Sidebar with Floating Button
AckySHINE Katoliki
☰
AckyShine

MASOMO YA MISA, MACHI 17, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 2 LA KWARESIMA

Featured Image

SOMO 1


Yer. 17:5-10


Bwana asema hivi: Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake, na moyoni mwake amemwacha Bwana. Maana atakuwa kama fukara nyikani, hataona yatakapotokea mema; bali atakaa jangwani palipo na ukame, katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, ambaye Bwana ni tumaini lake. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, uenezao mizizi yake karibu na mto; hautaona hofu wakati wa hari ujapo, bali jani lake litakuwa bichi; wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, wala hautaacha kuzaa matunda.

Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua? Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI


Zab. 1:1-4, 6 (K) 40:4


(K) Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake.

Heri mtu yule asiyekwenda

Katika shauri la wasio haki;

Wala hakusimama katika njia ya wakosaji;

Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo,

Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. (K)

Naye atakuwa kama mti uliopandwa

Kandokando ya vijito vya maji,

Uzaao matunda yake kwa majira yake,

Wala jani lake halinyauki;

Na kila alitendalo litafanikiwa. (K)

Sivyo walivyo wasio haki;

Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

Kw akuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki,

Bali njia ya wasio haki itapotea. (K)

SHANGILIO


Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako.

INJILI


Lk. 16:19-31


Yesu aliwaambia Mafarisayo: Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa. Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake. Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu. Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.

Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu, kwa kuwaninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao piawakafika mahali hapa pa mateso. Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao. Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea atokaye kwa wafu, watatubu. Akamwambia wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Andrew Mahiga (Guest) on December 22, 2023

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Peter Tibaijuka (Guest) on November 27, 2023

Baraka kwako na familia yako.

Lucy Kimotho (Guest) on October 7, 2023

Mwamini Bwana; anajua njia

Grace Majaliwa (Guest) on October 5, 2023

Nguvu hutoka kwa Bwana

John Malisa (Guest) on June 18, 2023

Mungu akubariki!

Francis Mrope (Guest) on November 30, 2022

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Thomas Mwakalindile (Guest) on September 26, 2022

Neema na amani iwe nawe.

Ruth Mtangi (Guest) on August 8, 2022

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Rose Mwinuka (Guest) on July 30, 2022

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Elizabeth Malima (Guest) on May 1, 2022

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Hellen Nduta (Guest) on February 26, 2022

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Andrew Mchome (Guest) on September 21, 2021

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Joy Wacera (Guest) on September 17, 2021

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Ruth Kibona (Guest) on September 6, 2021

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Richard Mulwa (Guest) on September 4, 2021

Katika imani, yote yanawezekana

Janet Mwikali (Guest) on July 20, 2021

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Moses Mwita (Guest) on July 13, 2021

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Andrew Mchome (Guest) on April 23, 2021

Rehema zake hudumu milele

Edwin Ndambuki (Guest) on March 17, 2021

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Josephine Nekesa (Guest) on March 4, 2021

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Janet Mwikali (Guest) on January 23, 2021

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Janet Mwikali (Guest) on November 29, 2020

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Nicholas Wanjohi (Guest) on July 18, 2020

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Elizabeth Mtei (Guest) on June 20, 2020

Rehema hushinda hukumu

Samuel Were (Guest) on June 13, 2020

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Joyce Mussa (Guest) on December 24, 2019

Sifa kwa Bwana!

Stephen Amollo (Guest) on April 17, 2019

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

James Kawawa (Guest) on April 16, 2019

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Grace Mushi (Guest) on February 17, 2019

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

James Malima (Guest) on December 18, 2018

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Mercy Atieno (Guest) on November 25, 2018

Endelea kuwa na imani!

Simon Kiprono (Guest) on January 22, 2018

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Faith Kariuki (Guest) on November 29, 2017

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Charles Mchome (Guest) on September 11, 2017

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Joseph Kawawa (Guest) on June 22, 2017

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Paul Kamau (Guest) on June 13, 2017

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Grace Minja (Guest) on May 10, 2017

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Joyce Nkya (Guest) on March 19, 2017

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Victor Malima (Guest) on January 3, 2017

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Victor Sokoine (Guest) on October 24, 2016

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Dorothy Nkya (Guest) on October 22, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Catherine Mkumbo (Guest) on September 18, 2016

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Sarah Karani (Guest) on August 15, 2016

Imani inaweza kusogeza milima

Peter Mwambui (Guest) on August 4, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

Alice Mrema (Guest) on July 22, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Stephen Amollo (Guest) on June 18, 2016

Mungu ni mwema, wakati wote!

Anna Sumari (Guest) on April 3, 2016

Mwamini katika mpango wake.

Anna Mahiga (Guest) on January 17, 2016

Neema ya Mungu inatosha kwako

Lydia Wanyama (Guest) on December 27, 2015

Dumu katika Bwana.

Diana Mallya (Guest) on November 27, 2015

Nakuombea πŸ™

Related Posts

MASOMO YA MISA,Β JUNI 25, 2023: JUMAPILI YA 12 YA MWAKA

MASOMO YA MISA,Β JUNI 25, 2023: JUMAPILI YA 12 YA MWAKA

SOMO 1

SOMO IRead More

MASOMO YA MISA, MACHI 28, 2022:
 JUMATATU: JUMA LA 4 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 28, 2022: JUMATATU: JUMA LA 4 LA KWARESIMA

SOMO 1

Isa. 65:17-21

Β 

Bwana asema: Tazama, mimi naumba mbingu mpya na nch... Read More

MASOMO YA MISA, APRILI 1, 2023: JUMAMOSI, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

SOMO 1

SOMO 1 - Kut. 3:1-8a, 13-15

... Read More
MASOMO YA MISA, APRILI 4, 2022: JUMATATU, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, APRILI 4, 2022: JUMATATU, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

SOMO 1

Β 

Dan.13:41-62

Β 

Palikuwa na mtu mmoja jina lake Yoakimu, ak... Read More

MASOMO YA MISA, MACHI 21, 2022: JUMATATU , JUMA LA 3 LA KWARESIMA

MASOMO YA MISA, MACHI 21, 2022: JUMATATU , JUMA LA 3 LA KWARESIMA

SOMO 1

2 Fal.... Read More

MASOMO YA MISA, APRILI 2, 2023: DOMINIKA YA MATAWI

SOMO 1

SOMO 1 

SOMO 1