catherine Mkumbo (Guest) on September 18, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Sarah Karani (Guest) on August 15, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
Peter Mwambui (Guest) on August 4, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
Alice Mrema (Guest) on July 22, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Stephen Amollo (Guest) on June 18, 2016
Mungu ni mwema, wakati wote!
Anna Sumari (Guest) on April 3, 2016
Mwamini katika mpango wake.
Anna Mahiga (Guest) on January 17, 2016
Neema ya Mungu inatosha kwako
Lydia Wanyama (Guest) on December 27, 2015
Dumu katika Bwana.
Diana Mallya (Guest) on November 27, 2015
Nakuombea π